Mimi ni mtaalamu wa Afya,najua nacho kuambia,pia nmewahi kuugua ..na sijakataa kwamba wanasababisha vidonda vya tumbo lakini siyo vidonda vya tumbo vyote husababishwa na Hpylory..ila nimekuambia kwamba siyo kila mwenye hao bacteria ana vidonda vya tumbo. Wewe hujaelewa nini?
Ndo maana ukilalamika dalili za vidonda vya tumbo,Kipimo cha awali utapimwa uwepo wa antigens kwenye kinyesi chako kujua kama una Hpylory,,ukiwa Positive...
Daktari anaenda mbele zaidi sasa kuhakiki kama una vidonda tumbo kwa kufanyiwa Endoscopy,hiyo ndo itaonyesha kama kweli una hivyo vidonda ama majeraha tumboni,mtaalamu ataandika pia na uwingi wa hivyo vidonda pamoja na ukubwa wa hivyo vidonda,,
Then utapewa dawa kwa ajili ya kuwaua kwanza hao bacteria,then kidonda kitaendelea kupona taratibu.
Same kwa aliye kutwa negative Hpylory,,naye atafanyiwa hicho kipimo kujua kama ana vidonda. Asilimia kubwa ya vidonda husababishwa na Hpylory..lakini pia vipo vidonda tumbk havisababishwi na bacteria...
Karibu kwa mjadala zaidi.