Nataka kuanzisha Msikiti binafsi

Nataka kuanzisha Msikiti binafsi

Mbona umepanic! siku hizi kuna misikiti imejikuta ni sehemu ya tatizo hilo kwa kupokea watu wenye imani kali wanaotumiwa kuuhujumu uislam kwa kufanya matendo yanayoashiria ugaidi. Usikatae sema labda hujui.

ilitakiwa utoe ya kueleweka kama hivyo..
 
nawaomba mods hii thread ifungiwe na kama hamtaifunga basi hapa itoeni fasta na muipeleke huko jukwaa la dini .
 
nawaomba mods hii thread ifungiwe na kama hamtaifunga basi hapa itoeni fasta na muipeleke huko jukwaa la dini .
ustadhijuma Mimi nimetaka utaratibu. Nifanyeje ili nianzishe msikiti wangu mwenyewe. Ungeniambia unatakiwa kufanya 1,2,3...basi. Au hiki kitu hakiwezekani ningekuelewa mkuu. Kakini nakushangaa unaniombea mabaya kwa Allah.
 
Last edited by a moderator:
Hapana mkuu. Siyo makanisa yote ni Mali ya wakristu. Kuna makanisa yanawamiliki wakristu na siyo wakristu wanamiliki makanisa. Makanisa haya yanayojiita ya kiroho yanamilikiwa na watu binafsi kabisa. Na ile michango yote inayotolewa, sadaka,zaka na hata fungu la 10 hawa wamiliki wanachukua mzigo wooote. Tofauti kabisa na RC, na KKKT. Hawa michango tunayotoa inaturudia tena katika huduma za kijamii kama mashule, na hospitali.

mkuu unapoongela kanisa unakuwa unaongelea ukristo namaanisha "mlutheri anaweza hama kutoka ulutheri na kwenda kwenye hayo makanisa ya kiroho vivyo hivyo kwa hao wengine pia"

mfano kuna waislamu wanaojiita Shia Sunni, Almadiya Nk .. Na wanakuwa na imani moja (UISLAM) ila wanapingana kiitikadi na kimienendo.. ndio mana ukiangali taasisi ikishakuwa kubwa kuna kuwa na ukinzani na watu wanakuwa na mitizamo tofauti misimamo pia inabadilika na hapo watu ndipo wanapoamua kuanzisha taasisi zao binafsi.
 
nawaomba mods hii thread ifungiwe na kama hamtaifunga basi hapa itoeni fasta na muipeleke huko jukwaa la dini .

wewe ni nani unataka kutawala jukwaa? ni siri gani hutaki huyu mtoa mada aijue .. wewe mpe njia au utaratibu wa kuweza fanikisha lengo lake.
 
ustadhijuma Mimi nimetaka utaratibu. Nifanyeje ili nianzishe msikiti wangu mwenyewe. Ungeniambia unatakiwa kufanya 1,2,3...basi. Au hiki kitu hakiwezekani ningekuelewa mkuu. Kakini nakushangaa unaniombea mabaya kwa Allah.

kama unataka kujenga msikiti na uwe kwa ajili ya ibada na uislamu kwa ujumla na wala si kwa maswilahi binafsi
 
Last edited by a moderator:
wewe ni nani unataka kutawala jukwaa? ni siri gani hutaki huyu mtoa mada aijue .. wewe mpe njia au utaratibu wa kuweza fanikisha lengo lake.

jeuri ya kuniuliza mm ni nani umeitoa wap? kwanza kabisa huu uzi upo against na jf rules now kuna jukwaa la dini kwa nn usipelekwe huko then kama mnataka kushirikiana kufungua msikiti binafsi basi muanzishe na dini yenu...pitia maelezo yangu hapo juu nimetoa ushahd (dalili)kutoka ktk qur,ani kuonyesha kuwa misikiti yote ni ya allah na imma kusema msikiti huu ni wangu ni makosa
 
ngoja waje wahusika watakueleza kwa uzzuuuri mie napita
 
hata makanisa yote ni mali ya wakristo ila utofauti unakuja kwenye misimamo.

je, dini ya kiislam haina madhehebu? kama inayo basi hata mtu binafsi anaweza kuanzisha la kwake kwa misingi anayoiona yeye itamfaa.

