Naunga mkono maneno ya Rais, tumekulia na kulelewa mazingira tofauti

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,052
Kuna watu wamekulia na kulelewa mazingira ambayo wamezoea kuwaona wazaxlzi wao wakiamka na kushinda kwenye bao na kupiga porojo, wakicheka wakati wote na kufurahi. Wakitoka hapo wanaenda kwenye kahawa, na pengine kwenye ngoma.

Na hawa ikatokea bahati mbaya, mzazi akaondoka Duniani, matanga yakiisha tu wanaanza kumtafuta mteja wa kununua nyumba ya marehemu baba yao, mashamva ya marehemu, n.k.. Wakizidiwa watauza mpaka nguo za marehemu.

Hawa ndio wale wakakosa mlo, watauza mpaka kitanda. Wakipata hela ya mauzo ya kitanda watakula pilau na biriani mpaka hela iishe. Ikiisha watatafuta kingine cha kuuza. Kama wana binti, watalazimishe aolewe haraka ili mahari iokoe njaa ya nyumbani. Binti akitoka nyumbani, akashinda kusikoeleweka lakini jioni akarudi na mchele, kuku, mdalasini, pilipili Manga, watamsifia kweli kuwa anawathamini wazazi wake.

Sasa ikatokea bahati, watu waliokulia mazingira ya namna hiyo wakaupata uongozi, cha kwanza wataanza kuangalia nini cha kuuza. Watauza mbuga za wanyama, watauza ardhi na mapori yote, watauza bandari. Na kama kungekuwa na soko la kuuza binadamu, wakiishiwa kabisa, watapenda wauze mpaka binadamu wenzao. Wao fikra zao ni kuwa ili upate fedha ni lazima uuze, uuze kila unachokiona. Wanaamini kuwa waliotangulia hawakuuza kwa savabu walikuwa hawana uwezo wa kuwatafuta wanunuzi. Hawa hawana mawazo ya kuzalisha, kwao maisha ili yawe mazuri wanaamini suluhisho ni kuuza ambavyo hawakuvitengeneza, na kwamba wakati wote havikosekani vya kuuza.

Kwa upande mwingine, wapo wanaoamini kuwa kuishi kwa kusubiria mzazi wako afe ili urithi mali ni laana. Wanawafundisha watoto wao namna ya kutumia vinavyowazunguka katika kuzalisha. Wamekulia katika mazingira ambayo kila aliyepo nyumbani anajivunia kufanya kitu, na ndiyo fahari yake. Ikatokea mwanafamilia kauza shamba, ukoo mzima unamjia na kumhoji kuna nini, maana ameuza sehemu aliyostahili kuzalishia.

Aliyekulia na kuelelwa mazingira ya hivyo, akiupata uongozi lazima kutakuwa na tofauti kubwa. Kwake rasilimali asilia ataziona ni vizalishia mali na siyo bidhaa ya kuiuza. Anayeiuza ataonekana ni adui wa jamii nzima na muuji wa vizazi vijavyo.

Katika mazingira haya mawili tofauti, mwanaJF yumkini una kundi lako unalilona kuwa lipo sahihi, lakini ndivyo jamii yetu ilivyojengeka.
 
Kuna watu wamekulia na kulelewa mazingira ambayo wamezoea kuwaona wazaxlzi wao wakiamka na kushinda kwenye bao na kupiga porojo, wakicheka wakati wote na kufurahi. Wakitoka hapo wanaenda kwenye kahawa, na pengine kwenye ngoma.

Na hawa ikatokea bahati mbaya, mzazi akaondoka Duniani, matanga yakiisha tu wanaanza kumtafuta mteja wa kununua nyumba ya marehemu baba yao, mashamva ya marehemu, n.k.. Wakizidiwa watauza mpaka nguo za marehemu.

Hawa ndio wale wakakosa mlo, watauza mpaka kitanda. Wakipata hela ya mauzo ya kitanda watakula pilau na biriani mpaka hela iishe. Ikiisha watatafuta kingine cha kuuza. Kama wana binti, watalazimishe aolewe haraka ili mahari iokoe njaa ya nyumbani. Binti akitoka nyumbani, akashinda kusikoeleweka lakini jioni akarudi na mchele, kuku, mdalasini, pilipili Manga, watamsifia kweli kuwa anawathamini wazazi wake.

