MWITONGO MAARIFA
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 276
- 1,428
Wabunge asilimia 90% hawajafanya chochote kwenye majimbo yao akiwemo Ndugai lakini wananchi na Raia Wala hawalalamiki hasa najiuliza Watanzania kwanini wanamshobokea Nassary? Jibu ninalopata ni kwamba huyu mtu ni potential kwa Taifa letu na natabiri one day atakuwa kiongozi mkubwa wa Taifa letu.
Katika umri wake na kipindi chake Meru amefanya mengi na ambayo wengi hawakuyatarajia, amepeleka Maji, ameibua ishu ya ardhi na kufanya utatuzi wa migogoro ambayo CCM wakiongozwa na mkapa walikuwa wanakataa mashamba hayo yasitoke kwa walanguzi.
Amesambaza Maji maeneo ambayo hayakuwa na Maji, ametangaza meru Duniani kote ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za afya....Leo hii meru imekuwa kimbilio la makabila yote na kila mtu anataka kuwaongoza wameru.
Ni Mbunge mahiri toka bungeni na nje ya BUNGE, ni mtu mcha Mungu anayejali Haki, aliweza kuwaumbua DC na genge lake Juu ya rushwa na hivyo kuvitetemesha vyombo vya dola. Kiumbe wa Aina hii lazima atafutiwe visa aondolewe ili wapigaji waendelee kula .....
Ukiona wazee wa mila wanaacha njia na kukimbizwa jua huyu mtu ni kichwa, ukiona mkuu was majeshi ameingia kuliteka Jimbo tambua aliyepo ni mtu mkubwa na hatari kwa chama tawala.
Mzee Sarakikya hajaingia kwenye game hii kimakosa Bali amelazimishwa kujiingiza kuakikisha kwamba Arumeru inaondoka upinzani na kwa miaka yote nadhani amejutia alichokifanya ambacho Ni kushiriki kuiangamiza mila na desturi yake.
Nassary nje ya Chadema au ndani ya Chadema ni kiongozi mzuri na mahiri ambaye watu hasa vijana wanampiga mawe kwa sababu TU ya mafanikio yake.
Nampongeza kijana Kama huyu na natamani ningekuwa na Mbunge Kama yeye. Waliondoka wengi Chadema hawakuvuma Kama Nassary kwa sababu hawakuwa na madhara kwa Taifa letu.
Mwisho nimtake TU Nassary kusimama imara na Bora akawe lecture ulaya kuliko kuwa mtumwa wa siasa za Tanzania zisizozingatia haki....
Sent using Jamii Forums mobile app
Katika umri wake na kipindi chake Meru amefanya mengi na ambayo wengi hawakuyatarajia, amepeleka Maji, ameibua ishu ya ardhi na kufanya utatuzi wa migogoro ambayo CCM wakiongozwa na mkapa walikuwa wanakataa mashamba hayo yasitoke kwa walanguzi.
Amesambaza Maji maeneo ambayo hayakuwa na Maji, ametangaza meru Duniani kote ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za afya....Leo hii meru imekuwa kimbilio la makabila yote na kila mtu anataka kuwaongoza wameru.
Ni Mbunge mahiri toka bungeni na nje ya BUNGE, ni mtu mcha Mungu anayejali Haki, aliweza kuwaumbua DC na genge lake Juu ya rushwa na hivyo kuvitetemesha vyombo vya dola. Kiumbe wa Aina hii lazima atafutiwe visa aondolewe ili wapigaji waendelee kula .....
Ukiona wazee wa mila wanaacha njia na kukimbizwa jua huyu mtu ni kichwa, ukiona mkuu was majeshi ameingia kuliteka Jimbo tambua aliyepo ni mtu mkubwa na hatari kwa chama tawala.
Mzee Sarakikya hajaingia kwenye game hii kimakosa Bali amelazimishwa kujiingiza kuakikisha kwamba Arumeru inaondoka upinzani na kwa miaka yote nadhani amejutia alichokifanya ambacho Ni kushiriki kuiangamiza mila na desturi yake.
Nassary nje ya Chadema au ndani ya Chadema ni kiongozi mzuri na mahiri ambaye watu hasa vijana wanampiga mawe kwa sababu TU ya mafanikio yake.
Nampongeza kijana Kama huyu na natamani ningekuwa na Mbunge Kama yeye. Waliondoka wengi Chadema hawakuvuma Kama Nassary kwa sababu hawakuwa na madhara kwa Taifa letu.
Mwisho nimtake TU Nassary kusimama imara na Bora akawe lecture ulaya kuliko kuwa mtumwa wa siasa za Tanzania zisizozingatia haki....
Sent using Jamii Forums mobile app