NATAKA kuingia Bongo movie ila Pakupitia sipaoni.

NATAKA kuingia Bongo movie ila Pakupitia sipaoni.

Joined
Apr 24, 2015
Posts
98
Reaction score
74
Mimi hapa nina kipaji cha kuandika Story zenye kiburudisha na kufundisha pia
Natamani kuingia Bongo Movie ili nifanye Mapinduzi makubwa na Kuikuza zaidi Tasnia hii na kuifanya ifikie level za juu zaidi lakini nashindwa na kosa pia namna ya kuingia kwani mala kadhaa nmefanya Mawasiliano na Wasanii kadhaa lakini bila mafanikio. Naombeni ushauri nifanyeje ili kuingia Bongo movie jamani.

Kipaji changu chemichemi hakiwezi kukauka.
 
Mtafute Msami atakusaidia....

Au anza kwa kujitolea ufanye kazi na wasanii wachanga na baadhi ya wenye majina makubwa, kuanzia hapo kama kazi zako ni nzuri utatafutwa tu.

Unamkumbuka mzee Kipara wa Kaole ya wakati huo??
Alijitoa sana yule mzee kwa hawa vijana wanaotamba kwa sasa kwenye tasnia, na kwa kujitoa kwake akajijengea heshima.

Na wewe jitoe kwanza.
 
Mkuu Wenzako walioko ndani wanatafuta pakutokea hawapaon, ww unatafuta pakuingilia, wanajaribu kule na huku lkn Bado, bongo movie Enzi hizo ila jaribu Kila mtu na bahati yake
 
Daaa mi mwenyewe sijui pa kuingilia sijui nikushauri nini?
 
Mimi hapa nina kipaji cha kuandika Story zenye kiburudisha na kufundisha pia
Natamani kuingia Bongo Movie ili nifanye Mapinduzi makubwa na Kuikuza zaidi Tasnia hii na kuifanya ifikie level za juu zaidi lakini nashindwa na kosa pia namna ya kuingia kwani mala kadhaa nmefanya Mawasiliano na Wasanii kadhaa lakini bila mafanikio. Naombeni ushauri nifanyeje ili kuingia Bongo movie jamani.

Kipaji changu chemichemi hakiwezi kukauka.
Kwa uandishi huo?...utaipeleka vipi level za juu bongo movie wakati huonyeshi hata userious?
 
eliakim xavery,

Unajua kuandika story au unajua kuandika script/screenplay?!

Kwenye filamu huandiki story bali unaandika script ambayo format yake ni 100% tofauti na story ya kawaida/novel. I know, wapo wanaoanza kwa kuandika story kisha ndo wanaandika script lakini kabla hujaota kufanya mapinduzi kwenye tasnia ya filamu unatakiwa kwanza kujifunza kuandika script!

Je, umeshawahi kuandika script au unafahamu jinsi ya kuandika script?

Kama unaweza kuandika stori unaweza kupata urahisi kidogo kuandika script kwa sababu, jambo la msingi utakalojifunza ni screenplay format na "miiko" yake... na hili muhimu sana!!

Kama hujawahi kuandika script; uliza swali lolote kuhusu hilo!!!
 
eliakim xavery,

Unajua kuandika story au unajua kuandika script/screenplay?!

Kwenye filamu huandiki story bali unaandika script ambayo format yake ni 100% tofauti na story ya kawaida/novel. I know, wapo wanaoanza kwa kuandika story kisha ndo wanaandika script lakini kabla hujaota kufanya mapinduzi kwenye tasnia ya filamu unatakiwa kwanza kujifunza kuandika script!

Je, umeshawahi kuandika script au unafahamu jinsi ya kuandika script?

Kama unaweza kuandika stori unaweza kupata urahisi kidogo kuandika script kwa sababu, jambo la msingi utakalojifunza ni screenplay format na "miiko" yake... na hili muhimu sana!!

Kama hujawahi kuandika script; uliza swali lolote kuhusu hilo!!!
Ahsante sana Mkuu, mim naandika story bado sjapata ujuzi wa kuandika Script.
kama Unauzoefu mkuu waweza ukanisaidia apo.
 
Ahsante sana Mkuu, mim naandika story bado sjapata ujuzi wa kuandika Script.
kama Unauzoefu mkuu waweza ukanisaidia apo.
Hebu kwanza weka hapa page moja ya stori yako yoyote hata kama utaiandika fasta hivi sasa! Hapo itasaidia kukuonesha tofauti ya kwanza kabisa kati ya stori na film script!

NOTE: Unapoandika script LAZIMA utumie screenwriting software ili uweze kufikia standard yake!! Nadhani zipo FREE software.
 
Mimi hapa nina kipaji cha kuandika Story zenye kiburudisha na kufundisha pia
Natamani kuingia Bongo Movie ili nifanye Mapinduzi makubwa na Kuikuza zaidi Tasnia hii na kuifanya ifikie level za juu zaidi lakini nashindwa na kosa pia namna ya kuingia kwani mala kadhaa nmefanya Mawasiliano na Wasanii kadhaa lakini bila mafanikio. Naombeni ushauri nifanyeje ili kuingia Bongo movie jamani.

Kipaji changu chemichemi hakiwezi kukauka.
embu igiza igizo lolote halafu tuma ki video humu ili tuone kama kweli unakipaji au mbabaishaji kama wababaishaji wengine wa bongo muvi


Maana tusije tukakutafutia chaneli kumbe na wewe huna kipaji bali ni mtafuta kiki kama harmorapa
 
embu igiza igizo lolote halafu tuma ki video humu ili tuone kama kweli unakipaji au mbabaishaji kama wababaishaji wengine wa bongo muvi


Maana tusije tukakutafutia chaneli kumbe na wewe huna kipaji bali ni mtafuta kiki kama harmorapa
Ah! Ye amesema ni mwandishi bhana... sasa mwandishi na kuigiza wapi na wapi?!
 
basi atunge stori yoyote na airushe humu jf aone muitikio wa watu ukoje na sio kukurupuka tu kisa maisha yamempiga ngwala
Story fupi kwa haraka
Katika kijiji cha Inama Inuka kulikuwa na Jama mmoja Jina lake Ndole, Jamaa Huyu alikuwa katili sana, Kwani Alikuwa anawatesa watu bila Huruma watu wasio na Hatia yoyote, Jamaa Ukimsalimia anakutusi Usipomsalimia anakupiga, (dawa yake ilikuwa ukimuona unamuepka) Mtu huyu alikuwa na Mtoto mmoja mdogo, na Mama mtoto huyo alikuwa alishaondoka kwa sababu ya Ukatili wa huyu jamaa ((nakumbuka alikuwa anakuja kwetu na kumchukua dada yetu ili akacheze na mwanaye Bila hata ridhaa ya Baba yetu)), Huyu jamaa alikuwa anaishi karibu na Barabara Ambapo walikuwa wanapita watu wengi Wengi wao walikuwa wakielekea Nchi jirani Ambapo walipokuwa wanafika pale wamechoka hivo ilikuwa inawalazim kuomba Huduma kadhaa kama Chakula,Maji,
Jamaa ukiomba Maji ya Kunywa alikuwa Anakuletea Ndoo ya Lita20 usipoyamaliza jamaa alikuwa Anakukata Kichwa, watu wengi aliwauwa kwa njia hiyo na Kuwapora mali walizokuwa nazo,
Jamaa alikuwa Na mwili pia uso wa kutisha hivo ilikuwa Vigumu kumkabiri ukiwa peke yako hata mkiwa zaidi ya mmoja ilikuwa vigumu kumkabiri.
Jamaa alikuwa Ana uwezo wa kuteka Basi akiwa peke yake na kuwapora abiria wote Mali zao.
 
Story fupi kwa haraka
Katika kijiji cha Inama Inuka kulikuwa na Jama mmoja Jina lake Ndole, Jamaa Huyu alikuwa katili sana, Kwani Alikuwa anawatesa watu bila Huruma watu wasio na Hatia yoyote, Jamaa Ukimsalimia anakutusi Usipomsalimia anakupiga, (dawa yake ilikuwa ukimuona unamuepka) Mtu huyu alikuwa na Mtoto mmoja mdogo, na Mama mtoto huyo alikuwa alishaondoka kwa sababu ya Ukatili wa huyu jamaa ((nakumbuka alikuwa anakuja kwetu na kumchukua dada yetu ili akacheze na mwanaye Bila hata ridhaa ya Baba yetu)), Huyu jamaa alikuwa anaishi karibu na Barabara Ambapo walikuwa wanapita watu wengi Wengi wao walikuwa wakielekea Nchi jirani Ambapo walipokuwa wanafika pale wamechoka hivo ilikuwa inawalazim kuomba Huduma kadhaa kama Chakula,Maji,
Jamaa ukiomba Maji ya Kunywa alikuwa Anakuletea Ndoo ya Lita20 usipoyamaliza jamaa alikuwa Anakukata Kichwa, watu wengi aliwauwa kwa njia hiyo na Kuwapora mali walizokuwa nazo,
Jamaa alikuwa Na mwili pia uso wa kutisha hivo ilikuwa Vigumu kumkabiri ukiwa peke yako hata mkiwa zaidi ya mmoja ilikuwa vigumu kumkabiri.
Jamaa alikuwa Ana uwezo wa kuteka Basi akiwa peke yake na kuwapora abiria wote Mali zao.
Good attempt
 
Wewe ni mzuri?

Hicho ndio kigezo kikubwa kinachoangaliwa kwenye industry ya filamu ya bongo.
 
Back
Top Bottom