Natamani kumuacha ila nashindwa

Natamani kumuacha ila nashindwa

Hivi wazazi wenzangu kwanini tunapeleka hawa vijana kusoma wasichokijua wala kutilia mkazo kukijua
Mtu upo chuo kikuu lakini hujui kutofautisha Lecture (mhadhara) na Lecturer (Mhadhiri),acha ngono zingatia masomo Huyo binti si mke wako na kamwe hawezi kuwa mkeo maana kama sasa huna uwezo wa kumtunza japo kwa kidogo je utaweza vikubwa hapo baadae?
Meaningful idea
 
Achana naye...huyo atakufanya usifikie malengo? Uko mwaka wa ngapi dogo? Piga shule ujiweke sawa kwanza!! Jiwekee malengo ya kupata GPA ya 5.0 uone kama utapata muda wa kupoteza!!
Mwaka wa pili
 
Hongera, hii ni dalili ya ujauzito, baada ya miezi kadhaa tegemea kupata mtoto tena atakua wa kiume sababu anakuchukia sana.

Ongeza upendo, tumia boom vizuri . kuwa na hekima na ujiandaye kwa malezi.
 
Hivi wazazi wenzangu kwanini tunapeleka hawa vijana kusoma wasichokijua wala kutilia mkazo kukijua
Mtu upo chuo kikuu lakini hujui kutofautisha Lecture (mhadhara) na Lecturer (Mhadhiri),acha ngono zingatia masomo Huyo binti si mke wako na kamwe hawezi kuwa mkeo maana kama sasa huna uwezo wa kumtunza japo kwa kidogo je utaweza vikubwa hapo baadae?
Tatizo sio kumuhudumia mkuu
Utamhudumiaje bila sababu za msingi?
Kwani yeye....au basi tubu.
 
Hivi wazazi wenzangu kwanini tunapeleka hawa vijana kusoma wasichokijua wala kutilia mkazo kukijua
Mtu upo chuo kikuu lakini hujui kutofautisha Lecture (mhadhara) na Lecturer (Mhadhiri),acha ngono zingatia masomo Huyo binti si mke wako na kamwe hawezi kuwa mkeo maana kama sasa huna uwezo wa kumtunza japo kwa kidogo je utaweza vikubwa hapo baadae?
Tafiti zinaonyesha kwamba 90% ya wanavyuo wa siku za sasa wanaconcentrate zaidi kwenye maisha ya mapenzi na ujinga ujina bila kusahau na u-social networking usio na mbele wala nyuma.

wanadhani kuoa na kuolewa ni jambo la kukurupuka, wanadhani watazaa na kuishi humo hostel kwenye maji na umeme wa bure bila kusahau room ya TZS 41,500/4month.
 
Endelea naye mkuu mpaka pale utakapokomaa kiakili, maana seems wewe na yeye wote bado watoto.
 
Tafiti zinaonyesha kwamba 90% ya wanavyuo wa siku za sasa wanaconcentrate zaidi kwenye maisha ya mapenzi na ujinga ujina bila kusahau na u-social networking usio na mbele wala nyuma.

wanadhani kuoa na kuolewa ni jambo la kukurupuka, wanadhani watazaa na kuishi humo hostel kwenye maji na umeme wa bure bila kusahau room ya TZS 41,500/4month.
Sio kweli
 
Af juz tu,ulituambia unasoma ordinary diploma,,,ukawa unaomba notes za adv Mathematics.
Vp diploma kumbe mnachukua bumu as usual?
 
Habari za wakati huu wanaJF,

Naomba niende moja kwa moja, Nimekua kwenye mahusiano na binti mmoja kwa mda wa mwaka 1 na 1/2 sasa.

Nimekumbana na yafuatayo:-
-Sikujua hapendi utani, nikamtania alinichoma kalamu na kwa kua nampenda nikavumilia.

-Wewe ni shetani tu kumbe unajifanya malaika. Pale unaponihitaji tu.

Sababu kaniomba tsh. laki 2 na 1/2 nikamgomea kwasababu hiyo ndo siku tumeingiziwa boom iitoshe na yeye kaingiziwa so sote tulikua na hela hivyo nikawa mgumu kumpa maana hana sababu za msingi.

- Toka mbele ya macho yangu shetani wewe.
Hapo ni baadaye kidogo tulikua tinaelekea COED kufanya UE nikataka kumsaidia begi ndugu yangu aliniaibisha mpaka machozi yalinitoka nikachukulia poa tu.

Baada ya paper nikamfuata tuongee nikamuuliza kulikoni.
Akanijibu kuna mtu alimuudhi hivyo alikua na hasira (hasira za mtu mwingine ziniangukie mimi?) (nikajisemea kimoyomoyo)
Nikajitahidi sana kuropoka nikamwambia siwezi kuendelea naye tena, akajibu poa (kirahisi) (sijui alijuaje nampenda)

Tukaagana vizuri tu mida ya usiku napigiwa simu rafiki yake akidai niende nikamuone (mpenzi wangu) coz muda wote analia tu.

Nikashindwa kujizuia nikaenda ndugu yangu"! Macho ya mtoto kike yalibadilika rangi nakuambia basi sijui ilikuaje nikamhug na kumsamehe kabisa.

Baada ya hapo ameendelea na tabia zake mara shetani mara toka mbele ya macho yangu mara my kuna lecture ananitongoza mambo mengi.

Kila nikitaka kumuacha naumia sana na sijui kwanini inanitokea hivi.

Ushauri wako ni wa maana sana, naomba matusi yasiwepo.
Nikitazama mbele kidogo..!
Naona kuna mmoja atakuja kuumizwa sana baadae kuliko ilivyo sasa hivi.
Na wewe ndio upo kwenye hatari kubwa.
 
Pole sana mkuu.....
Jaribu kumsahau kila kitu kinawezekana ni maamuzi tu binafsi.
Haijalishi ataumia kiasi gani ? Au wewe utaumia kiasi gani ?
pia ameshajua udhaifu wako kwamba huna msimamo kwa jambo ulisemalo, kama umesema utamuacha wewe muache kweli fanya mambo yako, ukimsamehe kila mara anajua udhaifu wako.

Kila kitu kinawezekana jaribu kufanya maamuzi sahihi bila kuyumbishwa na huyu mwanamke.

Ukizingatia wewe ni mwanaume na baba bora wa kesho, kuwa na maamuzi sahihi katika kila jambo ufanyalo
Waza mambo ya msingi na punguza mapenzi.
 
Back
Top Bottom