Nataka kumuacha japo ninampenda sana

Nataka kumuacha japo ninampenda sana

mambo ya nyakati

Senior Member
Joined
Aug 24, 2022
Posts
115
Reaction score
149
Habari wakuu,

Naombeni kunisaidia njia ya kumuacha mwanamke unayempenda sana, yaani ukikaa dk 5 lazima umuwaze. Nahitaji kumuacha kwasababu zangu binafsi, ingawa ananipenda sana na mimi nampenda sana kutoka kwenye moyo wangu.

Cha kwanza amenizidi umri miaka 9, cha pili ana mtoto, cha tatu kashaachana na wanaume sita ambao mimi nimewashuhudia na bado sijui huko nyuma. Kwa jinsi ninavyompenda naelekea kuwa chizi kabisa, ameniteka ufahamu wangu na moyo ila nataka nimuache.

Je, nitumie mbinu gani?

Asanteni.
 
Kwann umuache na unampenda kwani mtoto anaazuia kitugani kwenye mahusiano yenu
Nowdays kupendwa ni bahat sana na kumpata mtu mkaelewana ni habari nyingine
Hao wanaume sita wakat mpo pamoja au before??
Kabla hata ya kujuana
 
Single maza kwani Wana tatizo gani??
Wana matatizo mengi tu, cha kwanza wanafanya malengo na watoto wao yani wanaingia kwenye mahusiano kwaajili ya kutatua matatizo yake ya kiuchumi yeye na mtoto wake.

Kwa kifupi single mother %99 wanaingia kwenye mapenzi kwaajili ya kupata pesa za kulea mwanae tu yaani hawaangalii jambo jingine zaidi ya kutaka kupewa pesa tu ya kumlea mwanae.
 
Wana matatizo mengi tu, cha kwanza wanafanya malengo na watoto wao yani wanaingia kwenye mahusiano kwaajili ya kutatua matatizo yake ya kiuchumi yeye na mtoto wake, kwa kifupi single mother %99 wanaingia kwenye mapenzi kwaajir ya kupata pesa za kulea mwanae tu yaani hawaangalii jambo jingine zaidi ya kutaka kupewa pesa tu ya kumlea mwanae.
Kumbe lkn ni mtazamo sidhani km ni uhalisia
 
Back
Top Bottom