Nchi imejaa Wanasiasa Malaya au Wanasiasa Fisi?

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,067
Sifa mojawapo ya mtu mwenye kiwango kikubwa cha akili (High IQ), ni kuyaona mambo kabla hayajatokea.

Katika viongozi ambao walikuwa na uwezo mkubwa wa kuyaona mambo kabla hayajatokea, kwa Tanzania na Afrika ni Mwalimu Nyerere. Huyu mengi aliyasema ambayo wakati wake hayakuwepo lakini yalikuja kushuhudiwa baadaye.

1) Alizungumzia juu ya umuhimu wa kuweka taratibu ngumu za kumfukuza kazi mfanyakazi ili kuwazuia watawala au waajiri wababe, wanaoweza kukufukuza wakati wowote iwe kwa haki au uonevu, kwa vile tu wana madaraka. Kwa maneno yake Mwalimu alisema, "mkubwa anaamka tu kumwambia mfanyakazi, kuanzia leo huna kazi. Bwana mkubwa, nina watoto, nina familia, wataishije". Tukaja kushuhudia wakati wa utawala wa Magufuli, watu wanafukuzwa kwenye mikutano wa hadhara. Sasa hivi tunashuhudia Samia anavyowafukuza kazi kila kukicha maDC na maDED. Yaani mtu yawezekana ana ajira yake, anaondolewa toka kwenye ajira yake, anateuliwa kuwa DC au DED, baada ya miezi michache anafukuzwa. Hivi vyeo vya kuteuliwa vimekuwa vya kumpa utukufu mteuaji hata wakati asipostahili. Wateuliwa wanaishi kama watumwa au mateka wake. Rais alistahilk kupewa idadi ndogo sana ya watu wa kuwateua, wengine wote walistahili kuwa waajiriwa wanaolindwa na kuwajibishwa kwa sheria za ajira.

2) Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa kuna "wanasiasa malaya. Wananunulika kama bidhaa, wanauza utu wao". Wakati wa awamu ya 5 tulishuhudia biashara kubwa ya manunuzi ya wanasiasa iliyosimamiwa na Polepole.

Wanasiasa malaya aliowaona mwalimu miaka mingi iliyopita, tukaja kuwaona dhahiri zaidi wakati wa awamu ya 5, awamu ya Marehemu Magufuli na Samia.

Orodha ya wanasiasa hawa malaya ni ndefu sana, wanasiasa walinunuliwa kama madafu au migebuka, na mpaka leo wametapakaa Serikalini, na hivyo kudhihirisha kuwa nchi kwa kiasi kikubwa inaongozwa na wanasiasa malaya, wanasiasa wanaonunulika, wanasiasa wasio na heshima ya utu. Baadhi nilioweza kuwakumbuka:

Godwin Mollel alikuwa CHADEMA
Julius Kalanga alikuwa CHADEMA
Pauline Gekul alikuwa CHADEMA
Joseph Mkundi alikuwa CHADEMA
Maulid Mtulia alikuwa CUF
Zuberi Kachauka alikuwa CUF
Abdala Mtolea alikuwa CUF
James Millya alikuwa CHADEMA
Kalist Lazaro alikuwa CHADEMA
Cecil Mwambe alikuwa CHADEMA
Vincent Mashinji alikuwa CHADEMA
Chacha Ryoba alikuwa CHADEMA
Waitara alikuwa CHADEMA
Kitila Mkumbo alikuwa ACT
Lulandala alikuwa CHADEMA
Bashiru alikuwa CUF
Patrobas Katambi alikuwa CHADEMA.

Lakini kwa sasa, nchi inanyemelewa na wanasiasa fisi. Hawa hawanunuliwi lakini wananyemelea uongozi kwa mbinu chafu. Sifa kubwa za wanasiasa fisi:

1. Kuwatukuza watawala kwa kutumia unafiki mkubwa, na rushwa ya sifa kwa watawala. Hawawezi kukosoa chochote.

2. Kila kitu wanakigeuza kuwa ni mali ya Rais. Ikijengwa daraja, barabara, wanachuo wakipewa mkopo, n.k. lugha yao utasikia, "Rais amevunja rekodi, amejenga darasa au amechimba kisima, n.k". Wakati ni dhahiri isiyoshaka kuwa Rais hana pesa, tena hata yeye mwenyewe anafadhiliwa na kodi zetu. Hatoi pesa bali tunampa pesa. Lakini wanaongea huo ujinga ili Rais awaone na kuwasikia, na baadaye awape ulaji, siyo awape kazi.

3. Hawa hata Rais ikitokea bahati mbaya akateleza akaanguka, wao watasema, "Rais aonesha maajabu, apiga sarakasi mpaka chini kwa kiwango ambacho hakijwahi kufanywa na Rais yeyote Duniani"

Na bahati mbaya sana uwanasiasa fisi kwa baadhi ya watu umeweza kulipa, ndiyo maana WANASIASA FISI WANAONGEZEKA KWA KASI SANA. Wapo ndani ya Serikali na nje ya serikali. Wanasiasa fisi waliopo ndani ya Serikali wanataka waendelee kubakia kwenye nafasi zao na wengine wanataka wapande zaidi. Hawana uwezo wowote wa maana zaidi ya ufisi, yaani kutoa sifa za kinafiki.

Kafulila alipoondolewa kwenye uRC, ilikuwa kila siku makala ndefu za kumsifia Rais. Ufisi mwishowe ukalipa, angalao akaweza kutulia. Wapo wanafisi waliopo nje ya serikali, kama akina Mwamshamvwa ambao bado hawajaonwa, hawa wapo mitandaoni wakikesha, kusifu, kutukuza na kuwaabudu watawala mpaka wanafamilia wa Rais, wameamua kuwa wanasiasa fisi, ili kungojelea kurushiwa chochote, kuyafanya maisha yao yaliyododa angalao yabadilike na kuwa katika mwanga.

MWISHO
Wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, hata siku moja, kamwe hawataweza kuipeleka nchi mahali popote, maana malengo yao siyo kutoa mchango wa maendeleo kwa Taifa, bali kuyapa uhakika wa kushiba matumbo yao.

Tuwaepuke na kuwakimbia wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, na watawala wanaopalilia uwepo wa wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, kwa namna yoyote inayowezekana.
 
Tuwaepuke na kuwakimbia wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, na watawala wanaopalilia uwepo wa wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, kwa namba yoyote inayowezekana
Hakika, hawa tunatakiwa kuwanyoosha sio kuwakimbia!
IMG-20231006-WA0015.jpg
 
Sifa mojawapo ya mtu mwenye kiwango kikubwa cha akili (High IQ), ni kuyaona mambo kabla hayajatokea.

Katika viongozi ambao walikuwa na uwezo mkubwa wa kuyaona mambo kabla hayajatokea, kwa Tanzania na Afrika ni Mwalimu Nyerere. Huyu mengi aliyasema ambayo wakati wake hayakuwepo lakini yalikuja kushuhudiwa baadaye...
Hapo kwa Lucas mwashambwa uko sahihi kabisa. Actually kuna fisi na chawa
 
Kwa hiyo unataka kiongozi akifanya vizuri asipongezwe? Unaposema anatumia kodi zetu kwa hiyo asipongezwe unakuwa unaonesha uwezo wako mdogo wa kifikra, kwani umeona nchi ngapi ambazo viongozi wao wanakusanya kodi lakini wanashindwa kuwapelekea maendeleo watu wao? Hujaona wengine badala ya kuwahudumia wananchi wanaishia kutapanya pesa za umma kwa maslahi yao binafsi? Hujaona wengine wakifungua akaunti nje ya Nchi?

Sasa kwanini tusimpongeze Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama samia Tunapoona Akitoa Elimu bure hadi kidato cha sita,akitoa mikopo kwa wanafunzi wote wenye sifa wa akili ya juu ,akitoa Billion 48 kwa ajili ya kufadhili masomo ya wanafunzi zaidi ya 8000 wanaosomea stashahada jambo ambalo miaka ya nyuma lilikuwa haliwezekani ? Kwanini tusimpongeze tunapoona akijenga vituo vya afya ,vyumba vya madara kwa fujo, miundombinu ya barabara kama ambavyo barabara za njia nne zinakwenda kujengwa kutoka igawa Mbeya hadi Tunduma mkoani Songwe zaidi ya km 237.9? Kwanini tusimpongeze anapotoa Ruzuku ya Billion mia moja hamsini katika mbolea? Kwanini Tusimpongeze tunapoona bei ya korosho au mbaazi ikianza kupaa baada ya kutafuta masoko na kufanya ushawishi wa kidiplomasia kwa nchi kama chini mpaka tunasamehewa deni la Billion 31 fedha ambazo zinaweza kujenga vituo vya afya zaidi ya 60?

