NCCR wapinga mgao wa Majimbo UKAWA

NCCR wapinga mgao wa Majimbo UKAWA

Viongozi wa UKAWA walikubaliana kugawana maeneo ya kugombea ubunge na udiwani kivyama.Vigezo wanavyotumia kugawana nafasi na maeneo wanavijua viongozi wenyewe.Nimekutana na wanachama ambao walijiandaa muda mrefu kugombea maeneo husika na kujikuta maeneo hayo yanapewa Chama kingine ndani ya UKAWA wakati wao wamewekeza muda mrefu wagombee.

Vigezo vingi wanavyotumia ni takwimu za uchaguzi uliopita bila kujali mabadiliko mbalimbali ambayo yametokea kwa kipindi cha Miaka miatano.

UKAWA mnatumia vigezo gani kugawana maeneo hebu waelezeni wanachama wenu acheni utapeli.
Simama uwesabiwe ukawa ndio mambo ya mjini tulia kama umepigwa ganzi October watanzania wako na Ukawa.


swissme
 
Viongozi wa UKAWA walikubaliana kugawana maeneo ya kugombea ubunge na udiwani kivyama.Vigezo wanavyotumia kugawana nafasi na maeneo wanavijua viongozi wenyewe.Nimekutana na wanachama ambao walijiandaa muda mrefu kugombea maeneo husika na kujikuta maeneo hayo yanapewa Chama kingine ndani ya UKAWA wakati wao wamewekeza muda mrefu wagombee.

Vigezo vingi wanavyotumia ni takwimu za uchaguzi uliopita bila kujali mabadiliko mbalimbali ambayo yametokea kwa kipindi cha Miaka miatano.

UKAWA mnatumia vigezo gani kugawana maeneo hebu waelezeni wanachama wenu acheni utapeli.

Mkuu,
kuna thread zaid ya 100 zikieleza namana majimbo yalivyogawanywa.

lakini pia kuna ufafanuzi ma majimbo husika.

Pole zake huyo bwana, lengo ni kuingoa ccm akubali kumpisha mwenzie
 
mbinu zenu za kutugombanisha kwa kutumia vibaraka wenu mnaowatumia kwa maslai yenu hazita fua dafu .tumejizatiti kuulinda na kuutetea umoja huu kwa mbinu na gharama yeyote .ukawa wana msemaji na maazimio ,matamko yoyote yasiyosemwa na viongozi waandamizi na msemaji hayatakuwa na matokeo chanya yoyote, period!
 
Lakini NCCR mnalalamika nini? CHADEMA walishapotea pale walipoanza mgogoro na ZITTO na ndiyo maana wakaamua kuotesha Mbegu mpya ya CHADEMA HYBRID wakaiita UKAWA . NCCR mnatumiwa tu kama Karai la zege mwisho wa siku mtatupwa tu.
kumbe wewe ndio muasisi wa "KARAI"?
 
Back
Top Bottom