Sasa ikatokea bahati, watu waliokulia mazingira ya namna hiyo wakaupata uongozi, cha kwanza wataanza kuangalia nini cha kuuza. Watauza mbuga za wanyama, watauza ardhi na mapori yote, watauza bandari. Na kama kungekuwa na soko la kuuza binadamu, wakiishiwa kabisa, watapenda wauze mpaka binadamu wenzao. Wao fikra zao ni kuwa ili upate fedha ni lazima uuze, uuze kila unachokiona. Wanaamini kuwa waliotangulia hawakuuza kwa savabu walikuwa hawana uwezo wa kuwatafuta wanunuzi. Hawa hawana mawazo ya kuzalisha, kwao maisha ili yawe mazuri wanaamini suluhisho ni kuuza ambavyo hawakuvitengeneza, na kwamba wakati wote havikosekani vya kuuza.

Kwa upande mwingine, wapo wanaoamini kuwa kuishi kwa kusubiria mzazi wako afe ili urithi mali ni laana. Wanawafundisha watoto wao namna ya kutumia vinavyowazunguka katika kuzalisha. Wamekulia katika mazingira ambayo kila aliyepo nyumbani anajivunia kufanya kitu, na ndiyo fahari yake. Ikatokea mwanafamilia kauza shamba, ukoo mzima unamjia na kumhoji kuna nini, maana ameuza sehemu aliyostahili kuzalishia.

Aliyekulia na kuelelwa mazingira ya hivyo, akiupata uongozi lazima kutakuwa na tofauti kubwa. Kwake rasilimali asilia ataziona ni vizalishia mali na siyo bidhaa ya kuiuza. Anayeiuza ataonekana ni adui wa jamii nzima na muuji wa vizazi vijavyo.

Katika mazingira haya mawili tofauti, mwanaJF yumkini una kundi lako unalilona kuwa lipo sahihi, lakini ndivyo jamii yetu ilivyojengeka.
Watakuelewa wachache sana
 
Hakika, Tamaduni zina athari kubwa sana kwa binadamu yeyote. Mnapokuwa watu wa tamaduni nyingi tofauti inaweza kuwa vigumu sana kuelewana na kukubaliana muelekeo wapi na namna ya kuelekea huko.
 
Kuna watu wamekulia na kulelewa mazingira ambayo wamezoea kuwaona wazaxlzi wao wakiamka na kushinda kwenye bao na kupiga porojo, wakicheka wakati wote na kufurahi. Wakitoka hapo wanaenda kwenye kahawa, na pengine kwenye ngoma.

Na hawa ikatokea bahati mbaya, mzazi akaondoka Duniani, matanga yakiisha tu wanaanza kumtafuta mteja wa kununua nyumba ya marehemu baba yao, mashamva ya marehemu, n.k.. Wakizidiwa watauza mpaka nguo za marehemu.

Hawa ndio wale wakakosa mlo, watauza mpaka kitanda. Wakipata hela ya mauzo ya kitanda watakula pilau na biriani mpaka hela iishe. Ikiisha watatafuta kingine cha kuuza. Kama wana binti, watalazimishe aolewe haraka ili mahari iokoe njaa ya nyumbani. Binti akitoka nyumbani, akashinda kusikoeleweka lakini jioni akarudi na mchele, kuku, mdalasini, pilipili Manga, watamsifia kweli kuwa anawathamini wazazi wake.

Sasa ikatokea bahati, watu waliokulia mazingira ya namna hiyo wakaupata uongozi, cha kwanza wataanza kuangalia nini cha kuuza. Watauza mbuga za wanyama, watauza ardhi na mapori yote, watauza bandari. Na kama kungekuwa na soko la kuuza binadamu, wakiishiwa kabisa, watapenda wauze mpaka binadamu wenzao. Wao fikra zao ni kuwa ili upate fedha ni lazima uuze, uuze kila unachokiona. Wanaamini kuwa waliotangulia hawakuuza kwa savabu walikuwa hawana uwezo wa kuwatafuta wanunuzi. Hawa hawana mawazo ya kuzalisha, kwao maisha ili yawe mazuri wanaamini suluhisho ni kuuza ambavyo hawakuvitengeneza, na kwamba wakati wote havikosekani vya kuuza.

Kwa upande mwingine, wapo wanaoamini kuwa kuishi kwa kusubiria mzazi wako afe ili urithi mali ni laana. Wanawafundisha watoto wao namna ya kutumia vinavyowazunguka katika kuzalisha. Wamekulia katika mazingira ambayo kila aliyepo nyumbani anajivunia kufanya kitu, na ndiyo fahari yake. Ikatokea mwanafamilia kauza shamba, ukoo mzima unamjia na kumhoji kuna nini, maana ameuza sehemu aliyostahili kuzalishia.