Unaposema wanasiasa wanahama japo pia unachekesha sana. Kwa hiyo ulitaka waendelee kukaa kwenye vyama vya upinzani vilivyokosa Dira,muelekeo na malengo.vyama ambavyo vimeshindwa hata kujenga ofisi ya makao makuu ,vyama vya mifukoni mwao watu,vyama ambavyo ni kama mali ya watu binafsi na miradi ya kifamilia? Unataka waendelee kukaa kwenye vyama ambavyo kutwa nzima migogoro tu ya kugombea Ruzuku? Ni wajinga tu ndio wanaweza kukaa kwenye vyama vya aina hiyo.

Ndio maana wenye akili hukimbilia CCM Chama chenye itikadi inayoeleweka,sera na ajenda za kugusa maisha ya watu,chama chenye kuzungumzia ajenda na maisha ya watanzania,chama chenye kuleta matumaini katika maisha ya watanzania na chenye kushughulika na kero za watu.
 
Kwa hiyo unataka kiongozi akifanya vizuri asipongezwe? Unaposema anatumia kodi zetu kwa hiyo asipongezwe unakuwa unaonesha uwezo wako mdogo wa kifikra, kwani umeona nchi ngapi ambazo viongozi wao wanakusanya kodi lakini wanashindwa kuwapelekea maendeleo watu wao? Hujaona wengine badala ya kuwahudumia wananchi wanaishia kutapanya pesa za umma kwa maslahi yao binafsi? Hujaona wengine wakifungua akaunti nje ya Nchi?

Sasa kwanini tusimpongeze Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania Mama samia Tunapoona Akitoa Elimu bure hadi kidato cha sita,akitoa mikopo kwa wanafunzi wote wenye sifa wa akili ya juu ,akitoa Billion 48 kwa ajili ya kufadhili masomo ya wanafunzi zaidi ya 8000 wanaosomea stashahada jambo ambalo miaka ya nyuma lilikuwa haliwezekani ? Kwanini tusimpongeze tunapoona akijenga vituo vya afya ,vyumba vya madara kwa fujo, miundombinu ya barabara kama ambavyo barabara za njia nne zinakwenda kujengwa kutoka igawa Mbeya hadi Tunduma mkoani Songwe zaidi ya km 237.9? Kwanini tusimpongeze anapotoa Ruzuku ya Billion mia moja hamsini katika mbolea? Kwanini Tusimpongeze tunapoona bei ya korosho au mbaazi ikianza kupaa baada ya kutafuta masoko na kufanya ushawishi wa kidiplomasia kwa nchi kama chini mpaka tunasamehewa deni la Billion 31 fedha ambazo zinaweza kujenga vituo vya afya zaidi ya 60?

Unaposema wanasiasa wanahama japo pia unachekesha sana. Kwa hiyo ulitaka waendelee kukaa kwenye vyama vya upinzani vilivyokosa Dira,muelekeo na malengo.vyama ambavyo vimeshindwa hata kujenga ofisi ya makao makuu ,vyama vya mifukoni mwao watu,vyama ambavyo ni kama mali ya watu binafsi na miradi ya kifamilia? Unataka waendelee kukaa kwenye vyama ambavyo kutwa nzima migogoro tu ya kugombea Ruzuku? Ni wajinga tu ndio wanaweza kukaa kwenye vyama vya aina hiyo.

Ndio maana wenye akili hukimbilia CCM Chama chenye itikadi inayoeleweka,sera na ajenda za kugusa maisha ya watu,chama chenye kuzungumzia ajenda na maisha ya watanzania,chama chenye kuleta matumaini katika maisha ya watanzania na chenye kushughulika na kero za watu.
Umalaya wa mwanamke hautimii bila ufuska wa mwanaume! Hakuna malaya au fuska mwaminifu!
 
Jana nilikuwa namuangalia DC wa Bariadi akiongelea vifo vya Wasichana wawili waliopewa dawa ya kuongeza urefu wa matiti na Mganga wa kienyeji, na ikawasababishia umauti wao.

