Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,850
- 62,285
Nimepita katika mitaa kadhaa ya jiji la dar es salaam.
Nilichokiona kinasikitisha, Mitaa michafu, watu wamekondeana, fremu zimefungwa na zilizofunguliwa wateja ni wa kuhesabu.
Ukizunguuka ukaenda kwa wauza chipsi mafuta wameyachomea chipsi wameyarudia hata mara tano yamekuwa meusi tiii, wanakwambia brother hali ni ngumu hatuwezi kumwaga yale tuliyokwisha tumia.
Ukienda kwa mama ntilie, unawaona jinsi watu wanavyohustle, vijana wanawakopa, hela ya kula ngumu na wanakwambia wanakula mlo mmoja kwa siku.
Siku hizi kuangalia TV majumbani imeshakuwa anasa, hela ya king'amuzi kila mwezi mtihani!
Hali ni ngumu kitaa, hali ni mbaya sana. Nchi imekauka kaukau
Hivi viongozi wa serikali wanalijua hili?. Hivi wako aware na hali ya kiuchumi ya wananchi wao?
Serikali ilijue hili kuwa hali ni mbaya mtaani, data na Takwimu za makusanyo na kukua kwa uchumi hazitusaidii sisi wananchi, matangazo yenu hayajatranslate kwenye hali halisi huku kitaa!
Na hii ni Dar, Jiji kubwa vipi huko mikoani?
Nilichokiona kinasikitisha, Mitaa michafu, watu wamekondeana, fremu zimefungwa na zilizofunguliwa wateja ni wa kuhesabu.
Ukizunguuka ukaenda kwa wauza chipsi mafuta wameyachomea chipsi wameyarudia hata mara tano yamekuwa meusi tiii, wanakwambia brother hali ni ngumu hatuwezi kumwaga yale tuliyokwisha tumia.
Ukienda kwa mama ntilie, unawaona jinsi watu wanavyohustle, vijana wanawakopa, hela ya kula ngumu na wanakwambia wanakula mlo mmoja kwa siku.
Siku hizi kuangalia TV majumbani imeshakuwa anasa, hela ya king'amuzi kila mwezi mtihani!
Hali ni ngumu kitaa, hali ni mbaya sana. Nchi imekauka kaukau
Hivi viongozi wa serikali wanalijua hili?. Hivi wako aware na hali ya kiuchumi ya wananchi wao?
Serikali ilijue hili kuwa hali ni mbaya mtaani, data na Takwimu za makusanyo na kukua kwa uchumi hazitusaidii sisi wananchi, matangazo yenu hayajatranslate kwenye hali halisi huku kitaa!
Na hii ni Dar, Jiji kubwa vipi huko mikoani?
