Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Wewe ni mbumbumbu na kwa tabia yako hiyo ya kuendekeza vya kupewa bure utaendelea kuwa mbumbumbu wa kudumu,yaani huwezi kuchagua post gani ya kuchangia kizalendo?Kikao cha bunge ni kikao cha kikazi sio mkutano na waandishi wa habari (press conference).kuna tofauti ya kikao cha kikazi na press conference! Wanaotaka kugeuza bunge kuwa press conference ambamo muda wote waandishi wa habari wamo hawako sahihi
Wabunge wakishakaa na kumaliza kazi ya siku ndio taarifa za yale muhimu ya kazi na matokeo waliyofikia yanawekwa hadharani na maofisa habari wa bunge
Taarifa hizo haziwi na vitu vya kipuuzi kama vile vya mbunge gani amemtukana waziri au mbunge fulani kwa kumwita Kibaka nk.Zinakuwa na zile taarifa muhimu tu za kazi waliyofanya kwenye vikao.
Ikumbukwe pia kuwa Vikao vya kamati za bunge huwa havirushwi Live sababu ni vikao vya kikazi.Na kikao cha bunge ni kikao kikuu cha kikazi sio press conference .Sasa hivi wabunge watafanya kazi barabara kuliko zamani ambapo mara ingine mtu anaomba kuchangia ili tu auze sura kwenye TV aonekane.Wachangiaji unakuta wako msururu wakipigania tu kuonekana!!! Sasa hivi bunge litakuwa na wachangiaji very serious ambao wana hoja za nguvu na si wauza sura kwenye TV
Bunge la Tanzania litakuwa bunge la mfano la kuigwa duniani kwani litatoka na vitu serious vilivyofanyiwa kazi barabara na wabunge serious na habari zitakazotolewa ni zile za HAPA KAZI TU na si zile za mara mbunge kapigwa picha anasinzia bungeni nk
Pia Kazi kuu ya mbunge (Major duty) ni kuleta maendeleo kwenye jimbo lake anakotokea na si kuongeaa sana na kuchonga sana mdomo bungeni na kuanika sura sana kwenye kamera za Televisheni akiwa bungeni.Kuna wabunge majimboni hata kuwaona na kuwakuta ofisini kwao majimboni ni shida.Wao husubiri tu muda ufike wa bunge wachonge midomo na kuuza sura kwenye TV.