Mkuu wa Wilaya yeye alitumia muda mwingi kumsifu Mama mpaka akawa anakera.😁
 
Mbinu inazotumia sasa hivi CCM kuendelea kuwa na hayo mafisi ni kuendelea kuyafanya hayo mafisi kuwa maskini pia imeweza kuvicontrol vyombo vya habari radio, televisheni na magazeti hivi vyote kuanzia asubuhi mpaka usiku ni kusifu na kuiabudu serikali wakibadilisha sana labda watapiga umbea wa wasanii au habari za simba na yanga.
 
.2) Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa kuna "wanasiasa malaya. Wananunulika kama bidhaa, wanauza utu wao". Wakati wa awamu ya 5 tulishuhudia biashara kubwa ya manunuzi ya wanasiasa iliyosimamiwa na Polepole.

Wanasiasa malaya aliowaona mwalimu miaka mingi iliyopita, tukaja kuwaona dhahiri zaidi wakati wa awamu ya 5, awamu ya Marehemu Magufuli na Samia.
MWISHO
Wanasiasa malaya, hata siku moja, kamwe hawataweza kuipeleka nchi mahali popote, maana malengo yao siyo kutoa mchango wa maendeleo kwa Taifa, bali kuyapa uhakika wa kushiba matumbo yao.

Tuwaepuke na kuwakimbia wanasiasa malaya na watawala wanaopalilia uwepo wa wanasiasa malaya kwa namna yoyote inayowezekana.
Naunga mkono hoja nami niliwahi kutoa angalizohili Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!


View: https://youtu.be/Qc-nXKcZbbc?si=P-8J7oj598tKIRq2
P
 
Sifa mojawapo ya mtu mwenye kiwango kikubwa cha akili (High IQ), ni kuyaona mambo kabla hayajatokea.

Katika viongozi ambao walikuwa na uwezo mkubwa wa kuyaona mambo kabla hayajatokea, kwa Tanzania na Afrika ni Mwalimu Nyerere. Huyu mengi aliyasema ambayo wakati wake hayakuwepo lakini yalikuja kushuhudiwa baadaye.

1) Alizungumzia juu ya umuhimu wa kuweka taratibu ngumu za kumfukuza kazi mfanyakazi ili kuwazuia watawala au waajiri wababe, wanaoweza kukufukuza wakati wowote iwe kwa haki au uonevu, kwa vile tu wana madaraka. Kwa maneno yake Mwalimu alisema, "mkubwa anaamka tu kumwambia mfanyakazi, kuanzia leo huna kazi. Bwana mkubwa, nina watoto, nina familia, wataishije". Tukaja kushuhudia wakati wa utawala wa Magufuli, watu wanafukuzwa kwenye mikutano wa hadhara. Sasa hivi tunashuhudia Samia anavyowafukuza kazi kila kukicha maDC na maDED. Yaani mtu yawezekana ana ajira yake, anaondolewa toka kwenye ajira yake, anateuliwa kuwa DC au DED, baada ya miezi michache anafukuzwa. Hivi vyeo vya kuteuliwa vimekuwa vya kumpa utukufu mteuaji hata wakati asipostahili. Wateuliwa wanaishi kama watumwa au mateka wake. Rais alistahilk kupewa idadi ndogo sana ya watu wa kuwateua, wengine wote walistahili kuwa waajiriwa wanaolindwa na kuwajibishwa kwa sheria za ajira.

2) Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa kuna "wanasiasa malaya. Wananunulika kama bidhaa, wanauza utu wao". Wakati wa awamu ya 5 tulishuhudia biashara kubwa ya manunuzi ya wanasiasa iliyosimamiwa na Polepole.

Wanasiasa malaya aliowaona mwalimu miaka mingi iliyopita, tukaja kuwaona dhahiri zaidi wakati wa awamu ya 5, awamu ya Marehemu Magufuli na Samia.

