Nataka kuanzisha Msikiti binafsi

Nataka kuanzisha Msikiti binafsi

Ziroseventytwo

Platinum Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
9,163
Reaction score
17,067
Kama ilivyo kwa makanisa binafsi. Kina kakobe, Mwingira, Gwajima na Lusekelo. Haya makanisa ni Mali yao binafsi.

Ni utaratibu gani naweza kufuata nikaanzisha Msikiti binafsi?
 
Nijuavyo mimi misikiti yote ni binafsi.

Arusha ni mfano mzuri msikiti wa Bonmdeni unamilikiwa na familia ya Mkindi uwanja ulikuwa wa Babu yao BAKWATA wamejaribu kuleta uongozi wenye msikiti wamekataa na msikiti wao.

Ukienda msikiti wa Kaloleni ni hivyo hivyo.
 
Nijuavyo mimi misikiti yote ni binafsi.Arusha ni mfano mzuri msikiti wa Bonmdeni unamilikiwa na familia ya Mkindi uwanja ulikuwa wa Babu yao BAKWATA wamejaribu kuleta uongozi wenye msikiti wamekataa na msikiti wao.Ukienda msikiti wa Kaloleni ni hivyo hivyo.

Mkuu Ngongo, navyojua Mimi mtu kutoa uwanja kwa ajili ya kujenga msikiti haimaanishi kuwa huo msikiti ni wa binafsi.

Kwa mfano mtu mwenyewe kanisa binafsi ibada yake inaendeshwa tofauti na makanisa mengine. Lakini c kwa misikiti. Ibada yake ni ile ile.
 
Una nia nzuri na Allah awe nawe na utafanikiwa tu, usikatishwe tamaa na changamoto zitakazo kutokea kutimiza lengo lako.
 
Hamna msikiti binafsi kwa uelewa wangu kwa ufahamu wangu, ukijenga ni mali ya waumini wote, labda uanzishe dini yako out of islam
 
misikiti ni mali ya waislam wote

hata makanisa yote ni mali ya wakristo ila utofauti unakuja kwenye misimamo.

je, dini ya kiislam haina madhehebu? kama inayo basi hata mtu binafsi anaweza kuanzisha la kwake kwa misingi anayoiona yeye itamfaa.
 
hata makanisa yote ni mali ya wakristo ila utofauti unakuja kwenye misimamo.

je, dini ya kiislam haina madhehebu? kama inayo basi hata mtu binafsi anaweza kuanzisha la kwake kwa misingi anayoiona yeye itamfaa.

Hapana mkuu. Siyo makanisa yote ni Mali ya wakristu.

Kuna makanisa yanawamiliki wakristu na siyo wakristu wanamiliki makanisa. Makanisa haya yanayojiita ya kiroho yanamilikiwa na watu binafsi kabisa.

Na ile michango yote inayotolewa, sadaka,zaka na hata fungu la 10 hawa wamiliki wanachukua mzigo wooote. Tofauti kabisa na RC, na KKKT.

Hawa michango tunayotoa inaturudia tena katika huduma za kijamii kama mashule, na hospitali.
 
Una nia nzuri na Allah awe nawe na utafanikiwa tu,usikatishwe tamaa na changamoto zitakazo kutokea kutimiza lengo lako.

yani nawe wamsupport kwa akiri zake za kijinga "eti nianzishe msikiti binafsi" ktk uislamu hakuna msikiti binafsi yote ni ya allah
 
nani kakwambia misikiti ni nyumba za kufuga magaidi? akiri zipo chini ya hekaya ya mmarekani ....nakuonea huruma maskini wa akiri

Mbona umepanic! siku hizi kuna misikiti imejikuta ni sehemu ya tatizo hilo kwa kupokea watu wenye imani kali wanaotumiwa kuuhujumu uislam kwa kufanya matendo yanayoashiria ugaidi. Usikatae sema labda hujui.
 
Hamna msikiti binafsi kwa uelewa wangu kwa ufahamu wangu, ukijenga ni mali ya waumini wote, labda uanzishe dini yako out of islam

mkuu mi nna mashaka na huyu mleta mada yawezekana akawa si muislam...amekuja hapa kuudharirisha uislamu
 
Back
Top Bottom