Mathias Lyamunda
JF-Expert Member
- Apr 4, 2013
- 1,369
- 559
Nimeattach gazeti lenye tamko la chama cha nccr mageuzi wilaya ya Tarime kikipinga mgawanyo wa majimbo ndani ya Ukawa.
Ni dhahiri kuwa kuna tatizo kubwa ndani ya ukawa na viongozi wetu hawawi wakweli kuhusu kinachojiri ndani ya vikao, wanachoeleza kwa umma kinatofautiana na uhalisia.
Ni wakati sasa viongozi wa ngazi za Taifa wakawa wanaratibu mambo yao na viongozi wa ngazi za chini. Unafiki unaofanywa na viongozi ngazi ya Taifa hautasaidia kuwa na muungano imara, maana hadi sasa kuna sintofahamu na kujenga juu bila kuwa na msingi mzuri ni sawa na kujenga nyumba yenye paa zuri bila kuwa na msingi imara.
Sasa Tarime kuna NCCR habu tuambie walipata viti vingapi kwenye serikali za mitaa, matamko ya wahuni yanakuwa amplified na wapinzani wa UKAWA, na wewe unayabeba kichwa kichwa, hatutoi majimbo ili chama mishindwe, tutao jimbo kwa chama pale ambapo chama kina nguvu na mtandao wa kushinda. Siyo lazima kwenye UKAWA tukubaliane kila kitu, na viongozi wako wazi juu ya hili.