Aliyekulia na kuelelwa mazingira ya hivyo, akiupata uongozi lazima kutakuwa na tofauti kubwa. Kwake rasilimali asilia ataziona ni vizalishia mali na siyo bidhaa ya kuiuza. Anayeiuza ataonekana ni adui wa jamii nzima na muuji wa vizazi vijavyo.

Katika mazingira haya mawili tofauti, mwanaJF yumkini una kundi lako unalilona kuwa lipo sahihi, lakini ndivyo jamii yetu ilivyojengeka.

Andiko la akili kubwa.
Ndiyo uhalisia wa Maisha yetu.
Kuna hili lingine la kuishi maisha ya Tamaa na wivu.
 
Hakika, Tamaduni zina athari kubwa sana kwa binadamu yeyote. Mnapokuwa watu wa tamaduni nyingi tofauti inaweza kuwa vigumu sana kuelewana na kukubaliana muelekeo wapi na namna ya kuelekea huko.
Na hasa pale kila mmoja anapoamini utamaduni wake ndiyo bora, wakati ni ukweli kuwa kuna tamaduni zinafifisha ustawi wa jamii husika.
 
Inajulikana wanaoshinda kwenye vigenge vya bao na kahawa mpaka jioni bila kujishugurisha ni watu wa wapi. Na hii ni asili yao kama mleta mada alivyosema. Tusichelewe muuza Mali za umma
 
Sasa ikatokea bahati, watu waliokulia mazingira ya namna hiyo wakaupata uongozi, cha kwanza wataanza kuangalia nini cha kuuza. Watauza mbuga za wanyama, watauza ardhi na mapori yote, watauza bandari. Na kama kungekuwa na soko la kuuza binadamu, wakiishiwa kabisa, watapenda wauze mpaka binadamu wenzao. Wao fikra zao ni kuwa ili upate fedha ni lazima uuze, uuze kila unachokiona. Wanaamini kuwa waliotangulia hawakuuza kwa savabu walikuwa hawana uwezo wa kuwatafuta wanunuzi. Hawa hawana mawazo ya kuzalisha, kwao maisha ili yawe mazuri wanaamini suluhisho ni kuuza ambavyo hawakuvitengeneza, na kwamba wakati wote havikosekani vya kuuza.

Kwa upande mwingine, wapo wanaoamini kuwa kuishi kwa kusubiria mzazi wako afe ili urithi mali ni laana. Wanawafundisha watoto wao namna ya kutumia vinavyowazunguka katika kuzalisha. Wamekulia katika mazingira ambayo kila aliyepo nyumbani anajivunia kufanya kitu, na ndiyo fahari yake. Ikatokea mwanafamilia kauza shamba, ukoo mzima unamjia na kumhoji kuna nini, maana ameuza sehemu aliyostahili kuzalishia.
🤔
 
Kuna watu wamekulia na kulelewa mazingira ambayo wamezoea kuwaona wazaxlzi wao wakiamka na kushinda kwenye bao na kupiga porojo, wakicheka wakati wote na kufurahi. Wakitoka hapo wanaenda kwenye kahawa, na pengine kwenye ngoma.

Na hawa ikatokea bahati mbaya, mzazi akaondoka Duniani, matanga yakiisha tu wanaanza kumtafuta mteja wa kununua nyumba ya marehemu baba yao, mashamva ya marehemu, n.k.. Wakizidiwa watauza mpaka nguo za marehemu.

Hawa ndio wale wakakosa mlo, watauza mpaka kitanda. Wakipata hela ya mauzo ya kitanda watakula pilau na biriani mpaka hela iishe. Ikiisha watatafuta kingine cha kuuza. Kama wana binti, watalazimishe aolewe haraka ili mahari iokoe njaa ya nyumbani. Binti akitoka nyumbani, akashinda kusikoeleweka lakini jioni akarudi na mchele, kuku, mdalasini, pilipili Manga, watamsifia kweli kuwa anawathamini wazazi wake.

Sasa ikatokea bahati, watu waliokulia mazingira ya namna hiyo wakaupata uongozi, cha kwanza wataanza kuangalia nini cha kuuza. Watauza mbuga za wanyama, watauza ardhi na mapori yote, watauza bandari. Na kama kungekuwa na soko la kuuza binadamu, wakiishiwa kabisa, watapenda wauze mpaka binadamu wenzao. Wao fikra zao ni kuwa ili upate fedha ni lazima uuze, uuze kila unachokiona. Wanaamini kuwa waliotangulia hawakuuza kwa savabu walikuwa hawana uwezo wa kuwatafuta wanunuzi. Hawa hawana mawazo ya kuzalisha, kwao maisha ili yawe mazuri wanaamini suluhisho ni kuuza ambavyo hawakuvitengeneza, na kwamba wakati wote havikosekani vya kuuza.