Madhehebu yapo bt hawatofautian kwenye ibada.ibada ni ileile
 
Unaweza kuupa jina lako bt huwez kuanzsha ibada zako ata uwe ostadh kiac gan.ibada ni ileile
 
Kwanza kabisa naomba nianze kwa maamkizi mema Assalam alleykum warahmatullah wabarakatul.
Ama baada ya kumshukuru muumba wa mbingu na ardhi na ambaye ametakasika kwa sifa zote njema, hakuzaa wala kuzaliwa na si mwingine bali ALLAH SW na kumtakia rehma na amani mtufuku wa darja MTUME MUHAMMAD SAW naomba mada hii niichangie kwa kuanza kwa Quran 72:18 kuwa, Misikiti yote ni mali ya Mwenyezi Mungu na msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu. Hii haina maana tujenge misikiti kwa mtu mmoja au kikundi lakini lengo ikiwa kumuabudu na kumtakasa YEYE PEKEE na kwa kufuata Kitabu chake Quran na Sunnah tulizoachiwa na Mtume SAW

Unapojenga msikiti ina maana lile eneo ulilojenga umelitoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ie Wakfu hivyo basi huo msikiti hautakuwa wako binafsi hata kama uliujenga kwa pesa zako halali na unauhudimia kwa kila gharama inayotakiwa.
Vilevile utambue kuwa lazima ufuate kitabu cha Mwenyezi Mungu ie Quran na Sunnah alizotuachia Mtume Saw. Hivyo hauwezi kuwa msikiti wako binafsi bali umejenga na utakuwa miongoni mwa waliowekeza Swadakatuljaliah

Msikiti kama hautafuata mambo hayo yaliyoainishwa hapo juu ina maana utakuwa na sheria na taratibu zako binadamu. Huo sasa ndio utakuwa sio msikiti, sinagogi wala nini bali nyumba ya ibada uzijuazo wewe mwenyewe. Allah sw atuepushe na hili

Kwa haya machache nawasilisha Mwenyezi Mungu anajua zaidi

Wosia wangu
Mwanzo Jamii forum ilikuwa nyumba ya maarifa lakini kwa sasa imekuwa nyumba ya matusi, kashfa, kebehi, dharau na mengine yote mabaya. Jamani hebu turejee katika misingi ya Great Thinkers
 
Taasisi za kidini zinasajiliwa katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Hii ni pamoja na makanisa, misikiti, huduma au taasisi yoyote inayojihusisha na mambo ya kidini.
Hakuna tofauti kubwa katika taratibu za usajili kati ya shirika au chama cha kijamii na taratibu za usajili wa taasisi ya kidini. Tofauti unaweza kuwapo katika katiba, muundo wa uongozi na taratibu za uendeshaji.
Ili kusajili taasisi ya kidini zitahitajika nakala za katiba zisizopungua tano kwa kuwa katiba hiyo yaweza kuhitajika katika ngazi ya kata na wilaya kabla ya kwenda Wizara ya Mambo ya Ndani.
Mwishoni zinatakiwa zibaki nakala tatu za katiba hiyo ambazo zitapelekwa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa ajili ya kuwasilisha maombi ya usajili.
Mtapaswa kujaza fomu mbili yaani SA. 1 na SA. 2 na kutoa nakala nyingine mbili za fomu hizo. Fomu hizo zinapatikana katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani – Ofisi ya Msajili wa Taasisi za Kidini.
Katika fomu hizo mtahitajika kujaza taarifa mbalimbali ikiwemo; Jina, Mahali ofisi za taasisi zilipo,
 
acheni kupotosha nyie makafiri wakubwa
Misikiti yote ni ya mwenyezi mungu,, hakuna mwenye hati miliki ya msikiti wowote hapa duniani
 
Kama ilivyo kwa makanisa binafsi. Kina kakobe, Mwingira, Gwajima na Lusekelo. Haya makanisa ni Mali yao binafsi.

Ni utaratibu gani naweza kufuata nikaanzisha Msikiti binafsi?

Hakuna 'msikiti binafsi', labda utafute jina jingine la kuipa hiyo nyumba yako ya 'ibada'. Unaweza kuanzisha taasisi yako binafsi lakini sio 'msikiti'.
 
hata makanisa yote ni mali ya wakristo ila utofauti unakuja kwenye misimamo.

je, dini ya kiislam haina madhehebu? kama inayo basi hata mtu binafsi anaweza kuanzisha la kwake kwa misingi anayoiona yeye itamfaa.

Dhehebu ndio 'msikiti'? Katika uislamu, watu wa madhehebu tofauti wanaweza kuswali katika msikiti mmoja! Hakuna msikiti binafsi..
 
Hapana mkuu. Siyo makanisa yote ni Mali ya wakristu. Kuna makanisa yanawamiliki wakristu na siyo wakristu wanamiliki makanisa. Makanisa haya yanayojiita ya kiroho yanamilikiwa na watu binafsi kabisa. Na ile michango yote inayotolewa, sadaka,zaka na hata fungu la 10 hawa wamiliki wanachukua mzigo wooote. Tofauti kabisa na RC, na KKKT. Hawa michango tunayotoa inaturudia tena katika huduma za kijamii kama mashule, na hospitali.

kanisa ni mali ya Mungu ..Mungu humchagua mtu ampendaye ambaye ni mwaminifu kwake na kumpa jukumu la kulichunga/ kuliongoza kanisa ili watu wapate uponyaji wa roho na mwili (ndio maana hata waislamu utawakuta kanisani jambo ambalo ni vigumu kwa wakristo kuwakuta msikitini.)
 
Hapana mkuu. Siyo makanisa yote ni Mali ya wakristu.

Kuna makanisa yanawamiliki wakristu na siyo wakristu wanamiliki makanisa. Makanisa haya yanayojiita ya kiroho yanamilikiwa na watu binafsi kabisa.

Na ile michango yote inayotolewa, sadaka,zaka na hata fungu la 10 hawa wamiliki wanachukua mzigo wooote. Tofauti kabisa na RC, na KKKT.

Hawa michango tunayotoa inaturudia tena katika huduma za kijamii kama mashule, na hospitali.

Usipotoshe mkuu!

Makanisa mainstream yanachukua mpunga vizuri sana, tena kuwazidi akina Ngwajima. Wao wana miradi vitega uchumi, ambavyo vilianzishwa kwa sadaka za waumini lakini faida yake wanaroll nayo yote, check!

Shule na Hospitali, you still buying that ----? Waliingia mkataba na Serikali, wanapokea fedha za ruzuku kutoka Serikalini, FaizaFoxy atakuja kunieleza ni kiasi gani, na kwenye afya wameingia mikataba ya uendeshaji, Serikali inaweka watumishi na kuwalipa, na bado unachangia tozo la huduma, check!

Shule zinaendeshwa kama NGO, ada nafuu (uongo), na fedha za wahisani, wanaosapotiwa na Serikali za nje zinazotuibia, check!

Sadaka haikatwi kodi wala kufanyiwa auditing, ukitokea wizi ni kimya kimya, mfano Ujenzi wa Ukumbi wa Rugambwa, Ostabei ambao ulianza kutafutiwa fedha kwa mchango wa pili tangu Nyerere anasali pale, check!

Wana mchango wa pili kwa kila PR ya Kijamii wanayofanya, kutembelea wagonjwa, kuona yatima na kadhalika, wanaona uchungu sana kutoa sehemu ya mafungu yao kwa kazi hiyo, check!

Ni wezi, wanasisitiza maandiko yanayohamasisha sadaka, na nyimbo zake pia! Lile andiko la 'Ukikosana na nduguyo usilete sadaka yako...' huwa linakwepwa kama si kutotajwa kabisa, check!

Kimsingi yana historia ya wizi, biashara ya utumwa, kuunga mkono uvamizi na kusapotiana na wakoloni, rejea; wamisionari, check!

Hawa wanawaibia kwa mujibu wa sheria, na kwa akili ya hali ya juu, maamuma kondoo huwezi kuona, check!

Angalia uhusika wao wa moja kwa moja kwenye mambo yanayokuza ustawi, ujasiriamali, kukopesha, kusaidia mayatima, wajane, wagonjwa n.k, utagundua ni hasi au sifuri, check!

Ni matajiri kuliko makampuni mengi, wewe hujui hilo, check!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom