Nchimbi atambika kwenye kaburi la Gama

Nchimbi atambika kwenye kaburi la Gama

- Sasa ina maana kaka umekata tamaa kabisa na kushika Dola sasa unawalilia watu wa CCM, saafi sana nilidhani utalilia chama chako sasa unamlilia Lowassa saafi sana!!, chezea CCM wewe!!

Le Mutuz

Mkuu sijakata tamaa ila ni Lowasa tu na namuunga mkono kama hupendi saga chupa ubwie. Ni nani alikudanganya mimi ni chadema? Hii ni zamu yetu sasa kaeni chonjo vibaraka wote.
 
Mkuu sijakata tamaa ila ni Lowasa tu na namuunga mkono kama hupendi saga chupa ubwie. Ni nani alikudanganya mimi ni chadema? Hii ni zamu yetu sasa kaeni chonjo vibaraka wote.

kaka hapo kwenye red...wew ndo unaikana chadema leo???au ndo tuamini ni matokeo ya njaa za mjini..lol!!!!!
 
kaka hapo kwenye red...wew ndo unaikana chadema leo???au ndo tuamini ni matokeo ya njaa za mjini..lol!!!!!
Mkuu kuna kundi linaitwa Friends of Lowassa, pesa ikishatembea watu watawakana hata mama zao.
 
candind scope, unachanganya mambo Sana mkuu, kiukwel wale wanakijiji waliamishwa enzi za nyerere, na si mwinyi, chuki ya wanalituhi ilijotokeza kutokana na hilo na kubaliana nawewe, lakini ikumbukwe mareheme mzee gama, aliwasaidia pia Kama Una data ulizia miaka kazaa baada ya kuamishwa Yale mafuriko wamesahau??, kuhusu marehemu mzee gama na askofu Komba, ikumbukwe wakat gama anakuja songea alishatumikia nyazifa kazaa Kama mkurugenz wa idara, jkt, rc Dodoma, na baada ya kuondoka ruvuma then tabora, katibu mkuu wa chama, hadi Leo hajawahi jitokeza jembe Kama gama ruvuma na ndio rc alietoboa miaka mingi pale....kifo cha yafunani, ikumbukwe siku za mwisho za uhai wake afya Yake haikuwa nzuri, hili tukio lisihusishwe na gama, natural death ile......
 

Attachments

  • 1391549596090.jpg
    1391549596090.jpg
    40.3 KB · Views: 74
Last edited by a moderator:
Mkuu hao vijana (nawaita vijana kwa vile ni wadogo kwangu) huwa wanasahau kule walikotoka.
Mwaka 2005 nimekutana nao wote pale joint ya Mbunge fulani Morogoro, hata ukiwasalimia ilikuwa nyodo kwa kwenda mbele, ingawaje katika shula za msingi tulizo soma walikuwa hata kindergatten hawajaanza.
Nimekutana tena na Kamala kwenye ndege pale Kigali miezi kadhaa iliyopita(baada ya kumwagwa uwaziri), sasa ndo wanaanza kuguktuka kusalimia kila mtu.


Cheo ni dhamana , ukikipata kwa dhuluma utawadharau wengine kwa kujiona mjanja. Lakini matatizo yakikurudisha kwa waswahili wale wale ulioowaacha , ni kuomba radhi tu, hasa kwa wale mtu uliowaumiza.
Kutambika makaburini, hilo litakuwa kwa maagizo ya waganga, na huo ni ushirikina.

Katika siasa matawi ya juu is only temporary!

Sijui kama hawa wadogo wetu wanatambua kama cheo ni dhamana kwamba leo ni Juma kesho ni John! Na hasa hivi vyeo vya kisiasa. Wangekua wanajua hilo wasingekua wanatumia uhuni kupata madaraka na wakiondolewa wasinge ona nongwa na kuanza kumtafuta mchawi.

