M45
JF-Expert Member
- Aug 20, 2015
- 1,461
- 2,321
- Thread starter
- #101
umejuaje wanafanya yote hayo? ni kwa sababu unawafatilia au umeachia wakuendeshee maisha yako. Hawa watu wabinafsi, wasengenyaji na wachoraji wako kila kona. Hata humu wamo. Ndo hulka ya mwanadamu. Unachotakiwa ni kuanzisha mahusiano na nafsi yako. Ujijue wewe ni nani, ujipandishe thamani yako mbele ya macho yako na uwe accountable kwa Muumba wako tu. Unapofanya kitu lenga kujifurahisha wewe mwenyewe na uangalie kama kinamfurahisha Muumba wako. Ukikosea mahali kama ilivyo hulka ya mwanadamu, fanya toba kwa Mungu ' kisha jisamehe na ukubali matokeo ya kosa lako kisha songa mbele.
Kamwe usilenge kuwapendeza binadamu maana hawana asili ya wema. Hata uwe umefanikiwa kiuchumi kama Dangote watakusengenya na kukuchora, hata uwe umefanikiwa kiroho kama Hinnie watakuchora tu.
Cha msingi ni kutokuwaza watu wanasema nini juu yako, na hata ukijua wanasema nini juu yako kama utakuwa umeshatengeneza amani na nafsi yako maoni ya watu hayawezi kukuumiza. Kwa hiyo anza kufanyia kazi imani yako juu yako mwenyewe. Anza kujiamini na kujikubali. Ukijiamini na kujikubali utaanza kuhisi watu wanakuona kama unavyojiona wewe. Kama unajiona mtu mzuri hilo ndo la msingi. Kama unajiona una mapungufu na unahangaika kuyaondoa ili watu wakuone huna mapungufu lazima ujione mpweke maana hutaweza ku-dictate jinsi unataka watu wakuone au kukunenea. Ukijitambua, ukajikubali na kujiamini hata kama watu watasema tofauti na unavyojiona, wewe haitakusumbua kwa sababu utakuwa unajiambia "wanasema hivi kwa sababu hawanifahamu. Mimi ndiye ninayejifahamu na Muumba ndo anayenifahamu na kunielewa zaidi". Baaas, unaendelea na maisha yako.
Nakiri katika shauri zote katika huu uzi hii ni zaidi ya shauri.
endelea na moyo huo huo mkuu.