Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,157
- 4,454
Wadau mwenzenu nipo kwenye wakati mgumu sana psychologicaly, kuna dada anataka kuachika kwasababu yangu ilihali hana kosa lolote....Ishu iko hivi Kuna dada(mke wa mtu) nipo naye karibu sana kikazi, siku asipokuwepo ofisini kuna baadhi ya kazi zake hunachia nimsaidie namimi nisipokuwepo ofisini naye hunipa ushirikiano wa hivyo kutokana na nature ya kazi zetu kufanana sana.
Kutokana na ukaribu huu mmewe alianza kuwa na wasiwasi namimi, kwasababu kuna siku nilimpigia simu mkewe akapokea yeye bila hata kujibu salamu yangu akaniuliza shida yangu ni nini? mimi nikamueleza kwamba shida yangu ni ya kikazi nataka kuongea na mkewe,..... kumbe alikuwa naye jirani akampatia nikaongea naye, yalikuwa ni masuala ya kikazi tu yaliyohitaji ufafnuzi wa sekunde chache tu alafu zilikuwa ni saa za kazi, ishu ni kwamba huyu dada na mmewe walikuwa likizo.
Hivi majuzi huyu dada aliwahi kidogo kutoka ofisini kwasababu alikuwa anawahi kumpokea mmewe Airport alikuwa ametokea nje ya nchi kusimamia matibabu ya ndugu yake, all the way kwenda airpot na kuelekea nyumbani kwao tukawa tunawasiliana na huyu dada kuhusiana na vikazi alivyoniachia pale kazini nimsaidie mpaka nilipomaliza mida ya saa2 usiku.
Nikiwa nyumbani mida ya saa4 usiku mwanangu wa miaka3 alichukua simu yangu ikiwa chumbani mimi nikiwa sebureni akawa anaichezea, kwa bahati mbaya akapiga simu kwenda kwa yule dada ikapokelewa na mmewe kila akiongea simu yangu ilikuwa kimya maana alikuwa anaichea mtoto na hakujua kama kapiga simu. baadaye kidogo akapiga yeye, mwanangu akaniletea simu nilipoipokea kumbe ni yule bwana anapiga akaniambia maneno machache tu "HAJAKWAMBIA KWAMBA NIMERUDI? KUANZIA SASA NIMEKUACHIA" nilipojaribu kutaka kujua zaidi nini kinaendelea akanikatia simu, kila nikipiga simu ikawa haipokelewi, kwenye mida ya saa6 usiku akapiga yule dada akiwa amepigwa na kahifadhiwa kwa jirani ndipo nilipogundua nini kilitokea, nimejaribu kumuomba huyu jamaa tuonane tuongee ameniambia nikae mbali naye.
Wadau naombeni ushauri nimsaidieje huyu dada ili kuokoa ndoa yake maana jana amerudi nyumbani kwake lakini mmewe hamsemeshi kitu chochote, akijaribu kumuelewesha anamuambia aje kwangu yeye hataki kuishi naye, najisikia vibaya sana kwasababu mimi ndiyo chanzo na naofia maisha yangu kujisogeza kwenda kunusuru hii ndoa.
Kutokana na ukaribu huu mmewe alianza kuwa na wasiwasi namimi, kwasababu kuna siku nilimpigia simu mkewe akapokea yeye bila hata kujibu salamu yangu akaniuliza shida yangu ni nini? mimi nikamueleza kwamba shida yangu ni ya kikazi nataka kuongea na mkewe,..... kumbe alikuwa naye jirani akampatia nikaongea naye, yalikuwa ni masuala ya kikazi tu yaliyohitaji ufafnuzi wa sekunde chache tu alafu zilikuwa ni saa za kazi, ishu ni kwamba huyu dada na mmewe walikuwa likizo.
Hivi majuzi huyu dada aliwahi kidogo kutoka ofisini kwasababu alikuwa anawahi kumpokea mmewe Airport alikuwa ametokea nje ya nchi kusimamia matibabu ya ndugu yake, all the way kwenda airpot na kuelekea nyumbani kwao tukawa tunawasiliana na huyu dada kuhusiana na vikazi alivyoniachia pale kazini nimsaidie mpaka nilipomaliza mida ya saa2 usiku.
Nikiwa nyumbani mida ya saa4 usiku mwanangu wa miaka3 alichukua simu yangu ikiwa chumbani mimi nikiwa sebureni akawa anaichezea, kwa bahati mbaya akapiga simu kwenda kwa yule dada ikapokelewa na mmewe kila akiongea simu yangu ilikuwa kimya maana alikuwa anaichea mtoto na hakujua kama kapiga simu. baadaye kidogo akapiga yeye, mwanangu akaniletea simu nilipoipokea kumbe ni yule bwana anapiga akaniambia maneno machache tu "HAJAKWAMBIA KWAMBA NIMERUDI? KUANZIA SASA NIMEKUACHIA" nilipojaribu kutaka kujua zaidi nini kinaendelea akanikatia simu, kila nikipiga simu ikawa haipokelewi, kwenye mida ya saa6 usiku akapiga yule dada akiwa amepigwa na kahifadhiwa kwa jirani ndipo nilipogundua nini kilitokea, nimejaribu kumuomba huyu jamaa tuonane tuongee ameniambia nikae mbali naye.
Wadau naombeni ushauri nimsaidieje huyu dada ili kuokoa ndoa yake maana jana amerudi nyumbani kwake lakini mmewe hamsemeshi kitu chochote, akijaribu kumuelewesha anamuambia aje kwangu yeye hataki kuishi naye, najisikia vibaya sana kwasababu mimi ndiyo chanzo na naofia maisha yangu kujisogeza kwenda kunusuru hii ndoa.