Ni tatizo la kitaifa kuanzia ktk vyama vya siasa,serikalini na taasisi za umma na binafsi. Pengine tumeshindwa kutengeneza viongozi. Vijana wanatakiwa kutumia mfano wa akina Nchimbi kutambua kwamba njia za mkato ni sumu ya mafanikio endelevu!
 
Mkuu......nakuomba umuache Mzee Gama (RIP) apumzike kwa amani.......usiandike mambo kwa kusimuliwa kuhusu sera za serikali za wakati huo kuhusu vijiji vya ujamaa......



Hapa simjadilia Gama, ila ni yatokanayo ndani ya habari tunayojadili kuhusu Nchimbi kwa vile maisha yake ya kisiasa vigumu kuyatenganisha na mikikimikiki iliyofanywa na Nchimbi kumwangusha Gama kwenye kinyang'anyiro cha ubunge, na baada ya hapo Kikwete alipoingia madarakani ndio akashindilia msumari kwa kumwondoa ukuu wa mkoa alikokuwa Morogoro.

Laurence Mtazama Gama alikwua rafiki yangu ingawa nilikuwa mdogo. Gama ana sifa nzuri zaidi kuliko mbaya tunavyofikiria.
  • Alikuwa mchangamfu na mcheshi sana na mpenda kutabasamu
  • Alionekana muda wote ni mkakamavu sana si legelege
  • Alikuwa very social
  • Mpenda maendeleo
  • Mpenda michezo
  • Mhamasishaji mzuri
  • Mwenye kujituma
  • Mshauri
  • Mtoaji bila kinyongo
  • Hakuwa mbaguzi
  • Alijishusha kwa ye yote kuwa karibu naye
  • Alijituma sana kwa chama chake CCM
  • Popote alipoenda hakushindwa uongozi
  • Regional block ya Tabora iliyododa kwa miaka Gama alipifika alimaliza kwa muda mfupi tu, nk.

Michazo:
  1. Alijenga uwanja wa Majimaji
  2. Aliimarisha uwanja wa Lipuli Iringa
  3. Alijenga uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora

Timu kuwa alizoanzisha
  • Timu ya Lipuli Iringa hadi Daraja la kwanza (ligi kuu)
  • Timu ya Majimaji Songea Daraja la kwanza (Ligi Kuu) Ilitwaa ubingwa wa Jamhuri mara mbili Kibadeni akiwa ndani
  • Timu ya Milambo Tabora Daraja la Kwanza (Ligi Kuu)

Udhaifu wake:
Hakuwa tayari kulamba miguu ya mtu, ujue Gama ni kutoka familia ya kichifu, hakuwa na tatizo na watu wa kawaida kwa vile alikuwa very social, ila wakubwa waliotaka awatetemekee hakuwa tayari ndio maana hakubahatika kupata nafasi ya uongozi ngazi ya taifa. Wengi walipendekeza na kumtakia awe walao waziri wa michezo kutokana na mlolongo wa mengi aliyofanya kuhusu michezo lakini waliokuwa marais hawakuwa tayari kwa vile hakuwa tayari kuinama chini ya uvungu wa vitanda vyao na ndicho walichoshindana na hayati Askofu Mkuu Yakobo Yefunani Komba.

CCM alimtupa bila kujali mchango wake muhimu
Licha ya Gama kufikia hatua ya Katibu Mkuu wa CCM, kujenga viwanja vikubwa viwili nchini Majimaji na Ali Hassan Mwinyi vilivyomilikiwa na CCM hadi kuwapatia mapato mazuri ya makusanyo ya michezo, lakini hatimaye alitupwa kama ganda la ndizi baada ya kufaidi yaliyokuwamo ndani ya ganda hilo.
 
What goes around comes around. Nchimbi sasa ajichimbie jimboni kwake tu kwani huku nje keshajichimbia kaburi baada ya kusimamia watanzania wenzake wakiuawa na jeshi la polisi wakati yeye ndie aliyekuwa bosi wa wizara husika.


NO PERMANENT SITUATION.
 
Back
Top Bottom