Naweza, najua lakini sijiami.

Naweza, najua lakini sijiami.

Mchebe

Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
30
Reaction score
4
Kwanza nianze na kujiamini. Hivi ni kitu gani kinasababish m2 kutojiamini? Maranying napenda kukaa na watu wenye uwelewa wa kutosha kuhusu mambo, napia napenda kujifunza zaid. Lakini nakuwa sijiamini hususani pale wanapo anzisha topic: nakuwa muoga kuchangia kabisa na ingali kichwani huwa nina point zuri 2 ya kuchangia lkn nasita kuipresent, mara chache sana ninapojikuta nimeropoka, huwa wanakubali point yangu na kuisuppot kwa asilimia kubwa. huwa najiuliza nini hasa kinanisibu mpaka nakuwa muoga? hii hali huwa inanitokea mara kwa mara hata nikiwa na wazazi nyumbani. Tatizo hili linanisumbua xana na pia huwa napenda kujitenga pekeyangu kwa mda mrefu bila kuonana na marafk na hata sometym wanapojaribu kuonana na me huwaga nawa chukia pasi na sababu. Hii inapelekea baadhi ya watu wanasema me naringa. lakini me siringi huwa natumia silaa hiyo kuficha udhaifu wangu 2. Nisaidieni wakubwa, nawasikiliza nyie
 
una jini mahaba nenda kwa mganga au kaombewe kanisani atakaye kupa sayansi za humu JF imekula kwako
 
Jamani humu ni kusaidiana na kuelimishana hususani kwa mambo yale yanayotusibu au tusio yajua. So naombeni msaada jamani me nipo serious kwa hili. Kwani nimekuwa kama mtumwa katika maisha. Nateseka
 
pole sana au umelelewa na mama wa kambo kiasi kwamba ukaaminishwa kwamba ww si chochote kwenye dunia hii.

Ngoja nikupe mfano wangu: Mm nina confidence ya kujieleza mbele za watu, kujitetea, kuelezea feeling zangu bila woga wowote kiasi kwamba mara nyingi huwa nawaudhi watu kwani wengi huwa hawapendi kuambiwa ukweli. Hali hii pia imenipelekea nisiwe mtu wa kujichanganya sana kuepuka kugombana na watu.

Kwa upande wako sijui itakuwa tatizo ni nn au elimu ndogo inakunyima uhuru wa kujiamini. Jichunguze utagundua tu kinachosababisha usijiamini.
 
..itakuwa ni vema ukijifunza kuwasiliana..kuwasilisha mawazo yako maana kataika hoja yoyote ile, kila mtu anamawazo yake binafsi kwa mtazamo wake mwenyewe either from experience au kutoka kwa wengine.. just speak out your mind, ilimradi si kwa njia ya hasira, tusi, wala kejeli kwa wachangia mada wengine
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ni kweli madameA. Huenda ikawa nisababu inayochangia me kuwa hivyo. Nakumbuka nimelelewa kwenye mazingira kma hayo. Lakini kwangu ni tofauti kidogo, "me niliishi na mama yangu mdogo, alikuwa mkali kiasi kwamba nilikuwa nakosa hata uhuru katika maisha. Alinijengea mazingira ya kusoma kwa bidii 2 na kuachana michezo yote" nadhani hiyo inaweza kuwa ndio factor iliyopelekea me kuwa hivi
 
Pole zako,jitahidi kujichanganya halafu usiwaze sana kuhusu unachosema au kuongea
 
Pole sana, kwanza nikuulize swali kuhusu shule ulizopitia, ulikuwa unashiriki debate? au ulikuwa unakwepa? kama hukushiriki basi ulikosa kitu fulani cha kukujengea kujiamini mbele za watu. Anyway sio tatizo sana. kitu unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuanza kutoa fikra za uoga ulizo nazo kichwani, anza kuwa karibu na watu wanaoonyesha kukusikiliza na kukutia moyo katika yale unayoyasema na kufanya, tafuta mtu mwenye busara ambaye atakuwa ni mentor wako akusaidie kujenga kujiamini.

Mara nyingi mtu kama wewe unakuwa unaakiri "above average" na unajua mambo mengi na kwa jinsi ulivyojieleza unapenda kujifunza, anza sasa kuangalia hao marafiki zako wanakupa support unayiihitaji au ndo wanachangia kukuweka chini na kujiona kuwezi. Nakutakia kila la kheri na utafanikiwa.
 
the gratest secret for eliminating inferiority complex,which is another term for deep and pro found self doubt,is to fill your mind to overflowing with faith.
 
