natamani bunge la tz.....lingeendeshwa kingereza

Sijui ni ushamba , sijui ni ulimbukeni , sijui ndiyo ukoloni bado upo mpaka vichwani kwetu!. Mimi nashangaa sana mtu anapofikiri kujua kiingereza sijui ndiyo elimu ? . Hii kasumba inatusumbua sana, kama kiswahili tu watu kinawagonga unategemea mtu atakuwa na miujiza kuongea lugha ambayo siyo yake na haitumii mara kwa mara?. Mimi nafikiri kasumba hii inatutafuna na ndiyo inatufanya tusiendelee, hata wataalamu wetu huenda tunawalalamikia kuwa wamesaini mikataba mibaya, si wanajifanya wanajua kiingereza kumbe hawahjui wanaishia kusaini tu. Ukweli ni kwamba ni matatizo wa kuwatawaliwa na wakoloni, kwani hao wabunge walioongea kiingereza leo wanazidiwa kiingereza na Fabio Capelo -kocha wa Uingereza ? mbona waingereza tena ndiyo wenye lugha hawasemi hivyo na wala hata yeye haoni aibu. Mimi sijawahi sikia Marcio Maximo akichekwa kwa kiingereza chake kibaya, tena ni kibaya kuliko watanzania wengi wanavyooongea.

Tuache kiingereza kiwe lugha kama lugha zingine Kifaransa, kireno, kimatumbi n.k , hiyo sifa ya kiingereza kama ina maana hivyo je ni miongoni mwa sifa za kuwa Mbunge? kama siyo sifa kwanini sasa. Hiyo ni kutishana tu kunakotumiwa na wajanja wachache tena wasio na uwezo.

Nimesema kwamba kiswahili chenyewe ni shida kwa watu wengi mbona hatuchekani, mbona mzee wa kiraracha hawezi kutamka Nchi anasema NJI mbona hakuna anayemcheka au kwa sababu ni kiswahili?

Huyo Capello na Maurinho wanatoka mataifa makubwa na yanayojitosheleza sana hasa kimaendeleo. Hivyo wana lugha zao.Na hata akienda uingereza akaongea kwa kuunga unga bado wanamuadmire sana kwa sababu at least yeye ni multilingual kuliko waingereza wengi ambao ni bilingual?

Kuna debate kubwa uingereza kwa wao kutokuwa na uwezo wa kuongea lugha zingine while everybody in the world can speak a bit of english.

Sasa tukirudi kwenye point, demand ya sisi watanzania ni kujua kiingereza. Kwetu hii language ni very strategic kwa sababu tunazungukwa na mataifa karibu yote ambayo yana very good command ya english (except a few). Sasa hii inatupa challenge sana kupata kazi ambazo ni open pia kwa majirani zetu.

Mkikutana na mkenya au mganda na the same qualifications au hata kama umemzidi lakini akaweza kuwaimpress potential employers kwa lugha ya kiingereza basi ni likely watapata hiyo kazi kuliko wewe unayehangaika kuelezea point kisa lugha inakugonga.

Hata akija muitaliano au mjerumani muwekezaji japo hajui vizuri kiIngereza lakini ataprefer mfanyakazi anayejua kiingereza kuliko ambae hajui.
Sasa wakati huu tunapofungua mipaka kiingereza ni very strategic language than any other time in the history of Tanzania.
 
Sijui ni ushamba , sijui ni ulimbukeni , sijui ndiyo ukoloni bado upo mpaka vichwani kwetu!. Mimi nashangaa sana mtu anapofikiri kujua kiingereza sijui ndiyo elimu ? . Hii kasumba inatusumbua sana, kama kiswahili tu watu kinawagonga unategemea mtu atakuwa na miujiza kuongea lugha ambayo siyo yake na haitumii mara kwa mara?. Mimi nafikiri kasumba hii inatutafuna na ndiyo inatufanya tusiendelee, hata wataalamu wetu huenda tunawalalamikia kuwa wamesaini mikataba mibaya, si wanajifanya wanajua kiingereza kumbe hawahjui wanaishia kusaini tu. Ukweli ni kwamba ni matatizo wa kuwatawaliwa na wakoloni, kwani hao wabunge walioongea kiingereza leo wanazidiwa kiingereza na Fabio Capelo -kocha wa Uingereza ? mbona waingereza tena ndiyo wenye lugha hawasemi hivyo na wala hata yeye haoni aibu. Mimi sijawahi sikia Marcio Maximo akichekwa kwa kiingereza chake kibaya, tena ni kibaya kuliko watanzania wengi wanavyooongea.

Tuache kiingereza kiwe lugha kama lugha zingine Kifaransa, kireno, kimatumbi n.k , hiyo sifa ya kiingereza kama ina maana hivyo je ni miongoni mwa sifa za kuwa Mbunge? kama siyo sifa kwanini sasa. Hiyo ni kutishana tu kunakotumiwa na wajanja wachache tena wasio na uwezo.

Nimesema kwamba kiswahili chenyewe ni shida kwa watu wengi mbona hatuchekani, mbona mzee wa kiraracha hawezi kutamka Nchi anasema NJI mbona hakuna anayemcheka au kwa sababu ni kiswahili?

Kua na akili nzuri na kutokua na kasumba ni pamoja na kujijua mwenyewe matatizo yako na namna ya kuyatatua.

Kama unategemea nchi nyingine ili uishi bora na lugha yake ukaiongea vizuri, hii ni kwa faida yako mwenyewe ili uheshimike. Tz hatujitegemei kwa chochote hivyo bora na lugha za hao maboss wetu kama tunajifunza basi na tukajifunza kuongea vizuri kuonyesha uwajibikaji na unyenyekevu wetu la sivyo tunaonyesha kwao kutoweza chochote. Hata wachina walifanya hivyo walivyokua wanategemea Urusi, na sasa Kiingereza. Hata kondaKta wa daladala ama mpiga debe anajifunza na kuongekea Kiingereza kizuri si cha Uingereza bali cha nchi wanayoitegemea kwa tech na elimu - US. Hata majina ya majengo mapya yana majina yanayonakiliwa toka US.

Kiswahili kiendelezwe pia lakini je tunaweza kuwekeza kwenye Kiswahili wakati ufisadi umetubana, na huyo mtu mhimu asemaye Nji badala ya Nchi lazima akosolewe na ajirekebishe. Kama tulio jirani yake hatumkosoi basi ni picha halisi ya uzembe wetu ulivyokithiri ama tusivyooambilika - tunachukulia kila kitu kama ni comedy. Uzembe unaanzia kwa mambo madogo madogo kama hayo.

Hao makocha wa mpira wasiojua kiingereza uliowasema ni watu wamefikia uwezo wa juu katika yale wayafanyayo, utagundua kua wote wana soko wakati TZ kama Nchi wala hatuna soko.
 
in SHORT after colonial era, we dont ve a proper education system,under ccm each minister for education has the mandate of introducing the wrong ideas on the system.now the plan for form 4 as universal education will be worse!
 
nimeona jinsi wabunge walivyokuwa wanapata shida kujieleza walipokuwa wanagomembea uwakilishi wa SADEC nimecheka kupita kiasi kwa watu walikuwa wanatumia nguvu kupita kiasi ili waweze jielezea..........
Walishindwa kabisa kusema nini watakachokifanyia tz huko sadec zaidi watu wanataja tuu vyeti vyao feki.....embu jaribu kuicheki kwenye youtube hii hapa, Wagombea wa uwakilishi SADC
du ingekuwa hivi labla,
senk yu mrs spika, iam the mbunge from njombe representing my people, i say thank you my people for electing me your mbunge, i am going to do and do good job for you.bla bla bla
 
du ingekuwa hivi labla,
senk yu mrs spika, iam the mbunge from njombe representing my people, i say thank you my people for electing me your mbunge, i am going to do and do good job for you.bla bla bla

Nzuri Kipipili
 
nimeona jinsi wabunge walivyokuwa wanapata shida kujieleza walipokuwa wanagomembea uwakilishi wa SADEC nimecheka kupita kiasi kwa watu walikuwa wanatumia nguvu kupita kiasi ili waweze jielezea..........
Walishindwa kabisa kusema nini watakachokifanyia tz huko sadec zaidi watu wanataja tuu vyeti vyao feki.....embu jaribu kuicheki kwenye youtube hii hapa, Wagombea wa uwakilishi SADC

Naamini kuwa ingekuwa ni English wengi wao wasingethubutu kugombea Ubunge
 
du ingekuwa hivi labla,
senk yu mrs spika, iam the mbunge from njombe representing my people, i say thank you my people for electing me your mbunge, i am going to do and do good job for you.bla bla bla

Fo wananchi of njombe hu electing mi, Ai emu going to livenji by buildingi so many gesti housi in our njombe discreet so next time we get so many gesti as you know mrs spika, me and you we are coming from the same legion completili and we are all unmarried.
 
SADC hawana mainterpreters, ndiyo maana ilimlazimu mh. Spika kuwaeleza wagombea wajieleze kwa kimombo, ambayo ndiyo lugha itakayotumika. Hivyo kujua kiingereza ni lazima na iwe moja ya vigezo vya qualification. Mbunge anatakiwa kujenga hoja kwa kuelezea kiufasaha. Kama itakuwa shida, CHADEMA wana wabunge wasomi kibao ambao hawajachakachua vyeti vyao. Wapo akina Lissu, Zitto, Kahigi, Mtema, Mnyika. Hawa jamaa hata IQ zao hakuna mtu ataquestion. Vilevile kama nilimwelewa mtoa mada, anasema na bunge letu liendeshwe kwa kimombo pale Dom, hiyo itakuwa ngumu kutokana na wabunge wengind wa CCM kuwa na elimu ya ngumbaru. Mfano Jah People, Maji Marefu, Airo, Lusinde nk.
Ukiomba kazi kwenye mashirika ya kimataifa au ya kikanda kama Sekretariati ya SADC, African Development Bank, COMESA, hata sekretariat ya EAC, unaambiwa sharti uwe unamudu vizuri Kiingereza na itakuwa sifa ya ziada kama unamudu Kifaransa, Kireno na Kiarabu. Sijaona mahali ambapo wanataka Kiswahili. Kwenye mashirika ya Umoja wa Mataifa ndiyo usiseme. Kwa hiyo mimi naona watanzania tusiwe "inward looking" sana. Lazima tujitahidi kuzijua lugha muhimu duniani pamoja na kukienzi Kiswahili chetu. Vinginevyo fursa nyingi zitatupita. Hatuwezi kushindana kwenye masoko ya ajira hata katika biashara nje ya nchi. Kupuuza Kiingreza (na lugha zingine) ni kuwa "defensive". Wale wanaozijua wako "offensive". Ndiyo sababu kuna Watanzania wachache wanaofanya kazi Kenya huku Wakenya wakiwa wamejazana kwetu.
 
Nacheka kupita maelezo. Jamani lets be realistic kufahamu kiingereza inabuild some sort of confidence kwa mtu sasa angalia hawa watu halafu kesho mnawatuma wakasign mikataba matokeo yake kudanganywa na kudanganyika. Foundation matters bana(primary to High school education background). Nimeshuhudia watu wengi wenye degree selasini na uchee hizo za malkia lakini when it comes kujiexpress themselves unajiuliza hizi degree walipatia wapi??
 
Back
Top Bottom