Natafuta kazi, Nina Diploma ya Kilimo

Natafuta kazi, Nina Diploma ya Kilimo

Ww hapo ulipo ni ajira tosha unaweza kujiajiri ingia vijijini katoe elimu mjomba
 
Mimi ni muhitimu Wa stashahada ya kilimo na mifugo mwaka 2016 natafuta kazi kulingana na taaluma niliyo somea,,umri wangu miaka 25 napatikana Dodoma,,

Naomba kwa yeyote anisaidie kupata kazi hata kwenye mashirika binafsi,miradi ya kilimo na mifugo,,taasisi za utafiti wa mazao na wadudu,,natanguliza shukrani kama ntasaidiwa mtaani kugumu sana!!!
Jamani una diploma ya kilimo hlf unatafuta kuajiliwa.? Cooome on hebu katafute shamba bwana
 
Magufuli anagawa mashamba kwa kina bahkresa mwambie na wewe akugawie ulime kama umesoma kilimo sidhani kama unashida na ajira
 
Mimi ni muhitimu Wa stashahada ya kilimo na mifugo mwaka 2016 natafuta kazi kulingana na taaluma niliyo somea,,umri wangu miaka 25 napatikana Dodoma,,

Naomba kwa yeyote anisaidie kupata kazi hata kwenye mashirika binafsi,miradi ya kilimo na mifugo,,taasisi za utafiti wa mazao na wadudu,,natanguliza shukrani kama ntasaidiwa mtaani kugumu sana!!!

Nzega kuna eneo nataka kulima na kufuga je tunaweza fikiria kufuga nini au kulima nini mie ntatoa mtaji,uko tayari kukaa nzega?
 
Dah kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa yani kuna miwatu inafikiri kujiajiri ni kitu chepesi sana. Hamjui kuwa 70% ya mtaji wa biashara ni pesa? Unaweza kuwa na ideas kibaoo lakin kama hakuna pesa hamna kitu utafanya. Msizani kujiajiri ni makalio ambayo kila mtu ana uwezo wa kuwa nayo. Kujiajiri ni mchakato mrefu unaohusisha vitu vyingi ambavyo huunganishwa na pesa ili kutengeneza hio ajira yako.
 
Akili ndogo mkiwa Form six ndo mnafikiria hivi kwa Kijana wa Kimasikini aliyesoma kwa kutegemea Loan Board akimaliza na Kuanza kuhangaika ajira ni Sawa kabisa kilimo kipi atakifanya hapo atanunua na nini mbegu bora kila anayevuna pesa nzuri alianza kuajiliwa ukishapokea mishahara yako kadhaa ndo unafungua biashara. So si aibu kwa mdau hapo kutafuta kazi ila kama unataka kilimo cha kula tuu mwenyewe unaweza kufanya ila kilimo cha tija kinahitaji Pesa nyingi.
Dat is nonsense. Tatizo vijana hwapendi kuumiza kichwa. Apo utakuta kapost hili andiko kwa smartphone ya lakitatu. Lakini kwa kilimo cha tz hata kama una elfu 30000 unaweza aza kilimo na ukamake wonders. Wengi vijana wanakimbilia kilimo kikubwa bila experience. Hata kama umesoma kilimo ila bado huna experience. Think big but start small, get experience and diversify. Hapa ndipo vjana wa kikenya wanapotuacha mbali
 
Msaada wenu ndugu zangu kukaa sana mtaani hakufai bola nipate hata kazi ya kujitolea kuongeza ujuzi
 
vipi nikikupa kusimamia shamba eka 20? gharama ya pembejeo, nk vyote kwangu.
sikulipi mshahara ila tukutane kwenye mavuno. hapo vipi?
 
vipi nikikupa kusimamia shamba eka 20? gharama ya pembejeo, nk vyote kwangu.
sikulipi mshahara ila tukutane kwenye mavuno. hapo vipi?
Tuwasiliane tuyajenge sote wa tz ndugu
 
Back
Top Bottom