Nasumubuliwa na tatizo la GERD / Acid reflux

Nasumubuliwa na tatizo la GERD / Acid reflux

Huku mitaani mnatumia dawa bila kufanya vipimo kuhakiki kama kweli ni vidonda vya tumbo..kipimo pekee cha kuhakiki vidonda vya tumbo ni Endoscopy..ambapo mtaalamu atapitisha tube nyembamba mdomoni ikiwa na camera kwa mbele mpaka ifike kwenye utumbo mdogo..hiki kipimo ni ghali kidogo,kama huna bima andaa laki 3.

Lengo ni kuhakiki kama kweli client ana vidonda vya tumbo,na kama vipo vipo kwa uwingi gani na vina ukubwa gani.Acheni kutumia dawa za vidonda vya tumbo bila kufanya vipimo. Watu wengi wana H pylory ukiwapima stool,lakini unakuta hana dalili za vidonda vya tumbo..pia kuna watu wanapata Acid Reflux lakini hana vidonda vya tumbo.

Hivyo kipimo pekee cha ku verify vidonda vya tumbo ni Endoscopy.

Cc MENEMENE TEKERI NA PERESI
Asante mtaalaamu kwa kuongezea
 
upo sahihi kwenye maelezo, je kwa matumizi ya limau hayatonizidisha tatizo? mana wadau wamenambia niache tumia vitu vyenye acid
Usijaribu kutumia malimao ilihali una acid reflux, kuna watu wamepata acid reflux kwa kunywa malimao wakati mwanzo walikuwa wazima. Shauri ya kusikiliza madaktari uchwara wa mitandaoni
 
Limao ni very weak acid ambayo itaweza ku lower hydrochloric acid inayozalishwa na kuongeza hydrogen chloride gas inayokuchoma!!

Pia doctor anaweza kukushauri utumie ant acids kama magnesium pia!!

Maji moto ni long term solution ikiwa ni habit Yako ya kila siku ili ku refresh digestive system!!
Limao italower hydrochloric acid? Chemistry ya wapi hii mkuu? Hivi kama wewe sio mtaalam wa kitu fulani si ukae kimya kuliko kuexpose your ignorance? Kutokujua kitu si dhambi, kama hujui usijioneshe kwamba unajua,hutapungukiwa kitu. Eti na " kuongeza Hydrogen Chloride gas inayokuchoma". Hata hujishtukii
 
Kwahiyo unatarajia weak acid ukichanganya na strong acid concentration ya strong acid itabaki vile vile!!?

Kinachomuunguza ni nini kama sio hydrogen chloride gas inayofanya reflux kwenye umio!!?

Unataka kuniambia ile hydrochloric acid inayozalishwa inaruka kuja kwenye umio!!?
Locally weak acid Ina uwezo wa ku lower concentration ya strong acid


Limao italower hydrochloric acid? Chemistry ya wapi hii mkuu? Hivi kama wewe sio mtaalam wa kitu fulani si ukae kimya kuliko kuexpose your ignorance? Kutokujua kitu si dhambi, kama hujui usijioneshe kwamba unajua,hutapungukiwa kitu. Eti na " kuongeza Hydrogen Chloride gas inayokuchoma". Hata hujishtukii
hiyo
 
Kwahiyo unatarajia weak acid ukichanganya na strong acid concentration ya strong acid itabaki vile vile!!?

Kinachomuunguza ni nini kama sio hydrogen chloride gas inayofanya reflux kwenye umio!!?

Unataka kuniambia ile hydrochloric acid inayozalishwa inaruka kuja kwenye umio!!?
Locally weak acid Ina uwezo wa ku lower concentration ya strong acid



hiyo
Kwamba mkuu, weak acid ukichanganya na strong acid,ile strong acid itapungua ukali wake??Tena IN VIVO? Hebu tuandikie equation ya hiyo reaction.
Halafu kinachomuunguza mtu ni acid ndio maana hata dawa wanazopewa ni " anti acid", sio " anti gas". Acid inafikaje kwenye oesophagus? Zile muscles za kuzuia vilivyoko tumboni visirudi juu huwa zimelegea ndio maana hiyo acid inapanda juu na kusababisha hayo matatizo yote.
 
Kwa mwezi wa tatu sasa, nimekuwa nikusumbuliwa na maumivu ya kifua pamoja na kiungulia. Baada kujaribu kulienda deep tatizo nimegundua nasumbuliwa na hilo tatizo.

Naomba msaada wakuu
Pole sana mkuu. Kiungulia na maumivu ya kifua mara nyingi vinaweza kuhusiana na mfumo wa ulaji na mtindo wa maisha. Kwanza, jaribu kuacha kabisa sukari na kupunguza sana vyakula vya wanga kama wali, ugali, mikate, chapati, maandazi na hata maharage kwa kipindi fulani uone mabadiliko. Pia epuka matunda yenye sukari nyingi kama ndizi mbivu na yale yenye asidi nyingi kama machungwa na machenza. Maziwa nayo ni vyema ukayaepuka kwa muda.
Badala yake, kula zaidi protini (samaki, kuku, nyama, mayai, maini), mboga za majani, kabichi, pamoja na parachichi na matango kwa wingi. Haya matunda mawili yawe rafiki zako wa karibu.
Kuhusu mtindo wa maisha, jaribu kula milo miwili tu kwa siku na ufunge angalau masaa 12 kila siku. Mfano, mlo wa kwanza saa 5 asubuhi na wa mwisho saa 10 jioni. Baada ya hapo usile chochote zaidi ya maji. Pia epuka kula mara kwa mara na ukiweza, fanya mfungo wa masaa 24 angalau mara moja kwa wiki (unywe maji tu).
Hata hivyo, kwa kuwa maumivu ya kifua yanaweza pia kuwa dalili ya matatizo mengine muhimu ya kiafya, ni vizuri ukamuona daktari kwa uchunguzi na ushauri zaidi, hasa kama maumivu ni makali, yanarudiarudia, au yanaambatana na dalili nyingine.
 
Huku mitaani mnatumia dawa bila kufanya vipimo kuhakiki kama kweli ni vidonda vya tumbo..kipimo pekee cha kuhakiki vidonda vya tumbo ni Endoscopy..ambapo mtaalamu atapitisha tube nyembamba mdomoni ikiwa na camera kwa mbele mpaka ifike kwenye utumbo mdogo..hiki kipimo ni ghali kidogo,kama huna bima andaa laki 3.

Lengo ni kuhakiki kama kweli client ana vidonda vya tumbo,na kama vipo vipo kwa uwingi gani na vina ukubwa gani.Acheni kutumia dawa za vidonda vya tumbo bila kufanya vipimo. Watu wengi wana H pylory ukiwapima stool,lakini unakuta hana dalili za vidonda vya tumbo..pia kuna watu wanapata Acid Reflux lakini hana vidonda vya tumbo.

Hivyo kipimo pekee cha ku verify vidonda vya tumbo ni Endoscopy.

Cc MENEMENE TEKERI NA PERESI
Na hili ni tatizo la jamii zetu ,juzi binti mmoja aling'atwa na mbwa badala apelekwe hospitali apate matibabu wakaishia kumpakaa mafuta sijui ya nini ,wanajua wenyewe .

Leo dada kapumzika
 
Na hili ni tatizo la jamii zetu ,juzi binti mmoja aling'atwa na mbwa badala apelekwe hospitali apate matibabu wakaishia kumpakaa mafuta sijui ya nini ,wanajua wenyewe .

Leo dada kapumzika
Ila hii nchi, yaani hadi leo hii kuna watu hawajui kama mtu kang'atwa na mbwa kitu cha kwanza ni kumkimbiza hospital haraka? . Mi wakati nakua nimesimuliwa stori watu waliong'atwa na mbwa wakikosa matibabu wanaanza kubweka kama mbwa na kufanya niwe na hofu ingawa sijawahi kushuhudia mtu akifikia hiyo stage ya kubweka. Hao wanafamilia ya huyo binti hizo stori za watu kubweka kama mbwa wao hawajawahi kuzisikia? Kifo cha uzembe kabisa.
 
Back
Top Bottom