Naweza kuanza tuisheni ya advance (PCB)

Naweza kuanza tuisheni ya advance (PCB)

Pure Scientific

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2015
Posts
716
Reaction score
644
Kwanza natakunguliza shukran kwa wadau wa elimu ktk jukwaa hili mimi ni mwanafunzi niliyemaliza form four mwaka huu 2015 napenda kuuliza je ninaweza kuanza tuishen ya advance kwa mchepuo wa pcb hata kabla ya matokeo kwa sababu na itaji kujiandaa mapema ili nifanye vema advnce.....asante naombeni ushaur wadau
 
Anzaga tu dogo....hasa za mnyama physics
 
mbona naambiwa ni ngumu inahitaji maandalizi ya kutosha

Hakuna ugumu mbele ya maandalizi. Tatizo huwa ni muda kuwa mchache na mambo ya kusoma kuwa mengi, kama kuna uwezekano nakushauri KWA SAUTI KUBWA uanze sasa hivi.

Ukifika shuleni kazi yako itakuwa ni kupalilia tu na si kulima tena, huku ukisubili wakati wa mavuno(Nadhani hapa unenielewa)

Hii itakusaidia katika kuhakikisha kuwa
"The more often you revise the better will be your memoryi"
 
Hakuna ugumu mbele ya maandalizi. Tatizo huwa ni muda kuwa mchache na mambo ya kusoma kuwa mengi, kama kuna uwezekano nakushauri KWA SAUTI KUBWA uanze sasa hivi.

Ukifika shuleni kazi yako itakuwa ni kupalilia tu na si kulima tena, huku ukisubili wakati wa mavuno(Nadhani hapa unenielewa)

Hii itakusaidia katika kuhakikisha kuwa
"The more often you revise the better will be your memoryi"

asnte bro maana watu walikuwa wananitsha inabidi nianze mapema kwa kuwa nataka nipasue advance.......
 
Mkuu,

Kwanza hongera kwa kusoma PCB.

Ushauri wangu, soma sana Physics na Chemistry (high priority). Ukifanya hivi una chance kubwa ya kupata A kwenye masomo haya.

Ukisoma yote matatu kwa uzito unaolingana una chance kubwa ya kupata wastani au chini ya wastani na hivyo kuathiri matokeo yako ya jumla.

Tafakari.
 
Mkuu,

Kwanza hongera kwa kusoma PCB.

Ushauri wangu, soma sana Physics na Chemistry (high priority). Ukifanya hivi una chance kubwa ya kupata A kwenye masomo haya.

Ukisoma yote matatu kwa uzito unaolingana una chance kubwa ya kupata wastani au chini ya wastani na hivyo kuathiri matokeo yako ya jumla.

Tafakari.

lakini kwa nin nisiipe uzito zaidi biology na chemia kwanza na matokeo yakitoka nipige phy
 
Kama una uwezo mkubwa sio lazima uanze sasa....Unaweza kuta umepumzika unawasaidia wazazi nyumbani

Ila kama una uwezo wa kawaida,ni vema ukaanza kusoma now hasa hasa pyhisics ndio walimu wake ni wachache,na ina mambo mengi

Kila la heri daktari matarajiwa,Mungu na aitimilize ndoto yako
 
sasa usome wakati matokeo bado mbona una kihelehele we kijana je kama umefeli? subir matokeo yatoke ndo ujue we unaweza nunua nguo za mtoto wa kiume wakati mimba changa je akizaliwa wa kike? subir matokeo tatizo vijana BRN
 
Kinacho hitajika ni kujituma tuition haita kusaidia kitu kama hutajituma.All da best
 
lakini kwa nin nisiipe uzito zaidi biology na chemia kwanza na matokeo yakitoka nipige phy

Kwa habari ya 'twisheni' soma sana biology na physics. Ila biology iwe zaidi. Kemia haina shida sana na si lazima usome 'twisheni'.

usisahau, usije ukaweka 'weight' sawa kwenye kusoma hayo masomo matatu. Nazungumza kutokana na uzoefu.

Tafakari.
 
sasa usome wakati matokeo bado mbona una kihelehele we kijana je kama umefeli? subir matokeo yatoke ndo ujue we unaweza nunua nguo za mtoto wa kiume wakati mimba changa je akizaliwa wa kike? subir matokeo tatizo vijana BRN

ninauhakika mkubwa wa kufaulu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom