Nasumubuliwa na tatizo la GERD / Acid reflux

Nasumubuliwa na tatizo la GERD / Acid reflux

dos.2020

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2009
Posts
14,653
Reaction score
12,364
Kwa mwezi wa tatu sasa, nimekuwa nikusumbuliwa na maumivu ya kifua pamoja na kiungulia. Baada kujaribu kulienda deep tatizo nimegundua nasumbuliwa na hilo tatizo.

Naomba msaada wakuu
 
Lilinisumbua pia sanaa, mpaka ilifika wakati nachukia kula, nkiona chakula nahisi ni adhabu, vyakula vya asidi, soda, kachumbari tulikuwa maadui.
nkaenda hospitali(ccbrt) wakanipima wakanambia nina kitu kama skosei wanaita “Hpylori” wakanipa dawa ( dozi ya mwezi).

Matokeo yake nakula kila kitu na nipo fresh kabisa now days.

Tafuta hospitali yakueleweka utapona.

Zingatia; dawa ina sehemu yake, mfumo wa kula ndo muhimu zaidi, kama bdo ni mtu wa pasi ndefu na kujibana dawa haitasaidie,. Kula kupita kiasi ni kichocheo cha tatizo hilo kwa asilimia kubwa.

Kula kidogo ila mara kwa mara
Mfano;
saa moja(chai pekee ya moto au maji ya moto) ,

saa nne(uji/chai+ vitafunwa)

saa nane(msosi wa kueleweka *sio kwa wingi)

saa kumi(chai/uji)

Cha usiku kuanzia saa 12~saa mbili * usichelewe kula usiku bora uache kula kama muda umeenda.
 
Lilinisumbua pia sanaa, mpaka ilifika wakati nachukia kula, nkiona chakula nahisi ni adhabu, vyakula vya asidi, soda, kachumbari tulikuwa maadui.
nkaenda hospitali(ccbrt) wakanipima wakanambia nina kitu kama skosei wanaita “Hpylori” wakanipa dawa ( dozi ya mwezi).

Matokeo yake nakula kila kitu na nipo fresh kabisa now days.

Tafuta hospitali yakueleweka utapona.

Zingatia; dawa ina sehemu yake, mfumo wa kula ndo muhimu zaidi, kama bdo ni mtu wa pasi ndefu na kujibana dawa haitasaidie,. Kula kupita kiasi ni kichocheo cha tatizo hilo kwa asilimia kubwa.

Kula kidogo ila mara kwa mara
Mfano;
saa moja(chai pekee ya moto au maji ya moto) ,

saa nne(uji/chai+ vitafunwa)

saa nane(msosi wa kueleweka *sio kwa wingi)

saa kumi(chai/uji)

Cha usiku kuanzia saa 12~saa mbili * usichelewe kula usiku bora uache kula kama muda umeenda.
Nina tatizo hilo, ulipewa daw gani?
 
Kwa mwezi wa tatu sasa, nimekuwa nikusumbuliwa na maumivu ya kifua pamoja na kiungulia. Baada kujaribu kulienda deep tatizo nimegundua nasumbuliwa na hilo tatizo.

Naomba msaada wakuu
Pole sana mkuu.

Hilo tatizo nami nilikuwa nalo, lakini naona kama limeisha ama kwa kiasi kikumbwa limepungua kabisa.

Ninachoshangaa katika statement yako kwamba 'uligundua'!
Kugundua tatizo nadhani hufanyika hosipitali.

Sasa kama ulienda hospitali ukapimwa na kupatikana na tatizo hilo, kwa nini usipate ushauri wa kidaktari namna ya kutibu tatizo lako hilo?

Usidhani kufanana kwa maumivu ni kufanana kwa ugonjwa, waweza kuwa na tatizo jingine katika mfumo wako wa proton pump likasababisha kiungulia.

Fika hospitali haraka, onana na madaktari, chukuliwa vipimo.

Ugonjwa huu si tatizo sana unapowahi matibabu na kubadili mfumo wa maisha.

Haya yote utayapata hosipitali, acha kuuliza madawa ili uanze kutumia bila ushauri wa daktari atakayepima na kuona ukubwa wa tatizo na kukupangia dose, hapana kufakamia dawa bila ushauri wa dr hata kama ugonjwa sahihi ni huo.
 
Naomba msaada wakuu
Tafuta Matembele
Chukua Brenda saga hayo matembele weka maji glass 1
Baada ya kusaga vizuri kunywa km Juice

Matembele yana virutubisho vingi muhimu ambavyo ni:

Vitamini A
Vitamini C
Vitamini K
Vitamini B-complex (B1, B2, B3, B6, na folate)
Madini muhimu (chuma, kalsiamu, magnesiamu, potasiamu, na zinki)
Protini na nyuzinyuzi (fiber)
Antioxidants (Viambata vya kupambana na sumu mwilini)

Tumia siku 2 mpaka 3 utaona maendeleo yako yanavyokua
 
Tafuta Matembele
Chukua Brenda saga hayo matembele weka maji glass 1
Baada ya kusaga vizuri kunywa km Juice

Matembele yana virutubisho vingi muhimu ambavyo ni:

Vitamini A
Vitamini C
Vitamini K
Vitamini B-complex (B1, B2, B3, B6, na folate)
Madini muhimu (chuma, kalsiamu, magnesiamu, potasiamu, na zinki)
Protini na nyuzinyuzi (fiber)
Antioxidants (Viambata vya kupambana na sumu mwilini)

Tumia siku 2 mpaka 3 utaona maendeleo yako yanavyokua
Ile harufu ya tembele bichi naweza kutapika.
 
Pole, kwa mujibu wa tafiti mpya, GERD na ulcers zinachochewa na kuzidi kemikali inaitwa histamine 2 na siyo H pylori (Kila binadamu ana H pylori lakini si lazima apate ulcers)

Kuna mimea ya kubalance na kukaa sawa ikiwemo mtomoko, unga wa parachichi na mjaafari kwa ratio maalum.tuwasiliane kwa 0713039875
 
Amoxicillin doz ya siku 5, (2*3)
Clarithromycin dozi ya wiki 2, ( 1*2)
Omeprazole dozi ya siku 30 (1*2)

Nashauri ufike hospitali kwanza
Amoxycilin na GERD? inakuwaje hapo mkuu naomba ufafanuzi.

Nina hiyo shida toka 2024, nilibadili tu mfumo wa maisha dawa sikutumia japo nilipewa
 
Pole, kwa mujibu wa tafiti mpya, GERD na ulcers zinachochewa na kuzidi kemikali inaitwa histamine 2 na siyo H pylori (Kila binadamu ana H pylori lakini si lazima apate ulcers)

Kuna mimea ya kubalance na kukaa sawa ikiwemo mtomoko, unga wa parachichi na mjaafari kwa ratio maalum.tuwasiliane kwa 0713039875
Huo mmea utaenda kukaza LES, (lower esphageal sphincter) ilolegea?
 
Option number 2

Nunua mafuta ya Mzeituni -Olive Oil yale ya kupikia

Kunywa kijiko 1 kikubwa cha chakula kutwa ×3, utaona hali yako inavyokua baada ya muda
Moja wapo ya makatazo ukiwa na GERD ni mafuta, sasa hapo inakuwaje mkuu
 
VIdonda vya tumbo hivyo...mcheki huyu mwalimu wa Udom akupe dawa inasaidia sana 0756869343...usisahau kuleta mrejesho..siku tano tu
 
Back
Top Bottom