ROKY
Senior Member
- May 4, 2011
- 182
- 70
Habari zenu wana-JF,
Mimi ni mjasiriamali ninayetaka kujikita katika kilimo kikubwa cha kibiashara.
Ninafungua mashamba mapya maeneo ya Ruvu, mkoa wa Pwani.
Kwa kuanzia ninapanga kulima mpunga na kufuga samaki. Nikishasimama vizuri nitaongezea kilimo cha mazao mengine kama mboga na matunda kwa ajili ya soko la Dar es Salaam.
Natafuta taasisi zinazotoa mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kilimo, taasisi za hapa Tanzania au za nje.
Nimepitia mabenki mbali mbali kama TIB lakini wana masharti magumu kama vile kuwa na dhamana ya nyumba, pia hawakopeshi mkulima anayeanza (yaani start-up farmer), n.k.
Wana-JF naomba yeyote anayefahamu taasisi zinazotoa mikopo ya kilimo kwa masharti nafuu anijulishe ili niweze kuongezea nguvu juhudi zangu za kujikita kwenye kilimo kikubwa.
Kwa sasa ninaanza kidogo kidogo shughuli hizi za kilimo.
Natanguliza shukrani zangu.
Roky.
Mimi ni mjasiriamali ninayetaka kujikita katika kilimo kikubwa cha kibiashara.
Ninafungua mashamba mapya maeneo ya Ruvu, mkoa wa Pwani.
Kwa kuanzia ninapanga kulima mpunga na kufuga samaki. Nikishasimama vizuri nitaongezea kilimo cha mazao mengine kama mboga na matunda kwa ajili ya soko la Dar es Salaam.
Natafuta taasisi zinazotoa mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kilimo, taasisi za hapa Tanzania au za nje.
Nimepitia mabenki mbali mbali kama TIB lakini wana masharti magumu kama vile kuwa na dhamana ya nyumba, pia hawakopeshi mkulima anayeanza (yaani start-up farmer), n.k.
Wana-JF naomba yeyote anayefahamu taasisi zinazotoa mikopo ya kilimo kwa masharti nafuu anijulishe ili niweze kuongezea nguvu juhudi zangu za kujikita kwenye kilimo kikubwa.
Kwa sasa ninaanza kidogo kidogo shughuli hizi za kilimo.
Natanguliza shukrani zangu.
Roky.