M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
Nipo uwanja wa ndege wa "kimataifa" wa JK Nyerere nikisubiri usafiri wa kwenda Kilimanjaro kwa ndege ya Precision Air,hali hapa uwanjani ni mbaya sana kuna mamia ya abiria wanasubiri kusafiri toka jana usiku,kinachonisikitisha na kilichonisukuma kuandika thread hii ni kuwa hakuna taarifa yeyote toka kwenye uongozi wa uwanja juu ya kinachoendelea,tumefuatilia na jibu tulilopewa ni kuwa eti **** timu toka JWTZ inasubiriwa ije ikague uwanja,nilitegemea hayo yangefanyika mapema sana ili kuondoa tafrani hii lakini hadi sasa haijulikani timu hiyo itafika saa ngapi.Watanzania tupunguze kufanya kazi kwa mazoea,tunatia aibu sana.