Nawezaje kupata viti na meza za Coca-Cola?

Nawezaje kupata viti na meza za Coca-Cola?

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,472
Kuna wazo la kibiashara nalifanyia kazi ila mtaji umebana sana. Najaribu kubuni mbinu ninazoweza kutumia ili nianze tu na chochote nilichonacho huku nikiboresha kwa jinsi ninavyosogea.

Ningependa kujua ni utaratibu gani wa kuchukua ili kupata viti, meza, miamvuli na labda hata jokofu za Coca-Cola bila gharama yoyote.

Nadhani kama sikosei watakuwa wana utaratibu fulani wa kutoa vitu hivyo kama njia ya kujitangaza.

Natanguliza shukrani.
 
Kuna wazo la kibiashara nalifanyia kazi ila mtaji umebana sana. Najaribu kubuni mbinu ninazoweza kutumia ili nianze tu na chochote nilichonacho huku nikiboresha kwa jinsi ninavyosogea.

Ningependa kujua ni utaratibu gani wa kuchukua ili kupata viti, meza, miamvuli na labda hata jokofu za Coca-Cola bila gharama yoyote.

Nadhani kama sikosei watakuwa wana utaratibu fulani wa kutoa vitu hivyo kama njia ya kujitangaza.

Natanguliza shukrani.
Upo wapi Mkuu
 
Nenda kwa wakala mkuu wa coca mkoani mwako, kaone masharti ya kuweza kupewa hivyo vitu, ila Pepsi fasta unavipata kutokana na kununua creti kadhaa za soda kwao wanakupelekea kwa usafiri wao. Maana wamepata mteja mkubwa kwa hiyo lazima wakurinde usipotee kwa maofa ya fridge meza na viti kutokana na eneo lako la biashara
 
Nenda kwa wakala mkuu wa coca mkoani mwako, kaone masharti ya kuweza kupewa hivyo vitu, ila Pepsi fasta unavipata kutokana na kununua creti kadhaa za soda kwao wanakupelekea kwa usafiri wao. Maana wamepata mteja mkubwa kwa hiyo lazima wakurinde usipotee kwa maofa ya fridge meza na viti kutokana na eneo lako la biashara

Asante sana mkuu kwa ushauri wako na tip hiyo ya pepsi. Ubarikiwe.
 
Chek mtaan unapoishi kunakuwa na agent mmoja wa coca ulizia penye frij au vit walipogawa utapata namba ya ya Agent
 
Friji utapata kwa urahisi ila viti na meza hapo pagumu but nenda depo au piga mkono gari ya coca then waeleze shida yako
Friji 90% utapewa ila meza na viti utaambiwa mpaka vikinunuliwa otherwise waone una mgahawa mkubwa sanaaa na uhonge pesa kidogo watakupa kibongobongo.
 
Back
Top Bottom