Kwa upande mwingine, wapo wanaoamini kuwa kuishi kwa kusubiria mzazi wako afe ili urithi mali ni laana. Wanawafundisha watoto wao namna ya kutumia vinavyowazunguka katika kuzalisha. Wamekulia katika mazingira ambayo kila aliyepo nyumbani anajivunia kufanya kitu, na ndiyo fahari yake. Ikatokea mwanafamilia kauza shamba, ukoo mzima unamjia na kumhoji kuna nini, maana ameuza sehemu aliyostahili kuzalishia.

Aliyekulia na kuelelwa mazingira ya hivyo, akiupata uongozi lazima kutakuwa na tofauti kubwa. Kwake rasilimali asilia ataziona ni vizalishia mali na siyo bidhaa ya kuiuza. Anayeiuza ataonekana ni adui wa jamii nzima na muuji wa vizazi vijavyo.

Katika mazingira haya mawili tofauti, mwanaJF yumkini una kundi lako unalilona kuwa lipo sahihi, lakini ndivyo jamii yetu ilivyojengeka.
Ndugu yangu elewa pia huko unakokusema wanacheza bao ni kweli wanacheza kwa kuwa mtu anamiliki boti zake za uvuvi anakabidhi watu wenye shida ya ajira wakavue kutumia boti hizo wakirudi asubuhi wanampatia mmiliki fedha ya siku hiyo ya kukodishwa na pia samaki wa mlo na kuuza akitaka, basi wote wameingiza siku sio lazima uende kuvua kwa kuwa boti ni yako na ndio maana watu wake wanaamani na maisha mazuri kwa kuwa maisha ni akili wala sio nguvu na waloshaelewa nini maana ya kuwa na vitega uchumi.
Pili ulishapata jenga kijumba chako kariakoo ukampata muwekezaji kwa makubaliano ya kukavunja kajumba na kujenga ghorofa 8 umepewa flat 2 na fremu 6 baada ya miaka 30 ghorofa lote linakuwa mali yako hapo hapo umekodisha fremu na hiyo flat moja unakipato cha kukutosha kuendesha maisha yako si unajua bei za kariakoo kupangisha sasa kwa nini watu wasicheze bao ( wenzetu nyie wazungu mnaita early retirement) wanauhakika wa cashflow na maisha kula vizuri , kuvaa vizuri, kulala pazuri na kuweka mafuta ya gari kwa kutumia akili zao maisha ni akili fursa zipo tumia kuongeza kipato maana huwezi kungangania eti usikodishe boti ama usimpe mtu kijumba kivunjwe ajenge ghorofa nawe mufaidike wote kisa tu kuna tu vimaneno endeleeni kusema watu wako bize kutafuta bajeti huru isiyohitaji mkopo wala kuombaomba kupitia uwekezaji wenye tija ya kupandisha pato.
 
Akili ndogo siku zote hupenda mambo mapesi kwenye mambo magumu,ambayo huhitaji tafakari ya kina na yenye weledi mkubwa.

Mazingira huwa ni nyenzo muhimu katika kujenda fikra na athari za akili kwa mwanadamu yoyote,na katika hili mleta uzi umeongea jambo kubwa sana.
 
Nyinyi mliolelewa vizuri mmetatua changamoto zinazowakabili wananchi kwa kiwango gani?. Mbona mmejawa na ubinafsi hivyo.
 
Nyinyi mliolelewa vizuri mmetatua changamoto zinazowakabili wananchi kwa kiwango gani?. Mbona mmejawa na ubinafsi hivyo.
Waliolelewa vizuri ni akina nani, na wana ubinafsi upi? Fafanua.
 
