Nataka kuzaa watoto si chini ya 10

Nataka kuzaa watoto si chini ya 10

Super Sub Steve

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2011
Posts
17,689
Reaction score
11,276
Mi na mke wangu tulikubaliana tuwe na watoto wawili. Na tayari tumeshabarikiwa kupata hao kwa kadiri ya makubaliano ndo mwisho wa kuzaa. Lakini kila nikiwaangalia watoto wangu wawili napata shauku ya kuongeza wengine.

Watoto wangu nawapenda watoto wangu wapo vizuri kiasi kwamba napata faraja kuwa nao. Kama ningekuwa nao kumi hivi nadhani ningekuwa na furaha zaidi. Sasa kwa vile mke wangu hataki tena kuzaa nimekata shauri la kutimiza ndoto yangu ya kuwa na watoto kumi (bado nane)

Nakaribisha mdada yeyote ambaye anapenda kuwa na mtoto au watoto tufanye makubaliano ili niweze kufanikisha lengo langu. Dini au kabila sio kigezo sana. Ili mradi tu uwe na uwezo wa kuzaa.

Nafasi zipo wazi.
 
Aii unafikiri kuzaa hovyo na wanawake tofauti ni sifa?raha ya watoto uzae na mama mmoja, mlee watoto wenu pamoja kwa upendo na uwe na uwezo wa kuwalea, kama mlikubaliana kuzaa wawili na unajisikia kuongeza talk to your wife atakuelewa hata kama it will take time, acha kumkaribisha shetani kwenye ndoa yako ndugu!
 
nenda mitaa ya kariakoo pale nilisikia kuna duka wanauza incubators
 
Badala ya kuwaza hao ulionao watasomaje unawaza kuongeza wengine.

Idiot.
 
Unazaa watoto 10 una uhakika wa kuwatunza? Una uhakika wa kuishi miaka mingi kuhakikisha wanapata huduma stahiki mpaka watakapokua watu wazima wa kujitegemea???

Nahisi umekurupuka dogo, maisha ya sasa ni magumu sana, usitegemee leo una afya Unafanya kazi na kesho pia utakuwa hivyo!

Fikiria upya kabla ya kufanya hayo unayotaka kufanya#
 
Naungana na madaktari kwamba kila pafu moja la bangi linakaa kichwani miaka saba.... Mkuu nadhani umepitiliza mapafu ya bangi kuzidi umri wako wa kuishi, kwa mbali nakuona mitaa ya MIREMBE Dodoma
 
ulio nao wana umri gani? kabla ya kupata vidada, jiangalie kipato chako, watoto sio mchezo, sio mnaleta watoto kumi alafu mnawavalisha nguo za mtoto wa dada
 
Zaa tu ila kila 9 Dec tutahitaji hiyo team ikafanye usafi tutakapo ipangia.
 
Utaweza kuwa unaongea nao wote?

Watoto watakua utasema tu heh mwanangu kakua wakati hujachangia chochote kwenye ukuaji zaidi ya chakula na mavazi.

Hata shule hutoweza kuwapeleka shule za kueleweka.
 
Back
Top Bottom