Naweza kuwaelewa wanawake ila mwanaume unaendaje kanisa la mazingaombwe, muziki mnene na kumtolea sadaka mchungaji aishi kifahari ?

Naweza kuwaelewa wanawake ila mwanaume unaendaje kanisa la mazingaombwe, muziki mnene na kumtolea sadaka mchungaji aishi kifahari ?

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,455
Ni rahisi kuwaeliwa wanawake wanaoenda makanisa haya kwasababu wao wana hitilafu kidogo kwenye imani, ni rahisi kuvutwa na mazingira haya. Kwao haya makanisa ya miujiza, muziki mnene, ni kama sisi wanaume tunavyoangalia mpira zile kelele, shangwe, kutambiana na mpira ukiisha unasema “leo ilikuwa kali.”

Lakini mwanaume mzima, umepewa akili, macho yanaona vizuri, halafu unaenda haya makanisa ?

Unakaa dakika 10 tu tayari watu wanasukumwa wanaanguka kama majani ya mwembe. Wengine kila wiki wana mapepo yale yale. Najiuliza tu, bado hustuki tu ?

Halafu mchungaji anasema “mapepo yatoke!” mtu anaanguka. Lakini hujawahi kusikia “wagonjwa wote wa hospitali ya karibu wapone sasa hivi.” Hapo ndipo naanza kushuku hii ni trailer ya sinema fulani.

Katikati kanisa linageuka club ndogo. Muziki mnene, watu wanacheza kama sherehe ya kilabuni. Na wewe mwanaume umevaa suti yako nzuri unaanza kucheza bolingo kama uko kwenye TikTok challenge.

elimu yake ina mashaka au kwa uhakika alichonga O, sio ya ndevu ni ya form 4, confidence aliyonayo kwa kuona ana waumini wengi ataanza kuzungumzia vitu vya uchumi, geo politics, n.k. wale wasaidizi wake wanashangilia hata anapochanganya mafaili na wewe upo bize unatikisa kichwa, are u ok ?

Mchungaji meanwhile anaishi maisha ya kifahari, gari kali, suti kali, watoto shule kali. Wewe sadaka yako ndiyo nishati yake, lakini bado unapiga kelele “Mimi ni mshindi!” mpaka macho yanatoka kama umebanwa na mkanda wa suruali.

Halafu mwisho unaambiwa nunua maji ya upako na keki ya upako laki moja. Mimi hapo huwa najiuliza: imani yako imefikia level ambayo hata maji ya bomba hayakusaidii mpaka yawe na brand ya mchungaji?

Na sasa kuna ile nyingine ya ajabu zaidi. Unaambiwa “mkemee shetani kwa saa nzima!” watu wanapiga kelele “toka! toka! toka!” kama wanagombana na mbu chumbani. Wengine wanaambiwa watoke nje wachape ardhi kwa viboko wakimkemea shetani. Zimo kichwani kweli ?
 
Kwa wanawake naweza kuwaelewa wana udhaifu sana kwenye imani ni rahisi kurubuniwa, kwao aina hii ya makanisa ni kama sisi tunavyoangalia mpira.

Lakini kwa mwanaume wenye akili zake aliepewa advantage kwenye uono kweli unaendaje haya makanisa

Kanisa limejikita zaidi na miujiza, kinachoendelea ni mazingaombwe ya kusukuma watu waanguke, wengine unawaona kila wiki wanakuja kanisani na mapepo wanaanguka husutuki tu ? hujiulizagi kwanini wachungaji hao hawaendi mahospitalini ?

Kanisa ni muziki mnene na kucheza kwa fujo, na wewe kwa akili zako unaamka kuunga treila unaanza kucheza bolingo, na wewe upo proud kabisa

Mchungaji anaishi maisha ya kifahari, ana gari nzuri, watoto wake wanasoma shule nzuri, anavaa vizuri, hustuki tu sadaka yako ndio humtajirisha ? anavyoondoka anasema pigeni kelele mimi ni mshindi na wewe unapiga kelele macho yamekutoka kama umekabwa eti mshindi.

Unanunua keki na maji ya upako hadi laki 1, kwamba umeona imani yako ni dhaifu kuzidi hayo maji ?
Vijana kama aliekatakamba humutuu, na Minjingu Jingu huwambii kitu kuhusu haya makanisa.
 
Hua nakutana na akina mama wanatembea kwa miguu kutoka kwa mwamposa, watoto mgongoni, wamepauka, wamechoka 😂

Asante mwamposa kwa kuwanyoosha wapuuzi
 
Katikati kanisa linageuka club ndogo. Muziki mnene, watu wanacheza kama sherehe ya kilabuni. Na wewe mwanaume umevaa suti yako nzuri unaanza kucheza bolingo kama uko kwenye TikTok challenge.
Hahaha umenikumbusha mbali sana tulikua tunaliita Diisco la Yesu enzi hizo acha kabisa unacheza staili zote hadi WaCkoJako na hakuna anaekuuliza hahaha
 
Sema jamaa kawakamata,nadhani kuna wakati akikaa na mkewe ndani wanacheeeka jinsi wamefanya watu mazombi🤣🤣🤣🤣🤣
Wanaanza kudiscuss uponyaji wa michongo aliyokuwa anaifanya 😂
 
Wamerogwa akili hawawezi kuelewa lolote, wamejazana ktk hayo makanisa wakisubiri miujiza na matendo ya maajabu which is nonsense.

Sio makanisa hayo tu, kitendo cha kupeleka sadaka kanisani/misikitin huo ni ujinga, maana Mungu wao ndie mwenye majukumu ya kuwalisha hao wachungaji/viongozi wa kidini wanaofanya hiyo kazi yake, na si wewe mfuasi.

Mungu kashindwa kuwabariki viongozi wa kidini anakusubiri wewe muumini ujinyime ndipo uwape?, yaani kiufupi ukitoa sadaka huna utofauti na anayehonga/kutoa rushwa kwa madhumuni ya kusaidiwa jambo.

Unatoa sadaka ili ubarikiwe, unatoa sadaka ili upone/mambo yako yaende sawa, yaani unamshawishi Mungu mmiliki wa mali zote ikiwepo unazomiliki wewe, unachukua unamrudishia ili akutatulie shida zako huu ni UPUMBAVU wa kiwango kikubwa.

Tuamke jamani tuache upumbavu.
 
Mambo ya imani usipokuwa wa imani hutayaelewa abadani. Siwezi kamwe kubeza imani ya mtu.

Ndio maana kwa waganga unamkuta mheshimiwa uchi wa mnyama anachanjwa chale. Yote ni kuamini
 
Mambo ya imani usipokuwa wa imani hutayaelewa abadani. Siwezi kamwe kubeza imani ya mtu.

Ndio maana kwa waganga unamkuta mheshimiwa uchi wa mnyama anachanjwa chale. Yote ni kuamini
Nakazia hapa.Sijui kwanini watu wameshupalia Sana imani za watu
 
Back
Top Bottom