Orodha ya wanasiasa hawa malaya ni ndefu sana, wanasiasa walinunuliwa kama madafu au migebuka, na mpaka leo wametapakaa Serikalini, na hivyo kudhihirisha kuwa nchi kwa kiasi kikubwa inaongozwa na wanasiasa malaya, wanasiasa wanaonunulika, wanasiasa wasio na heshima ya utu. Baadhi nilioweza kuwakumbuka:

Godwin Mollel alikuwa CHADEMA
Julius Kalanga alikuwa CHADEMA
Pauline Gekul alikuwa CHADEMA
Joseph Mkundi alikuwa CHADEMA
Maulid Mtulia alikuwa CUF
Zuberi Kachauka alikuwa CUF
Abdala Mtolea alikuwa CUF
James Millya alikuwa CHADEMA
Kalist Lazaro alikuwa CHADEMA
Cecil Mwambe alikuwa CHADEMA
Vincent Mashinji alikuwa CHADEMA
Chacha Ryoba alikuwa CHADEMA
Waitara alikuwa CHADEMA
Kitila Mkumbo alikuwa ACT
Lulandala alikuwa CHADEMA
Bashiru alikuwa CUF
Patrobas Katambi alikuwa CHADEMA.

Lakini kwa sasa, nchi inanyemelewa na wanasiasa fisi. Hawa hawanunuliwi lakini wananyemelea uongozi kwa mbinu chafu. Sifa kubwa za wanasiasa fisi:

1. Kuwatukuza watawala kwa kutumia unafiki mkubwa, na rushwa ya sifa kwa watawala. Hawawezi kukosoa chochote.

2. Kila kitu wanakigeuza kuwa ni mali ya Rais. Ikijengwa daraja, barabara, wanachuo wakipewa mkopo, n.k. lugha yao utasikia, "Rais amevunja rekodi, amejenga darasa au amechimba kisima, n.k". Wakati ni dhahiri isiyoshaka kuwa Rais hana pesa, tena hata yeye mwenyewe anafadhiliwa na kodi zetu. Hatoi pesa bali tunampa pesa. Lakini wanaongea huo ujinga ili Rais awaone na kuwasikia, na baadaye awape ulaji, siyo awape kazi.

3. Hawa hata Rais ikitokea bahati mbaya akateleza akaanguka, wao watasema, "Rais aonesha maajabu, apiga sarakasi mpaka chini kwa kiwango ambacho hakijwahi kufanywa na Rais yeyote Duniani"

Na bahati mbaya sana uwanasiasa fisi kwa baadhi ya watu umeweza kulipa, ndiyo maana WANASIASA FISI WANAONGEZEKA KWA KASI SANA. Wapo ndani ya Serikali na nje ya serikali. Wanasiasa fisi waliopo ndani ya Serikali wanataka waendelee kubakia kwenye nafasi zao na wengine wanataka wapande zaidi. Hawana uwezo wowote wa maana zaidi ya ufisi, yaani kutoa sifa za kinafiki.

Kafulila alipoondolewa kwenye uRC, ilikuwa kila siku makala ndefu za kumsifia Rais. Ufisi mwishowe ukalipa, angalao akaweza kutulia. Wapo wanafisi waliopo nje ya serikali, kama akina Mwamshamvwa ambao bado hawajaonwa, hawa wapo mitandaoni wakikesha, kusifu, kutukuza na kuwaabudu watawala mpaka wanafamilia wa Rais, wameamua kuwa wanasiasa fisi, ili kungojelea kurushiwa chochote, kuyafanya maisha yao yaliyododa angalao yabadilike na kuwa katika mwanga.

MWISHO
Wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, hata siku moja, kamwe hawataweza kuipeleka nchi mahali popote, maana malengo yao siyo kutoa mchango wa maendeleo kwa Taifa, bali kuyapa uhakika wa kushiba matumbo yao.

Tuwaepuke na kuwakimbia wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, na watawala wanaopalilia uwepo wa wanasiasa malaya na wanasiasa fisi, kwa namba yoyote inayowezekana.
U DED si ajira ya kudumu...

U DC si ajira ya kudumu....

Wakitenguliwa hurudi kule walikotoka....unafeli wapi ?!!!

Hili nalo ni "rocket science"?!!!

Malalamiko yako ni ya KIPUUUMBAAAVUUUR
 
Umeamka na shida zako kichwani....

Badala ya KUPAMBANA nazo unaamua kuwafanya wanasiasa "punching bag" la kufika kwako "or....sm"....

Ujinga + Upumbavu
 
Ninampongeza Rais Samia kwa kuwakumbuka wanafunzi wa DIPLOMA.....

Tulipata "boom".....nao wapate sasa......

Bilioni 48 kwa "beneficiaries" 8000 ni mwanzo mzuri

#Siempre JMT
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom