Hivi mtu ili awe mwanachuoni inabidi awe na sifa gani?
1️⃣ Asome sana na kwa muda mrefu kwa wanachuoni wenye kusifika kwa fani mbalimbali za elimu ya uislamu na lugha ya kiarabu, itikadi sahihi , maadili sahihi, sunna sahihi na tabia njema zilizochukuliwa katika mafunzo sahihi ya Mtume Muhammad
صلى الله عليه وآله و سلم.
2️⃣Yeye mwenyewe akiisha soma ayafanyie kazi yale aliyojifunza kwa wanachuoni wa zama zake na wale waliopita kabla yake( asiwe miongoni mwa wale masheikh waovu wanaowaambia watu kwamba fuateni maneno yangu mazuri na msiangalie vitendo vyangu vibaya) kwa hiyo anatakiwa kujipamba na kusifika kwa sifa zote za elimu sahihi ,tabia njema, itikadi sahihi , lugha ya kiarabu na sunna sahihi zilizotolewa katika hadithi sahihi za mtume Muhammad
صلى الله عليه وسلم.
3️⃣Akishasoma yeye pia asomeshe sana wengine elimu sahihi, itikadi sahihi na maadili sahihi na kwa muda mrefu kiasi kwamba wanachuoni wa zama zake na wale watakaokuja baada yake wajiridhishe na wathibitishe kuwa yeye ni mwanachuoni.
4️⃣ Sheikh ambaye
(A) Masheikh zake hawajulikani (haijulikani kasoma wapi!)
(B) Wanafunzi wake hawajulikani!. (haijulikani elimu aliyosoma kaifanyia nini!)
(C) Vitabu vyake havijulikani. .
(D) Itikadi (A'qiyda) yake haijulikani.
(E) Madhehebu yake hayajulikani.
(F) Msimamo, maadili na mienendo yake haijulikani.
(G) Ikiwa chochote kilichotajwa hapo juu kati ya A, B, D, E, na F hakijulikani!
HUYO SIYO MWANACHUONI!