field marshall1
JF-Expert Member
- Sep 17, 2017
- 1,594
- 3,606
Nilisoma kwenye gazeti la Kiswahili kuwa gavana wa Banki kuu Prof. Florens Luoga akisema uchumi wetu unakua vizuri na tuna akiba kubwa ya USD 5.0 Billions na hii itatosha kuendesha nchi kwa miezi mitano bila ya nchi kukusanya kodi au watu kufanya kazi, siku hiyo hiyo Rais Magufuli akatamka maneno hayo hayo.
Ninamfahamu Prof. Luoga kama mwalimu wangu na mkuu wa Chuo wakati nikisoma, nilimuona kama mtu mwenye credibility kubwa kwenye jamii ila kilichonishangaza aidha kwa kutojua au kwa makusudi alinishangaza aliposema kuwa hiyo akiba ya fedha za kigeni ni kubwa kuliko akiba ya nchi za Africa Mashariki! Ilishangaza sana.....
Sikutaka kushangaa zaidi hivyo nilienda kwenye website ya Central Bank of Kenya na kuangalia reserve ya siku hiyo.
Kifupi tu ni kwamba hatujawahi kuwa na akiba kubwa ya pesa za kigeni kuishinda Kenya kwa sababu Kenya wana tax base kubwa na kodi zao zinalipika tofauti na kwetu ambapo ni wachache tu wanaolipa kodi lakini wanakamuliwa kodi kubwa zisizolipika.
Namwelewa Dr. Patrick Ngugi Njoroge (Gavana wa Central Bank of Kenya) kama mtu makini sana, mchumi mzuri wa IMF, si hivyo tu huyu gavana pia kwa kiasi kikubwa aliaminika na Umoja wa Mataifa hadi kuchaguliwa mwenyekiti wa U.N Task force ya mambo ya Digital Financing ya SDG mwaka jana akiwa bado Gavana...Ningeweza kumfananisha na Prof. Assad kwa uchapaji kazi wake au kama Prof. Benno Ndullu kabla ya kuchanganya professional yake na siasa!
Wakati gavana wetu, Prof. Luoga mwalimu wangu wa Tax Law akisema tunayo akiba kubwa ya kutosha miezi mitano bila kufanya kazi ya USD Billions 5.0 niliamua kucheki akiba waliyonayo wenzetu wa kaskazini kwetu, Kenya. Akiba waliyonaya Kenya kwenye Banki kuu yao ilikuwa USD. 8.8 Billions na haijawahi kushuka kufika Billioni 7 au chini, sisi akiba yetu ya miezi mitano haijawahi kuvuka USD 5.8 Billions kwa kipindi tajwa sasa leo professor wa Tax Law na gavana wa banki kuu atasema vipi kitu ambacho si sahihi??? Leo tutamwamini vipi mtu kama huyo? Hata mtoto wa darasa la kwanza hawezi kushindwa kujua ipi ni kubwa kati ya 5 na 8.8!
Je ni utamaduni wetu kudanganya?
Katika kipindi hiki tangu aingie rais Magufuli mbona Propaganda zimekuwa nyingi...Kuna kitu wanaficha au wanataka wasifiwe hata kama hawastahili sifa? Sijasema wakati wa Kikwete hakukuwa na hizi propaganda, la hasha zilikuwepo ila hazikuwa nyingi hivi na za kijinga jinga kama za wakati huu, Sishangai kusikia rais mwenyewe alijifanya kushangaa kutekwa kwa Mo Dewji na wazungu wabantu na sarakasi nyingi na maigizo mengi yaliyofuata baadaye.
Ukienda Youtube utakutana na propaganda za akina Musiba anachoongea hakina sense ila ni comedy...Akili ndogo zinazoendelea kumtuma akaongee senseless zinashangilia. Akitukana, kuchafua wengine, kuropoka nk kwa hao anaonekana shujaa. Kweli Taifa letu limepotea!
Mambo madogo madogo ya “Dr. Shika” yanapewa kipaumbele.......watu wanasahau mambo ya msingi kuhusu maisha ya watanzania. Madawa hayapo, yaliyopo aidha yameisha muda wake au hayafai kwa matumizi ya binadamu (Refer: Report ya CAG), bajeti ya afya imetekelezwa kwa asilimia chini ya 40, bajeti ya dawa kwa asilimia 16. Wao wanapelekwa India, Africa kusini na nchi nyingine vipi Watanzania kama mimi na wewe ambao baba na babu zetu hawakuwa na nafasi serikalini....Si tutaishia hospitali za wilaya ambazo kwanza kulazwa hapo unatoka na ugonjwa mwingine, badala ya kupona unapata magonjwa mengine? Ni nini kinashindwa kuboresha huduma za afya angalau zikafanywa universal, tukose mengine yote lakini tuwe na haki ya kuishi?
Nchi ni yetu sote, Watanzania tuna akili za kuweza kutambua tunakoelekea, leo hii uchumi wetu unaenda kwenye asilimia 4 kutoka 7.2% halafu watu na akili zao watakwambia ni kitu cha kawaida kwa vile hata Marekani uchumi wake unakua kwa asilimia 2....Kweli hata akili za utambuzi mdogo tu hakuna? Ni wapi wamesikia uchumi wa nchi za dunia ya kwanza unakuwa kwa asilimia 7? wasomi wetu wanashindwa kuelewa hata hilo..Ndiyo maana wajenzi wa TBA kwenye hosteli za Chuo Kikuu walisema kuwa eti ile mipasuko ya kuta Expansion joint.....Sawa ni expansion joint sasa ilikuwaje mlikimbilia kuziziba?