Thanx real deal kwa ushauri wako mzuri nimepata kitu kigeni toka kwako thanks
 
Sababu haukupewa haki ya kuongea na walio kulea.
Wazazi wengine wanafikiri mtoto haki ya kuongea hana, au kila anachoongea mtoto ni upuuzi kwao.
Hivo mtoto ataogopa kuongea, anaogopa kukosolewa na kukashfiwa.

Jinsi ya kutatua tatizo, anza kunywa bia na watu wasio kujua, mbali na unapoishi.
Halafu jifanye umelewa, ongea sana, hapo utakua unafanya mazoezi ya kuongea.
Kama masele cha pombe, jifanye unaangukia watu maksusi alafu unasema samahani. Na unaongea nao.


Hakuna binadam perfect, hivo kama unaogopa kuongea ili kasoro zako wasizione, utapata tabu maishani.
Watu wengine wanapenda watu wenye kasoro, au wale wasio ogopa kukosea.

Na wanao ogopa kukosea hawapendwi kabisa, sababu mtu mwisho ataogopa kukosea pia akiwa nawe.
Ndio maana wanakwita unaringa.
 
Pole sana, duniani hakuna binadamu ambaye yuko perfect katika kila idara. Bahati nzuri umeshajifahamu kwamba una woga wa kutoa mawazo yako mbele ya wazazi, ndugu na jamaa na marafiki si ajabu hata hapa JF unaweza kuendelea na hiyo tabia yako ya woga kuchangia mada mbali mbali hapa jamvini. Jitahidi ushiriki katika kutoa mawazo yako na tabia hii ya kujitenga na marafiki zako ipunguze sana kama utaweza kufanikisha haya basi labda woga uliokuwa nao utapungua sana au kumalizika kabisa. Kila la heri katika kupambana na woga uliokuwa nao.

Kwanza nianze na kujiamini. Hivi ni kitu gani kinasababish m2 kutojiamini? Maranying napenda kukaa na watu wenye uwelewa wa kutosha kuhusu mambo, napia napenda kujifunza zaid. Lakini nakuwa sijiamini hususani pale wanapo anzisha topic: nakuwa muoga kuchangia kabisa na ingali kichwani huwa nina point zuri 2 ya kuchangia lkn nasita kuipresent, mara chache sana ninapojikuta nimeropoka, huwa wanakubali point yangu na kuisuppot kwa asilimia kubwa. huwa najiuliza nini hasa kinanisibu mpaka nakuwa muoga? hii hali huwa inanitokea mara kwa mara hata nikiwa na wazazi nyumbani. Tatizo hili linanisumbua xana na pia huwa napenda kujitenga pekeyangu kwa mda mrefu bila kuonana na marafk na hata sometym wanapojaribu kuonana na me huwaga nawa chukia pasi na sababu. Hii inapelekea baadhi ya watu wanasema me naringa. lakini me siringi huwa natumia silaa hiyo kuficha udhaifu wangu 2. Nisaidieni wakubwa, nawasikiliza nyie
 
Ngoja umalize shule, ukishafanya interview mbili tatu utaanza kujiamini! Lol.
 
inaonekana ukiwa mdogo hukupewa muda wa kutosha kucheza na wenzako hivyo ulijijengea tabia ya kuwa mwenyewe hii ilikupunguzia uwezo wa kujiamini mbele ya wenzako.. pia ulifanya mambo yako kwa hofu ya mtu fulani (mfano: mzazi) zaidi ulifanya mambo yako kwa hofu pia ya kushindwa.. with all this and others adrenal glands were affected .. with this effects wakati unapotaka kufanya jambo lolote ambalo hujalizoea kwa haraka akili inatuma info kwa adrenal glands na kumwaga kemikali ambazo nizakujiandaa kushambulia.. ndipo hapo utakapo anza kuingiwa hofu..

ushauri tumia muda wako mwingi kuwa na marafiki mkishare ideas epuka kujitenga na wenzako kwa kukaa mwenyewe
pia acha kujiona unadharaulika itengeneze akili yako ujione wewe ni bora kuliko yeyote..

hope it helps
 
Pole sana. Utakua ulijeruhiwa ulipokua mdogo , hii ni ishara ya majeraha ya ndani . Waone watumishi wa Mungu watakuombea na utakua huru. Nami nilikua muoga sana nadhani kuzidi wewe.
 
Back
Top Bottom