Nawezaje kutoa mzigo airpot?

Nawezaje kutoa mzigo airpot?

KeXMO

Member
Joined
Jul 25, 2021
Posts
20
Reaction score
0
Wakuu napenda kufahamu

Niliagiza mzgo wangu wa simu kwa kutumia FedEx kwa matumizi yangu. Nimejarbu kuwapelekea invoice kwa sababu unahitajika kufanyiwa clearance ila inaonekana gharama ni kubwa Sanaa mara pesa ya clearance agent km kilo na nusu na bado wanahitaji tin number , bado custom na tax ili mzgo utoke

So mwenye uzoefu ushauri wenu

Na ni kampuni gani ambayo naweza kutumia kuagiza kutoka mataifa ya ulaya na USA wanafanya kabsa clearance na hakuna usumbufu km huu ulojitokeza?

Maoni yenu na ushauri
 
So mwenye uzoefu ushauri wenu
Hakuna short cut katika hili swala
  • Lipia Agent charges zao
  • Lipia TAX/ VAT utakayoelezwa na TRA
  • Lipia TBS - Iwapo nao watakudai
Ili kujifunza zaidi pitia hii link
Pia rejea hizi thread;
 
Sasa kama hata tin namba huna unaishije mjini? Nyie ndio tunawatafuta unamiliki pesa halafu hamchangii maendeleo
 
Hakuna short cut katika hili swala
  • Lipia Agent charges zao
  • Lipia TAX/ VAT utakayoelezwa na TRA
  • Lipia TBS

Ili kujifunza zaidi pitia hii link
Pia rejea hizi thread;
Mkuu kwa uzoefu wako wa miaka mingi katika haya mambo ya kununua bidhaa nje ni njia ipi rahisi ya kununua kitu nje kama vile laptop au simu ambayo inawezesha kukwepa haya magharama?
 
Uliagiza simu ngapi? Kama moja tu afu kwa FEDEX basi haya matatizo umejitafutia mwenyewe.
 
Uliagiza simu ngapi? Kama moja tu afu kwa FEDEX basi haya matatizo umejitafutia mwenyewe.
Unashangwazwa na Tozo kwenye simu Airport!

Sikia hili swala langu, Miwani ya macho ambayo kiuhalisia haitakiwi kulipiwa Tozo, sababu ni sehemu ya kifaa tiba, Ila nililazimika kulipia TZS 81,661.89 kama tozo
1628687579496.png
 
Alipaswa afanyeje mkuu?

Kuagiza simu moja nje ni upotezaji pesa na muda.

Angeweza kununua hiyo simu ndani au kuagiza mtu amletee ila sio kuagiza simu moja tu ya matumizi binafsi tena kwa FEDEX.

Mara nyingi bei ya simu bongo haina tofauti na nje hasa kama ni simu moja tu.
 
Unashangwazwa na Tozo kwenye simu Airport!

Sikia hili swala langu, Miwani ya macho ambayo kiuhalisia haitakiwi kulipiwa Tozo, sababu ni sehemu ya kifaa tiba, Ila nililazimika kulipia TZS 81,661.89 kama tozo
View attachment 1888422

Sijashangazwa na tozo, matter of fact inabidi wakate tozo ndo kazi yao.

Nimeshangaa mtu kuagiza simu moja tu nje kwa fedex.

Kuna kasumba kwamba simu nje ni nafuu au original nk. Haya yanaweza kuwa kweli kama unanunua in bulk ila kama ni simu moja tu ya matumizi binafsi you're better off kununua nchini au kuagiza mtu aje nayo kama unafahamiana na mtu nje.
 
Back
Top Bottom