Natamani wanaume wote tungeweka mgomo kwenye suala la kuhonga. Imefika wakati wadada wa mjini wamegeuza miili kuwa duka

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,702
36,124
Siku moja wakati natoka lindo nikafika bar moja asubuhi nikapaki Suzuki yangu ili nipate supu. Mara mdada mmoja akaja kunisalimia na kujichekesha. Akaniuliza unanikumbuka nikasema yes. Nikamkaribisha supu akasema ameshiba. Wakati nainuka nikampa cha ten, akasema sasa tutawasiliana vipi. Nikashangaa !!! Nikajiuliza moyoni kwani kuna ulazima kila mtu mnayefahamiana kubadilishana namba. Tumebadilishana namba. Next day mtu ananiomba kodi ya nyumba. Huu ni udangaji wa dhahiri.

Huu ni mfano mmoja tu. Kila siku tunakutana na wadangaji. Mmoja aliniomba hela akanunue iPhone huku mimi simu zangu ni za laki na nusu. Hii hali tumeisababisha sisi wanaume kwa kutanguliza fedha kama ulimbo nao wamezoea. Wanaona ni haki yao kununuliwa simu, kulipiwa kodi ya nyumba, umeme, kununuliwa usafiri n.k

From now onwards nitaichunga senti yangu.
 
Kijana Ni lazima uwe na vipaumbele
1503014402.jpg
 
Mwanaume bahili sio kidume Cha mbegu, Ni masikini
Sasa sisi tunapata wapi fedha ya kututosha na kuwahonga?
Hivi tumewazidi nini kwenye utafutaji?
Naona kama wamekuwa special group.
Kwenye Ile topic ya special group kwenye civics form one tuwaongeze na hawa wahongwaji.
 
Mwanaume bahili sio kidume Cha mbegu, Ni masikini
Ndg yangu, WANAWAKE WENGI HASA WAREMBO WAMEGEUKA KUWA MATAPELI siku hizi. Kila kukicha wanapanga njama namna ya kumchomoa kidume mapesa bila ya yeye demu kuvua pichu. Manake plan yao ni kukutoa ww hela na tena hata puchi asikuvulie. Inaonekana ww ndg yetu tunayekupenda Bujibuji umewezekana hapo. Inabidi tukusaidie JF member mwenzetu. Kwa mwendo huo umeshaangamia.. na kama bado, utaangamia soon na utafilisika kabisaaaaa. Au labda unasapoti tu kwa ajenda binafsi
 
Wewe fala nini, unataka uzikwe na pesa zako....unamjua ginimbi???? Embu acha hizo, wape wanawake ila angalizo kwa kiasi ambacho hakiumizi uchumi wako, akitaka ela ambayo uwezi achana nae, she has a certain class ambayo sio yako, uki afford pambana akupe tunda kwa raha zakee
 
Siku hizi mapenzi ya kweli hakuna. Tusijifanye tunataka wanawake ndiyo wawe na mapenzi ya kweli kana kwamba wanaume wanayo.

Wanaume wengi huwa wanataka kupiga na kusepa tu. Wanawake wengi wameshalijua hilo na wameamua kama mbwai mbwai tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom