Nataka kuhama Bongo

Nataka kuhama Bongo

Kabla hujaondoka hapa, tafadhali wasiliana kwanza na Le Mutuz System.
Yeye ana uzoefu wa miaka 30 huko majuu na hataki kabisa kusikia habari za huko.
Lakini ushauri wangu, naomba ukomae hapa hapa nyumbani kwa sababu pana fursa kibao tu kama utajituma.
Tatizo la vijana hususan wanaomaliza chuo huwa wanakuwa na ndoto fulani za abunuwasi wanapokuwa huko, sasa wakishafika kitaa na kuona upepo tofauti, akili huwa zinawahama na kutamani kwenda majuu kwa sababu huwa wanahisi kwa hadhi ya elimu waliyonayo pamoja vyeti vyao, hawawezi kufanya kazi za huku kitaa ambazo ndio zinawatoa wengine.
duuh, hahaha, miaka 30, yaani thirty good years abroad na bado has nothing on his hand. pole sana.
 
nakushauri nenda AFGHANISTAN, utawakuta wenzio walima mimea ya cocaine na wabwia unga wenzio wengi sana, utaenjoi laifu sana kule. ukishindwa afghan, mwombe Mungu akusaidie uende ahera.


Nenda mwenyewe wivu tu wa kike
 
Sababu zipi zimekupelekea kutaka kuhama bongo?
 
alshababu wako Somalia bwana sio Mombasa na kericho...nenda mkuu au Kisumu na Eldoreti hakuna sehemu nzuri kama huko hapa duniani nimetembea nchi nyingi lakini huko nomaa safi sana...

uchumi wa eldoret ukoje??
Ukiweza taja na population,bongo hii michosho tu,better to find out for new challenges
 
alshababu wako Somalia bwana sio Mombasa na kericho...nenda mkuu au Kisumu na Eldoreti hakuna sehemu nzuri kama huko hapa duniani nimetembea nchi nyingi lakini huko nomaa safi sana...


Usalama ndio la Msingi zaidi kuliko mji unavoonekana Mkuu.
Sidhani hata kidogo kwenda huko.
 
Mie kuhama tz Lowasa akiwa rais itabidi nikutafute niwe mgeni wako tangulia mkuu
 
hahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,mkuu nini kimekukumba hapa tz hadi uhisi amani yako inatoweka?
 
Habari za Leo.

Nakuja hapa kwa heshima kubwa iliyo ndani ya Jukwaa hili.
Nataka kuhama Bongo/Tanzania Muda wowote ila sijaafiki Nchi nitakayoenda nitakapoondoka.

Hivyo naomba bila hiyana mniongoze katika hili

Je Ni Nchi gani Barani Africa hata Ulaya ,Amerika na Mashariki ya Kati naweza.kuwa Mhamiaji Bila Usumbufu?

Ushauri wako ni Muhimu Zaidi.

karibu sweden ..
 
Kama una fedha za kutosha nenda Malta na unapewa uraia mara moja. Lakini inatakiwa uwe na fedha... dola 865,000 ambazo utawekeza kwenye benki yao. Hii nchi wanasaka fedha za kufufua uchumi wao na passport yao inakuwezesha kutembea Ulaya na USA bila kuomba visa. Kuna na nchi ndogo ndogo kama Dominica nk ambazo hutoza fedha chache kidogo kama dola 100,000. Hata USA ukiwa na dola milion moja nadhani unaweza kupewa investor's visa (hii ya USA sina uhakika sana.


$500,000 kwa usa
 
Nenda Luxembourg. Ila ujue kifaransa. NI nchi ndogo iliyo tajiri na uchumi mzuri
 
Njoo hapa Bankok Thailand..fursa kibao, heshima rundo.kupata visa nenda Nairobi.kuna wa Nigeria na wa west kwa ujumla wengi sana hapa.maisha ni rahisi ambavyo huwezi kufikiria.usafiri, appartments, vyakula,biashara ni nyingi na hazina mikwara kama kwetu.wamachinga wamepewa nafasi kila kona..street hawkers na mama ntilie wa kutoka sehemu mbalimbali nje na thai wanashirikiana na wenyeji kufanya biashara.wenyeji wanaheshimu wageni ni balaa.ukishuka airport yao ya "subhanabhumi"utakaribishwa na bango kubwa"THE OPPORTUNITY HAVE LANDED WELCOME TO BANKOK"yaani wewe ni fursa umetua kwa hiyo unatakiwa kutumika.
Pia vijana wenzangu wenye kuwaza kufanya biashara za madini Bankok is the best place you can meet with international gemstones buyers
Njoo aise usiogope.mfano waweza pata appartment ye ye room 1 sebule, kitchen na toilet kwa 2500bhats.sawa na dola 80.bill za maji na umeme ni vichekesho.ni bhat 100 flat rate.gesi huku ndio kwao imeleta mapinduzi makubwa sana ya uchumi.watanzania tujiandaeni na ujio wa matumizi ya gesi yetu.tusiwaachie wahindi na wengine kutoka asia wa dominate sekta hii nikimaanisha biashara na fursa zinazotokana na gesi, biashara, gas stations zote ziwe za wazawa.katiba yetu itamke wazi mambo kama haya.ng'wabeja sana.
 
Nenda Afghanistan, Palestina ama Afrika ya kati...utasuuzika moyo wako kwani huko ni action tupu siyo km bongo ulikokuchoka.
 
Mimi nakushauri nenda nchi yoyote ya Kiarabu.
Habari za Leo.

Nakuja hapa kwa heshima kubwa iliyo ndani ya Jukwaa hili.
Nataka kuhama Bongo/Tanzania Muda wowote ila sijaafiki Nchi nitakayoenda nitakapoondoka.

Hivyo naomba bila hiyana mniongoze katika hili

Je Ni Nchi gani Barani Africa hata Ulaya ,Amerika na Mashariki ya Kati naweza.kuwa Mhamiaji Bila Usumbufu?

Ushauri wako ni Muhimu Zaidi.
 
Back
Top Bottom