Natamani kuwa na mpenzi

Kwanza hongera sana, kwa kuona matatizo yako ya uchokoraa kama fursa na chachu ya kupambana na maisha na kupata elimu. Ushauri wangu ni kukomaa na shule. Ukiwa chuoni na kusettle kidogo tu, utapata mchumba ambae ni msomi mwenzio. Na mtasaidiana masomo pia. Hakikisha mapenzi hayapotezi ndoto yako ya kuwa na digirii.

Kila la kheri mwanangu.
 
mmmmh, nawe jifunze uongo kidoncho. hujui wanawake hatupendi kuambiwa ukweli? khaaa.
 
hongera kwa mafankio uliyofkia. Kwenye swala la mapenz hasa wewe ambae unayakuta ukubwani hivi sidhan (japo sipingi moja kwa moja) kama utampata anaekufaa kwa staili hii ya kutoa namba hapa. Matapeli ni wengi. Kuwa makini.

Asante kwa ushauri,je? Unadhani njia ipi bora ya kufanikisha hili.
 

Nikwambie kitu...! we endelea kwanza kuweka mambo yako sawa, wanawake tupo wengi. wasiwasi wangu unaweza kuishia njiani ukianza hayo mambo unayotaka sasa hivi. Wish you all the best!
 
ndugu pole sana, ila ukae ukijua kuwa wewe SIO MSHAMBA kama unavyofikiria na wala sio kwamba huna bahati wala nini. Nilichokiona kwako ni ujasiri ambao vijana wengi wa rika lako hawana, ni la kuamua kuhangaika na shule na kuachana na mambo ya wadada. Hongera sana! Ninachokushauri ni kukomaa na shule, jenga maisha yako kwanza, hayo mambo ya mapenzi yatakuja automatically ,na wala usiwe desperate kutafuta mpenzi maana unaweza kukwaa maradhi ndugu kwa kuwa ulishajitunza muda wote huo uje kuharibu sasa? NO! Muombe M/Mungu akujaalie mke mwema, na kwa sasa akujaalie ufanikiwe katika masomo yako na malengo yako yote yatatimia Inshaallah!
 
Achana nao mwana kazana na shule hao ukipata kazi nzuri watalundikana uwaoe. Hawana mpango kivileeeeee.
 
Itafute elimu then pesa kwa bidii zote hayo mengine yatajileta yenyewe, utasifiwa mpaka ujiogope mwenyewe
 
Chasaka kwanza hongera sana kwa kuubadili mtazamo wa watu juu ya machokoraa na kuwaonyesha watoto wote ktk hali hiyo kuwa wanaweza.
Pia nakushauri uendelee na mawazo yako ya kuwa msomi na usome zaidi maana ukichanganya mapenzi na hv ww ni mgeni ktk hilo, hakika utapoteza ndoto zako zote.
 
Last edited by a moderator:
Nikwambie kitu...! we endelea kwanza kuweka mambo yako sawa, wanawake tupo wengi. wasiwasi wangu unaweza kuishia njiani ukianza hayo mambo unayotaka sasa hivi. Wish you all the best!

Nikushukuru sana sana,naamini ushauri wako unatoka moyoni
 

Dah! Mungu na akulinde rafiki,ushauri wako umeingia sana akilini,nadhani upweke ulinisumbua hadi nikaweka namba yangu hadharani bila kufiki sana na nimeanza kupokea simu nyingi sana
 

Unahitaji mpenzi kwa ajili ya nn? Sio tamaa ya ngono kweli ndio inakusukuma?
 
nimefurahishwa na uwazi wako.
hongera ila kuwa makini
 

hongera kwa msimamo wako kijana.ila hujajibu swal wa malengo au wa kudo nae?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…