Inabidi tuangalie kama elimu yetu inatosha na inasaidia kunyanyua taifa letu maana yanayofanyika sasa yanashangaza.
Ninamfahamu Prof. Luoga kama mwalimu wangu na mkuu wa Chuo wakati nikisoma, nilimuona kama mtu mwenye credibility kubwa kwenye jamii ila kilichonishangaza aidha kwa kutojua au kwa makusudi alinishangaza aliposema kuwa hiyo akiba ya fedha za kigeni ni kubwa kuliko akiba ya nchi za Africa Mashariki! Ilishangaza sana.....
Sikutaka kushangaa zaidi hivyo nilienda kwenye website ya Central Bank of Kenya na kuangalia reserve ya siku hiyo.
Kifupi tu ni kwamba hatujawahi kuwa na akiba kubwa ya pesa za kigeni kuishinda Kenya kwa sababu Kenya wana tax base kubwa na kodi zao zinalipika tofauti na kwetu ambapo ni wachache tu wanaolipa kodi lakini wanakamuliwa kodi kubwa zisizolipika.
Namwelewa Dr. Patrick Ngugi Njoroge (Gavana wa Central Bank of Kenya) kama mtu makini sana, mchumi mzuri wa IMF, si hivyo tu huyu gavana pia kwa kiasi kikubwa aliaminika na Umoja wa Mataifa hadi kuchaguliwa mwenyekiti wa U.N Task force ya mambo ya Digital Financing ya SDG mwaka jana akiwa bado Gavana...Ningeweza kumfananisha na Prof. Assad kwa uchapaji kazi wake au kama Prof. Benno Ndullu kabla ya kuchanganya professional yake na siasa!
Wakati gavana wetu, Prof. Luoga mwalimu wangu wa Tax Law akisema tunayo akiba kubwa ya kutosha miezi mitano bila kufanya kazi ya USD Billions 5.0 niliamua kucheki akiba waliyonayo wenzetu wa kaskazini kwetu, Kenya. Akiba waliyonaya Kenya kwenye Banki kuu yao ilikuwa USD. 8.8 Billions na haijawahi kushuka kufika Billioni 7 au chini, sisi akiba yetu ya miezi mitano haijawahi kuvuka USD 5.8 Billions kwa kipindi tajwa sasa leo professor wa Tax Law na gavana wa banki kuu atasema vipi kitu ambacho si sahihi??? Leo tutamwamini vipi mtu kama huyo? Hata mtoto wa darasa la kwanza hawezi kushindwa kujua ipi ni kubwa kati ya 5 na 8.8!
Je ni utamaduni wetu kudanganya?
Katika kipindi hiki tangu aingie rais Magufuli mbona Propaganda zimekuwa nyingi...Kuna kitu wanaficha au wanataka wasifiwe hata kama hawastahili sifa? Sijasema wakati wa Kikwete hakukuwa na hizi propaganda, la hasha zilikuwepo ila hazikuwa nyingi hivi na za kijinga jinga kama za wakati huu, Sishangai kusikia rais mwenyewe alijifanya kushangaa kutekwa kwa Mo Dewji na wazungu wabantu na sarakasi nyingi na maigizo mengi yaliyofuata baadaye.
Ukienda Youtube utakutana na propaganda za akina Musiba anachoongea hakina sense ila ni comedy...Akili ndogo zinazoendelea kumtuma akaongee senseless zinashangilia. Akitukana, kuchafua wengine, kuropoka nk kwa hao anaonekana shujaa. Kweli Taifa letu limepotea!
Mambo madogo madogo ya “Dr. Shika” yanapewa kipaumbele.......watu wanasahau mambo ya msingi kuhusu maisha ya watanzania. Madawa hayapo, yaliyopo aidha yameisha muda wake au hayafai kwa matumizi ya binadamu (Refer: Report ya CAG), bajeti ya afya imetekelezwa kwa asilimia chini ya 40, bajeti ya dawa kwa asilimia 16. Wao wanapelekwa India, Africa kusini na nchi nyingine vipi Watanzania kama mimi na wewe ambao baba na babu zetu hawakuwa na nafasi serikalini....Si tutaishia hospitali za wilaya ambazo kwanza kulazwa hapo unatoka na ugonjwa mwingine, badala ya kupona unapata magonjwa mengine? Ni nini kinashindwa kuboresha huduma za afya angalau zikafanywa universal, tukose mengine yote lakini tuwe na haki ya kuishi?
Nchi ni yetu sote, Watanzania tuna akili za kuweza kutambua tunakoelekea, leo hii uchumi wetu unaenda kwenye asilimia 4 kutoka 7.2% halafu watu na akili zao watakwambia ni kitu cha kawaida kwa vile hata Marekani uchumi wake unakua kwa asilimia 2....Kweli hata akili za utambuzi mdogo tu hakuna? Ni wapi wamesikia uchumi wa nchi za dunia ya kwanza unakuwa kwa asilimia 7? wasomi wetu wanashindwa kuelewa hata hilo..Ndiyo maana wajenzi wa TBA kwenye hosteli za Chuo Kikuu walisema kuwa eti ile mipasuko ya kuta Expansion joint.....Sawa ni expansion joint sasa ilikuwaje mlikimbilia kuziziba?
Inabidi tuangalie kama elimu yetu inatosha na inasaidia kunyanyua taifa letu maana yanayofanyika sasa yanashangaza.