Natamani kujua maisha ya marehemu Al Habib Alhaji Aziz Massanga (Zingizi)

Zee la unga unataka nimueleze kivipi?

Nijaribu kumueleza km wenzangu?

Muuza madawa ya kulevya utamuelezeaje?
Binafsi nilikuwa simjui ila mitandao ilinifanya nijiulize nilisearch kama mwanzisha uzi ila hola....
Ilibaki kidogo tu nianzishe Uzi

Ila Katika mambo sikuyafikiria ni watu wenye roho ya aina yako ambao wameegemea uvivu na kuacha kushughulika na maovu yao na kushughulika na maouvu ya watu

inawezekana hapo ulipo una kesi mbalimbali hatuzijui unashughulika na dhambi za Zingizi ambaye kwa watu wanamuombea Pepo. sijui watu unaoishi nao huko wanakuombea nini ingawa unaonekana mkereketwa
jiandae Kiongozi usihangaike na mwenzio keshafanya yake we tengeneza njia yako ya sasa na baadae

Kuna kasumba mbaya sana inayofanywa na watu wabaya wachache kwa kuwasema matajiri wengi vibaya wakishakufa jamii inayobaki inakazana na kubaki na maovu tu, ila juhudi za kazi hawataki kusema alifanya biashara usiku na mchana hawataki kusema, alisafiri alikaa bila kulala hawataki, aliajiri watu na kuwaongoza hawasemi, utasikia tu aliuza unga aliabudu shetani
wanasahu hata wenyewe wanafanya matendo hayohayo mengine mabaya na huku hata maskini hawawakumbuki

Kama kazi ya vipodozi isingempa utajiri kila mwanamnchi angefanya biashara ya vipodozi kama ni rahisi,ni strategy za soko ndo zinazotofautisha biashara moja na nyingine, inawezekana na wewe una duka lako la vipodozi hapo hujatoka ndo maana unaona wenzio Monsterz.

Hata darasani hamkuwa wa kwanza wote lazima kuna walioshika namba sababu ya namna yakufikiri kwa jinsi walivyoweza kujipanga.

Hata zama hizi za sasa ingawa hali ni ngumu kuna watu hawalali wanaumia wanafanya kazi, wanafanya projects, wanafanya biashara ndogo na kubwa,wanapitia shida za kodi,wanatapeliwa,hawakati tamaa, tena biashara wanaifanya kwa upendo kutoka moyoni kuisaidia jamii, halafu siku wakiondoka hapa duniani wanajitokeza watu wanaongea tu kirahisi wanavyojisikia juu ya maisha ya wenzao walioishi hapa duniani.

Mungu akusamehe tu Brother pengine ni roho ya wivu sababu bado hujawin.........

Toba haikuwekwa kwa maksudi yakufanya dhambi ila ni kwa mwenye hekima na uadilifu kutambua lililojema nakubadilika tungekuwa wema sana tungekaa peponi...kungekuwa hamna haja yakupita duniani sababu wote ni malaika.
 
mrangi ni kichwa hasa huwa namkubali sana, kungekuwa na mapendekezo ya kuingiza watu kwenye idara fulani huyu angefaa maana Dar anaijua in and out pia na watu maarufu, majambazi, matapeli, wauza ngada na matajiri wote anawajua na hustle zao...

Ingawa naona hapa kwa huyu jamaa umeamua kuficha baadhi ya mambo, haiingii akilini mtu atoke kuuza mgahawa aibuke kuwa tajiri ghafla. Kwa namna yoyote huyu bwana alijihusisha na madawa ya kulevya au biashara nyingine iliyompa ukwasi kwa ghafla hivyo...

Huyu jamaa ni very potential maana taarifa nyingi nyeti anazo...

Salute popote ulipo...
Waislam hawaachi kumtetea

Hata kama alifanya Haram na Dhulma ilimradi kasaidia waislam na kujenga Masjid bas roho zao kwatu.

Na watasema peponi ameenda huyo

UNAFIKI MBAYA SANA



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu alikuwa anafanya biashara ya vipodoz
Na wakina sauli s.h amon
Walianza kitambo Sana.... Vipodoz vilikuwa vina ingiza Hela sana
Huyu jamaa Kuna wakati alitupaga connection ya kufata maziwa super milk toka Zimbabwe na kuyaleta Tanzania kuuza...... Nakumbuka hadi mtaji alitu boost wakati huo Zimbabwe oya oya

Ova
Hivi S.H AMON mpaka mikoani ni za Sauli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
story za marehemu zingizi kuwa mtoaji na kipenzi cha watu wa kariakoo huku chanzo cha mafanikio yake kikihusishwa na biashara ya dawa za kulevya, nazifananisha na story za christopher michael coke aka dudus, ambaye alikuwa drug dealer mkubwa sana nchini jamaica miaka kadhaa iliyopita.

biashara ya unga ilimfanya dudus kuwa tajiri na mtu mweye authority kubwa nchini kwake. alitumia sehemu ya utajiri wake kusaidia watu masikini wa mji aliokuwa anaishi. lakini hii yote ilikuwa ni kutafuta protection.

mwisho wa siku alitengeneza kundi la watu ambalo lilikuwa loyal kwake kwa kila kitu.watu hawa ndio walitumika kuleta upinzani mkubwa sambamba na kuziba njia siku askari wa marekani walipoenda kumkamata.

kwa sasa yupo gerezani akitumikia kifungo cha miaka 23 baada ya kukiri makosa aliyotuhumiwa.

moral of the story : usihadaike na baadhi ya watu waliofanikiwa kimaisha huku wakitumia sehemu ya mafanikio yao kusaidia watu wengine.

drug dealers ni watu makini sana.
kila wanachokifanya, hukifanya kwa malengo.
ikiwemo kutafuta kivuli cha kuficha uovu wao. au kuandaa kundi la watu masikini watakaowatetea kufa na kupona siku ambayo mamlaka itaamua kuwadhibiti.

christopher michael coke aka dudus.
08-56-59-images.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom