Natafuta Shamba

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,578
Reaction score
28,700
Wakuu natafuta shamba la kununua lenye ukubwa usiopungua hekari 30, kwa ajili ya project yangu ya kilimo mwaka ujao ninayotegemea kuifanya nje kidogo ya jiji la Dar es Salam, shamba hilo naomba liwe na sifa zifuataazo:


  1. Liwe na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo hususani mahindi
  2. Liwe eneo lenye water-table iliyo karibu, eneo ambalo nikichimmba kisima cha ku-drill nitapata uhakika wa maji kuanzia lita 5,000 kwa siku, na iwe ni kwa mwaka mzima.
  3. Liwe pembezoni mwa mji lakini umbali usizidi km 50 kutoka Dar es Salaam.
  4. Liwe linafikika kwa urahisi kwa gari kwa ajili ya kusafirisha mazao yangu kutoka shambani
  5. Uwepo wa umeme japo si muhimu sana

Kwa mwenye kuwa nalo au yeyote mwenye kuuza naomba tuwasiliane hapa au kwa PM hususani kwa mambo kama bei, vibali na location.

Natanguliza shukrani
 

Maeneo ya hivyo ni lazima yawe huko Mlandizi,Kibaha,Kisarawe,na Mkuranga. Ila kama una ubavu nenda Bagamoyo maeneo baada ya kupita Kiwangwa kama unakwenda Msata, ile ardhi inamea mahindi vizuri sana, tatizo iko nje ya umbali unaotaka ww. Umeme upo, ndio unapita sasa, na maji ndio wanatawanya sasa hivi ya bomba.

Au jaribu Kidugalo, kuna ardhi nzuri sana ya mahindi,ila maji mtihani,umeme bado. Ni km 100 hivi toka Dar kwenda kule. Gwata ni km 115 toka Buguruni kwenda kule, tatizo la Gwata ni mifugo,ila ardhi ipo kubwa.
 

Malila kila siku unanipa kibwagizo kipya , Gwata ni wapi huko?
 
Kuna shamba kisalawe lina hekali24 lina sifa zote ila lipo km,60 kutoka dar
 

Lipo dar es salaam zoo mbele heka moja 2m
 
Malila kila siku unanipa kibwagizo kipya , Gwata ni wapi huko?

Zipo Gwata mbili, mimi nazungumzia Gwata ya Kisarawe. Kama ukifika Mzenga, kuna njia inakwenda Mafizi kupitia Mwanamsekwa, Nyani hadi Gwata. Gwata pana watu wengi sana,wakulima na wafugaji,usafiri wa bus kuja Buguruni upo kila siku, usafiri wa tren upo. Ardhi ipo nzuri sana kando ya mto Ruvu. Lipo gulio kubwa kwa siku nne mfululizo,la mifugo zaidi. Biashara ya nyumba za wageni inalipa sana kuanzia alhamisi mpaka jumapili.

H/shauri ya Kisarawe wanataka kujenga mnada wa kisasa pale,viwanja vimepanda bei vibaya baada ya plan hiyo kuwekwa peupe. Mimi nilifuata ardhi ya kuotesha cocoa. Jamaa zetu Waarabu wamekomba mapande ya ardhi kinoma. Sijasikia ugomvi wa ardhi kule. Maji ni mto Ruvu, ni nguvu yako. Na migomba inamea pia.

Gwata ya pili iko Migindu huko Chalinze,

Swali lingine kaka!!!!!!!
 

Ahsante
 

Hebu siku moja tufanye tuonane tufunge safari tukatembelee hiyo mitaa maana kwangu ni sehemu ngeni kabisa.

Ardhi ya huko bei zikoje?
 
Hebu siku moja tufanye tuonane tufunge safari tukatembelee hiyo mitaa maana kwangu ni sehemu ngeni kabisa.

Ardhi ya huko bei zikoje?

Kwa eka moja ilikuwa Tsh 50,000/ kwa eka, juzi nilisikia imepanda mpaka 80,000/ kwa eka. Naamini baada ya hawa jamaa kutoka mashariki ya kati kuvamia itakuwa inacheza kwenye laki moja hivi.

Nikirudi Dar mwisho wa mwaka tutafutane tukatembee mitaa ya kule.
 

Thnx kwa info,kiongozi vp khs Nguvu kz! Tractor zinapatikanaje huko?
 
Thnx kwa info,kiongozi vp khs Nguvu kz! Tractor zinapatikanaje huko?

Mkoa wa pwani nguvu kazi ni tatizo kubwa sana, ukiona mtu ana nguvu kazi nzuri basi ujue kaitoa mikoa ya mbali,sio Pwani na Lindi. Kwa upande wa trector, naomba niwe mkweli,sikuona,labda kwa vile haukuwa msimu wa kulima.
 



Lipo moja kijiji cha Zegero ni kilomita 35 toka Mlandizi Mjini. 0715 203386
 
Shukrani sana mkuu naona ulipo hakiharibiki kitu mkuu...

Umegusia suala la mifugo naomba kuchomekea hapa hapa maana uzi ni wangu haitakua shida sana

Naomba kama una details za namna ya kuotesha majani kwa ajili ya ng'ombe wa maziwa kisasa utusaidie, maana nasikia Kenya kuna watu wanalisha ng'ombe 30 wa maziwa kwa kutumia hekari 1 kwa mwaka mzima kwa kuwaoteshea majani.

Kama una lolote juu ya hili naomba msaada wako tafadhali mkuu
 
Mkuu samahani kwa kuingilia uzi, kwa swali lako la kuotesha majani ya mifugo wengi kwenye eneo dogo, technology inayotumiwa kenya kwa manufaa makubwa ni hydroponic fodder hii ni technologia ya kukuza mimea bola udongo na kwa majani ya mifugo wanatimia zaidi barley kiswahili chake sijui. Ndani ya siku saba unakwa umeshapata majani mabichi kwa mifugo yako. Ni technology ngeni kidogo lakini naona wemzetu wemufaika . Kwa maelezo jinsi ya kupata technologia hii google hyroponics kenya. Kuna bwana ambaye anauza technologia hii na siyo gharama kubwa sana.
 
Shukrani sana mkuu

Ngoja nifuatilie google nitaleta mrejesho

Nashukuru sana kwa moyo wako wa ku-share aisee
 
Karibu mkuu, naamini mtanzania akipata technologia hii itakuwa rahisi na wengine pia kupata kwa urahisi.
 
Karibu mkuu, naamini mtanzania akipata technologia hii itakuwa rahisi na wengine pia kupata kwa urahisi.
Mkuu nimefuatilia hii kitu imenistusha sana aiseee

Hekari moja ya ardhi inaweza kulisha ng'ombe zaidi ya 500 wa maziwa kila siku kwa mwaka mzima(non stop daily).
Nimeshangaa sana aisee,hii technology imeshafika mpaka Kenya na wako tayari kuoa training kwa mtu yeyote kwa gharama ya Ksh 1500 around Tsh 30,000 na wako tayari kukupeleka mpaka site ukafanya kwa vitendo.

Ni teknolojia simplena nafuu sana hasa kwenye maeneo ya maji na uhaba wa ardhi aisee

Bado nafuatilia, nimejaribu kuwasiliana nao kwa email nafikiri watanijibu soon, ili nipate details nyingi zaidi

Ila naona hii kitu inawezekana sana hasa hapa Bongo.

Nikipata details zote na training yao ntamwaga hapa jamvini data zote ili kila mtu afaidike

Shukrani sana kwa moyo wako mkuu hasa kwa kunipigisha hatua katika ndoto yangu ya kumiliki kiwanda cha maziwa soon.
 
Asante nami nasubiria hapa nipate ujuzi zaidi. Ila hii habari ya maji nayo yaweza kuwa kikwazo kiangazi ambapo ndo malisho adimu. Labda tujue kama inakubali maji ya kisima pia.
 
Mkuu ASIGWA heshima kwako tunasubiri miBARAKA ya hiyo kitu unaenda kuchimbua! Tunapokuwa na Options nyingi inasaidia kufanya uchaguzi wa Busara kwamba kipi kinafaa kufanya kwa wakati gani na kwann! Kuwa na mifugo michache yenye Afya ndo ufugaji wa kisasa! Kiukweli wengine tunafaidika sana na Michango yenu wakuu Hongera kwa aliekuwa na Wazo lakuanzisha JF!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…