Nawezaje kubadili muandiko

Nawezaje kubadili muandiko

Short Boe

Member
Joined
Nov 15, 2021
Posts
20
Reaction score
16
Mimi ni kijana umri wangu miaka 21 elimu yangu form four lakini nakabiliwa na changamoto ya kuandika sina amani na mwandiko wangu kila ninapoandika wenzangu wanacheka wanasema naandika kama mtoto wa shule ya msingi

Nimejitahidi kubadili lakini bado na hali hii inanikosesha raha kabisa ikitokea ishu ya kuandika hapa kazini napiga chenga msaada wenu wakubwa
 
Mi ni kijana umri wangu miaka 21 elimu yangu form four lakini nakabiliwa na changamoto ya kuandika sina amani na mwandiko wangu kila nqpoandika wenzangu wanacheka wanasema naandika kama mtoto wa shule ya msingi nmejitahidi kubadili lakini bado na hali hii inanikoseshq raha kabisa ikitokea ishu ya kuandika hapa kazini napiga chenga msaada wenu wakubwa
Usijali Kijana, issue ya mwandiko ni miongoni mwa vitu ambavyo vinatutofautisha binadamu, mwandiko ni sawa na maumbile yetu, hayawezi kuwa sawa sawa ata siku 1

Mwandiko waga tunaanza kuutengeneza tangu primary, ikishindikana hapo ndo basi tena ni ngumu sana kubadirika tena, kwa hapo ulipofkia huwezi tena kuchange art yako ispokuwa unatakiwa uipende na kuichukulia Kama sehemu ya Kiungo chako cha mwili

Jiamini kijana kuna watu wana art mbaya sana na wana nafasi kubwa tu serikalini, ila kwakuwa mwandiko haurepresent kilichopo kichwani au kile anachokitoa katika jamii basi anapotezea tu, kukwepa kuandika wala hakukusaidii ispokuwa ndo kunazidi kupunguza hali yako ya kujiamini

potezea maneno ya wenzio inaonekana bado mna Mambo ya kitoto sana, issue ya kuchekana mwandiko wanafanya watu ambao bado haeajajitambua na kupevuka vizuri, ukichekwa na wewe ukamaindi jua ndo unazidi kuwapa nafasi ya kuzidi kukutania, ila Kama wanakutania alafu we unapotezea watachoka tu na kusahau
 
Mi ni kijana umri wangu miaka 21 elimu yangu form four lakini nakabiliwa na changamoto ya kuandika sina amani na mwandiko wangu kila nqpoandika wenzangu wanacheka wanasema naandika kama mtoto wa shule ya msingi nmejitahidi kubadili lakini bado na hali hii inanikoseshq raha kabisa ikitokea ishu ya kuandika hapa kazini napiga chenga msaada wenu wakubwa


Huo mwandiko wako unata uweje??!!
 
Usijali Kijana, issue ya mwandiko ni miongoni mwa vitu ambavyo vinatutofautisha binadamu, mwandiko ni sawa na maumbile yetu, hayawezi kuwa sawa sawa ata siku 1

Mwandiko waga tunaanza kuutengeneza tangu primary, ikishindikana hapo ndo basi tena ni ngumu sana kubadirika tena, kwa hapo ulipofkia huwezi tena kuchange art yako ispokuwa unatakiwa uipende na kuichukulia Kama sehemu ya Kiungo chako cha mwili

Jiamini kijana kuna watu wana art mbaya sana na wana nafasi kubwa tu serikalini, ila kwakuwa mwandiko haurepresent kilichopo kichwani au kile anachokitoa katika jamii basi anapotezea tu, kukwepa kuandika wala hakukusaidii ispokuwa ndo kunazidi kupunguza hali yako ya kujiamini

potezea maneno ya wenzio inaonekana bado mna Mambo ya kitoto sana, issue ya kuchekana mwandiko wanafanya watu ambao bado haeajajitambua na kupevuka vizuri, ukichekwa na wewe ukamaindi jua ndo unazidi kuwapa nafasi ya kuzidi kukutania, ila Kama wanakutania alafu we unapotezea watachoka tu na kusahau
Nimekuelewa vizuri kaka umenifanya nimepata amani barikiwa Sana kaka
 
Nataka uwe mzuri

Kuna miandiko ya aina nyingi na kila uzuri wa muandiko upo machoni kwa aupendaye, hii ni sawa na uzuri wa mwanamke upo machoni kwa amtazamaye na ampendaye sio lazima mwanamke nimpendaye mimi na wewe umpende yaani kuna vigezo vyangu vya uzuri wa mwanamke na ni hivyo hivyo lazima utuwekee vigezo vya mwandiko mzuri unaoupenda.

Labda nikusaidie; Tafuta muandiko wa mtu yeyote unaouona kwako ni mzuri halafu chukua peni na daftari uwe unajaribu kukopi herufi moja moja za huo muandiko kwa taratibu, zoezi hili litafutie muda kila siku uwe ukilifanya, hii ni njia moja ya kuupa mkono na vidole mazoezi ya kunyumbumbulisha herufi kwani Muandiko ni sanaa ya vidole jinsi vinavyoichezea kalamu juu ya karatasi, hii ni sawa na mpira wa miguu ni sanaa ya miguu jinsi inavyochezea mpira uwanjani--- natumai ukijibidiisha katika njia hii hatimaye unaweza kuona matunda, usikate tamaa, hakuna kukata tamaa ukiwa hai na nafasi unayo.🙏🏻🙏🏻
 
Mie nilibadili muandiko nipo form two, inawezekana ila sema inahtaji muda mawazo ya jamaa aliepita ya kuiga muandiko na herufi flan flan yafanyie kazi
 
Usijisikie vibaya mdogo wangu. Wewe unahitajo msaada wa utumie mbinu gani. Mimi madhani uanze kwa kuumba herufi moja moja kwanza. Naamini ukifanya mazoezi mengi utafanikiwa

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
Kuna miandiko ya aina nyingi na kila uzuri wa muandiko upo machoni kwa aupendaye, hii ni sawa na uzuri wa mwanamke upo machoni kwa amtazamaye na ampendaye sio lazima mwanamke nimpendaye mimi na wewe umpende yaani kuna vigezo vyangu vya uzuri wa mwanamke na ni hivyo hivyo lazima utuwekee vigezo vya mwandiko mzuri unaoupenda.

Labda nikusaidie; Tafuta muandiko wa mtu yeyote unaouona kwako ni mzuri halafu chukua peni na daftari uwe unajaribu kukopi herufi moja moja za huo muandiko kwa taratibu, zoezi hili litafutie muda kila siku uwe ukilifanya, hii ni njia moja ya kuupa mkono na vidole mazoezi ya kunyumbumbulisha herufi kwani Muandiko ni sanaa ya vidole jinsi vinavyoichezea kalamu juu ya karatasi, hii ni sawa na mpira wa miguu ni sanaa ya miguu jinsi inavyochezea mpira uwanjani--- natumai ukijibidiisha katika njia hii hatimaye unaweza kuona matunda, usikate tamaa, hakuna kukata tamaa ukiwa hai na nafasi unayo.🙏🏻🙏🏻
Ahsante Sana kaka nashukuru kwa ushauri ntalifanyia kazi
 
Mie nilibadili muandiko nipo form two, inawezekana ila sema inahtaji muda mawazo ya jamaa aliepita ya kuiga muandiko na herufi flan flan yafanyie kazi
Shukrani pamoja Sana ndugu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom