Nataka Kumuona Mwanangu!

Nataka Kumuona Mwanangu!

Na ikawaje ukaachana na Huyo dada?

Hapa kwa huyu dada naomba niongee na wanaume wenzangu:

Kweli kweli nawasihi, kama umempa mimba binti na huna mpango naye basi usimuingilie kwenye mahusiano yake mapya. Hili nimeliona sana kwa wakaka wengi wa kibongo. Yani basi tu alimradi binti wa watu asiwe na amani na asianzishe mahusiano mapya.

Dah sijui nilielezeeje hili zaidi. Lakini inauma sana.
 
Mentor 1998 form one? Sasa inabidi niwe mwangalifu humu, kumbe mimi naweza kuwa kwenye list ya vizee humu pamoja na mpenzi wangu FaizaFoxy
 
Mahusiano yana milima na mabonde yake,,
Ila maumivu yake ni makali sana,,,kupona kwake kunahitaji 'muda.'.pole mkuu kama yalikukuta kweli.
Kila mtu akieka kisa chake cha mapenzi unaeza ukajiona wewe una afadhali loo!
 
Pole sana dokta, mapenzi yana changamoto nyingi sana aiseee, kuna nyakati za kufurahia, kuna nyakati za kuumiza kiasi kwamba unatamani ufe,ila all in all twatakiwa kupambana nazo na kusonga mbele ili maisha yaende, ila binadamu tuna roho mbaya sana aiseee
 
Tumalizie tupate kujifunza zaidi.
Tuambie walau kwa muhtasari jamn..

Yaan wazazi wako kama nawaona hasahasa mama aliekukanya tangu mwanzoni.
Nataman kujua hatma ya huyo bibie na huyo Kijana wake Wa chuo.
 
Mentor Tanga school ulikaa bweni gani?, mimi nilikua Twiga jirani na mabweni ya mbuni
 
Daaaaaa pole sana sana mkuu nikweli au nihadithi maana mmg
 
Kiukweli mahusiano yana changamoto nyingi sana Pole sana nimefurahi tu hayo maeneo uliyoyataja Tanga, Niliposikia Raskazone hadi mwili ukanisisimka aisee Nimepamic Tanga kwakweli,Chumvini,Mwamboni, makorora, kwaMinchi, Sahare, Donge, barabara ya1_20, nguzo8, mwambani beach,Kisosora, nguvumali, Kange,M/mapana, bila kuisahau club LAKASACHIKA
 
Waliona walivyokuwa wakipendana
Wakawakubalia kuwa pamoja mwishoni
Wakafunga ndoa kubwa
Ilikuwa nderemo na vifijo, vibwebwe na vigoma
Wakapata watoto
Na wakaishi kwa furaha maisha yao yote.​
Ilikuwa ndoto yangu. Ndoto ya miaka mingi ijayo........
[/SIZE][/I][/B]

Pole sanaa bro,
Stori yako inasikitisha sanaaa! sio kwako tuu bali kwa Mwanaume yeyote aliyejitoa kwa dhati dhidi ya mpenzi/mke mtarajiwa.

Tutajifunza mengi kama utakaza moyo na kutumalizia ilivyoishia bro.
 
Umesubmit hili andiko saa kumi na nusu alfajiri. Kwa maana hiyo ulikuwa uliandika usiku wa manane. Pole sana mkuu.

Maisha ni kusonga mbele. Lakini nimegundua wazazi huwa wana vitu wanaviona, ambavyo kwa wakati ule, moyo wa mtu huwa umefukiwa kwenye mapenzi kiasi kwamba hujali wanachokisema.

Kwa wale ambao bado hawajaoa, mzazi akikwambia usiomwoe yule binti au usiolewe na yule kijana, usifanye haraka kuoa. Uache wakati useme. Na mara nyingi Mungu huutoa ukweli ili wewe uamue cha kufanya.
 
Back
Top Bottom