Ndugu yangu elewa pia huko unakokusema wanacheza bao ni kweli wanacheza kwa kuwa mtu anamiliki boti zake za uvuvi anakabidhi watu wenye shida ya ajira wakavue kutumia boti hizo wakirudi asubuhi wanampatia mmiliki fedha ya siku hiyo ya kukodishwa na pia samaki wa mlo na kuuza akitaka, basi wote wameingiza siku sio lazima uende kuvua kwa kuwa boti ni yako na ndio maana watu wake wanaamani na maisha mazuri kwa kuwa maisha ni akili wala sio nguvu na waloshaelewa nini maana ya kuwa na vitega uchumi.
Pili ulishapata jenga kijumba chako kariakoo ukampata muwekezaji kwa makubaliano ya kukavunja kajumba na kujenga ghorofa 8 umepewa flat 2 na fremu 6 baada ya miaka 30 ghorofa lote linakuwa mali yako hapo hapo umekodisha fremu na hiyo flat moja unakipato cha kukutosha kuendesha maisha yako si unajua bei za kariakoo kupangisha sasa kwa nini watu wasicheze bao ( wenzetu nyie wazungu mnaita early retirement) wanauhakika wa cashflow na maisha kula vizuri , kuvaa vizuri, kulala pazuri na kuweka mafuta ya gari kwa kutumia akili zao maisha ni akili fursa zipo tumia kuongeza kipato maana huwezi kungangania eti usikodishe boti ama usimpe mtu kijumba kivunjwe ajenge ghorofa nawe mufaidike wote kisa tu kuna tu vimaneno endeleeni kusema watu wako bize kutafuta bajeti huru isiyohitaji mkopo wala kuombaomba kupitia uwekezaji wenye tija ya kupandisha pato.
Lakini kuna maswali ya kujiuliza, kama unashinda unacheza bao, hiyo pesa ya kununulia boti za uvuvi au jengo la kupangisha, ulizipata wapi na kwa namna gani? Uliuza ardhi ya urithi? Au nyumba ya urithi? Hata kama umerithi, ujue alikuwepo ambaye hakuwa anashinda anacheza bao, ndiye aliyetengeneza huo urithi ambao wewe baadaye unaukodisha.

Kama ni mali za urithi (maana boti za kukodisha haziwezi kudondoka kama mvua), bado utakuwa unaniunga mkono kwamba, hao wacheza bao watakuwa wamelelewa katika mazingira ya kusubiria wengine wafe ili warithi. Au wanasubiria mahari ya binti ili wakanunue mtumbwi.

Nashukuru kwa kuniunga mkono kuwa wa jamii hiyo, fikra zao huwa ni kuuza na siyo kuzalisha. Babu zao waliwarithisha ardhi na nyumba za makuti Kariakoo, walipofariki baba zao, wao wakafanya kazi ya kuuza. Walionunua, wale Wakinga wa Njombe, wanaoamini katika kuzalisha, wakazivunja nyumba mbovu, na kujenga majengo ya ghorofa. Hakuna ugomvi. Kwa sababu wakinga wamenunua majengo mabovu kwa jasho lao, na wacheza bao wamepewa kilicho chao, wanacheza bao huku wakiwa na uhakika wa kula biriani na pilau, huku wakifikiria wauze nini tena.
 
Lakini kuna maswali ya kujiuliza, kama unashinda unacheza bao, hiyo pesa ya kununulia boti za uvuvi au jengo la kupangisha, ulizipata wapi na kwa namna gani? Uliuza ardhi ya urithi? Au nyumba ya urithi? Hata kama umerithi, ujue alikuwepo ambaye hakuwa anashinda anacheza bao, ndiye aliyetengeneza huo urithi ambao wewe baadaye unaukodisha.

Kama ni mali za urithi (maana boti za kukodisha haziwezi kudondoka kama mvua), bado utakuwa unaniunga mkono kwamba, hao wacheza bao watakuwa wamelelewa katika mazingira ya kusubiria wengine wafe ili warithi. Au wanasubiria mahari ya binti ili wakanunue mtumbwi.

Nashukuru kwa kuniunga mkono kuwa wa jamii hiyo, fikra zao huwa ni kuuza na siyo kuzalisha. Babu zao waliwarithisha ardhi na nyumba za makuti Kariakoo, walipofariki baba zao, wao wakafanya kazi ya kuuza. Walionunua, wale Wakinga wa Njombe, wanaoamini katika kuzalisha, wakazivunja nyumba mbovu, na kujenga majengo ya ghorofa. Hakuna ugomvi. Kwa sababu wakinga wamenunua majengo mabovu kwa jasho lao, na wacheza bao wamepewa kilicho chao, wanacheza bao huku wakiwa na uhakika wa kula biriani na pilau, huku wakifikiria wauze nini tena.
Watu wanatafuta wanapata ndio wanacheza bao ukishakuwa na uhakika wa investment zinaleta fedha ya kufanya mambo yako unapata jeuri , huwezi kwenda kucheza bao kama huna uhakika wa chakula ,malazi na mavazi, haijalishi wamerithi au wamezipata vipi hizo ni mali zao kama nyie wengine babu zenu hawakufanya wakati hawa wengine babu zao walihakikishia kizazi hadi kizazi uhakika wa maisha tunawapa heko wao na mila zao na tamaduni zao za kuwafanya wawe wanafurahia maisha kwa kizungu tunasema babu ametengeneza genaration fortune acha watu waenjoy, na sie ambao hatuna acha tutafutie generation zetu wealth kwa kutumia akili.
 
Back
Top Bottom