Naleta uzi jukwaani baada ya kuona uzi wa MwanaDiwani jana (
https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=784297) ukieleza jinsi umatu wa wanabumbuli huko Tanga walivyojitokeza katika mkutano.
Nimpongeze Nape na Kinana kwa ziara nzuri zinazoitwa za kujenga chama vijijini ( Japo mimi naamini ni za kukiua chama - nitaeleza sababu).
Pili Nimekuwa nikijiuliza JE NI KWELI NAPE NA KINANA HAWAJAJUA SABABU ZA WANANCHI WENGI KUHUDHURIA MIKUTANO YAO AU WANATUZUGA? NA KAMA WANATUZUGA - JE WANAMFARIJI NANI JUU JA HILI?
Sababu zinazowafanya watanzania kuhushuri mikutano zilizo wazi ni
1) Viongozi wa chama ni lazima wahudhurie. Hawana option ya kuchagua hata kama hawako tayari. Tumeona mpaka ma DC na DED wakilazimika kuambatana na ziara. Hivyo hili Nape / Kinana halijui?
2. Wenye shida mbalimbali kuja kusikiliza kuna nini kipya cha kutatua shida zao? Huu ni mfano wa wahudhuriaji wengi waliojitokeza Huko Bumbuli kujua msimamo juu ya kiwanda na chai zao, Mtwara mjini kujua uhalisia wa gesi inavyotoka, Singida mashariki (Kwa Lissu) kujua hatima ya mgodi wa sagharu, Mwanza - kujuona ahadi ya meli kubwa iliyoahidiwa na JK. n.k. wengine mtasaidia kuainisha maeneo na sababu.
3) Masikini wanaofuata mgao wa kanga, T shirt, mafuta ya bodaboda / bajaji, ubwabwa n.k ambo husombwa na malori. Ifahamike kuwa wahudhuriaji hawa wengi huwa hawana dhamira za zati kuja kusikiliza ndio maana bila usafiri hawaji au hivyo vitakrima hawaji.
Hapa unaweza tofautisha na wahudhuriaji wa mikutano ya vyama pinzani. Hakuna mtu hata mmoja anaegharamiwa usafiri ili kufika uwanjani bali wanaenda kwa nia ya kusikiliza sera na mikakati ya wapinzani.
4) Uhamasishwaji wa wanachama na wananchi juu ya kuhudhuria mikutano unaofanywa mtaa kwa mtaa. Hivyo wengi wanakuja kwa kuwa wainekane na kiongozi wao wa mtaa kuwa walihudhuria na si matakwa yao toka moyoni kuhudhuria.
5) kundi kubwa la wafanyabiashara na baadhi ya viongozi/ watumishi wa umma kufika kwa ajili ya kulinda maslahi binafi katika kazi zao. Kama inavyofahamika kuwa ukijiweka wazi wazi kuwa uko uponzani basi hata kabiashara kako kataandamwa, kila kukicha polisi wako na wewe na makosa ya kubambikwa. Hivyo kinafiki lazima walete nyuso ila ktk nafsi sio.
Sasa hizi sababu zote ina maana Nape na Kinana hawazijui au wanatuzuga? Je wanatudanganya sisi wananchi au wanajidanganya nafsi zai?
Pia nilisemaziara ni za kukiuwa chama sababu
1. Wananchi wanaenda kusikiliza nini chama kinataka kusema juu ya shida zao. Hotuba hujikita kulaumu zaidi utendaji mbovu wa serikali ambayo ni ya CCM, kuponda wapinzani kuwa hawataleta maendeleo hali ya kuwa CCM ina miaka zaidi ya 50 ikiwa hijafanya vya kutosha kushawishi wananchi. Upinzani kuleta machafuko hali ya kuwa wananchi wanashuhudia machafuko yakianzishwa na aidha vyombo vya dola au na wanaCCM mbele ya vyombo vya dola bila hatua stahiki kuchukuliwa.
2. Wananchi wanahitaji kuambiwa ni hatua gani zimechukuliwa na chama juu ya wafuja uchumi. Kitu ambacho chama chenyewe kuonyesha kimeshindwa kuwawajibisha wahisika na kimeamua kujiunga nao kuendeleza uhujumu.
Hivyo kwa hotuba hizi chama kitazidi kudidimia tu ikilinganishwa na kabla ya ziara ambapo wananchi8 walikuwa "undecided"
Niishie kwa kusema CCM inajichimbia kaburi lake kwa ziara zake.