Nasubiri mshahara wa Octoba 2017

Nasubiri mshahara wa Octoba 2017

20fanaka

Senior Member
Joined
Apr 19, 2017
Posts
144
Reaction score
138
Serikali ya awamu ya tano imekuwa inajinadi kuwa si ya kisiasa bali ni ya kiutendaji zaidi. Na President amekuwa akisema yeye ni msema kweli na anaamini kuwa msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Kwa dhana hiyo tu niliipa imani yangu na kuitetea mbele ya watu wanayoipinga. Hata pale ahadi ya serikali ya kushughulikia wafanyakazi hewa kwa miezi miwili ilipofeli niliyaelewa maelezo ya serikali kuwa tatizo ni kubwa kuliko walivyodhani.

Tulio na imani na serikali tulijipa mda wa kutosha kuwa atleast January 2017 italipa stahiki zilizosimamishwa ikiwa imeshamaliza uhakiki, HAIKUWA.

Tukasema tusubiri bunge la Feb tupate maelezo rasmi ya serikali kupitia kwa wawakilishi wetu, serikali ikakiri kumaliza uhakiki. Tukatumaini kwa kuchelewa basi April italipa, Holla.!!

Tukabashiri Serikali inajipanga kufanya fresh start ktk bajet mpya ya 2017/2018 ili July kieleweke, HAIKUWA

Serikali ikatoa maelezo bayana kuwa kilichokuwa kinatatiza ni rufaa za vyeti na kwamba hatma yake ilikuwa 30,Sept na kwamba tayari serikali ilikuwa imetenga fedha kwa ajiri ya increament na madaraja ambayo yangelipwa baada ya Septemba 30.

Hivyo mimi na watumishi wenzangu wenye nasaba kama zangu tnasubiri Oktoba hii.

Lakini kwa hii 'verse' mpya ya Mkuchika naanza kuwa na wasiwasi iwapo serikali hii ni ya 'wasemakweli' na 'watendaji' watatekeleza Octoba hii.

Baada ya Oktoba kupita bila increament na madaraja yaliyosimamishwa kurejeshwa, mtazamo wangu na wenzangu juu ya serikali hii utakuwa tofauti kabisa (hata kama malipo hayo yatafanyika April kabla ya Mei Mosi ambayo ni kejeli kabisa) nitajua tu kuwa sasa wafanyakazi tutakuwa tumegeuzwa punching bag ya serikali dhidi ya raia jambo ambalo ni unafiki, na tutafanya kazi kinafiki kweli..

KUTOKA NDO HATUTOKIII..!!!

UPDATE..
Postponed to November
Ok let's make it November, hata si mbali mbona
 
Serikali ya awamu ya tano imekuwa inajinadi kuwa si ya kisiasa bali ni ya kiutendaji zaidi. Na President amekuwa akisema yeye ni msema kweli na anaamini kuwa msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Kwa dhana hiyo tu niliipa imani yangu na kuitetea mbele ya watu wanayoipinga. Hata pale ahadi ya serikali ya kushughulikia wafanyakazi hewa kwa miezi miwili ilipofeli niliyaelewa maelezo ya serikali kuwa tatizo ni kubwa kuliko walivyodhani.

Tulio na imani na serikali tulijipa mda wa kutosha kuwa atleast January 2017 italipa stahiki zilizosimamishwa ikiwa imeshamaliza uhakiki, HAIKUWA.

Tukasema tusubiri bunge la Feb tupate maelezo rasmi ya serikali kupitia kwa wawakilishi wetu, serikali ikakiri kumaliza uhakiki. Tukatumaini kwa kuchelewa basi April italipa, Holla.!!

Tukabashiri Serikali inajipanga kufanya fresh start ktk bajet mpya ya 2017/2018 ili July kieleweke, HAIKUWA

Serikali ikatoa maelezo bayana kuwa kilichokuwa kinatatiza ni rufaa za vyeti na kwamba hatma yake ilikuwa 30,Sept na kwamba tayari serikali ilikuwa imetenga fedha kwa ajiri ya increament na madaraja ambayo yangelipwa baada ya Septemba 30.

Hivyo mimi na watumishi wenzangu wenye nasaba kama zangu tnasubiri Oktoba hii.

Lakini kwa hii 'verse' mpya ya Mkuchika naanza kuwa na wasiwasi iwapo serikali hii ni ya 'wasemakweli' na 'watendaji'

Baada ya Oktoba kupita bila increament na madaraja yaliyosimamishwa kurejeshwa, mtazamo wangu na wenzangu juu ya serikali hii utakuwa tofauti kabisa (hata kama malipo hayo yatafanyika April kabla ya Mei Mosi ambayo ni kejeli kabisa) nitajua tu kuwa sasa wafanyakazi tutakuwa tumegeuzwa punching bag ya serikali dhidi ya raia jambo ambalo ni unafiki, na tutafanya kazi kinafiki kweli..

KUTOKA NDO HATUTOKIII..!!!
ikiwa hujui falsafa ya chama cha mapinduzi basi subiri,chama kinachowajali wanyonge kinajipambanua siku zote katika kauli zake,kinamuelekeo ,na imani.
 
Kairuki aliongea ukweli alupokua anakabidhi wizara, pesa hakuna. Mkuchika anafanya drama tu kuwafanya watumishi wawe occupied wakati serikali anahaha kujaribu kuuokoa uchumi wa nchi unaoelekea "bonde la Hinom"
 
Mh! Wewe umeambiwa unahakikiwa umri bado unasubiri mshahara mpya!
 
"....mpaka uzalishaji uongezeke" mkuu
"....mpaka tuhakiki umri" mkuchika.
asante!
 
Kuna mtumishi ambae mpaka leo hii bado ana imani na serikali hii..??duh mimi mbwembwe zao tu mwanzoni nikajua hawana pumzi hawa.
Serikali inaweza tatizo haisemi ukweli, na imeshachelewa kuusema huo ukweli.
Inachopaswa kufanya sasa ni kulipa hayo madaraja waliyoyatoa kisha wakayasimamisha na mapunjo yake, watoe increament za miaka miwili na mapunjo yake, halafu wauseme huo ukweli sasa kuwa baada ya hapo hawaajiri tena, hawapandishi madaraja, hawaongezi increament, wala hawaongezi mishahara kwa kuwa HAMU YA SERIKALI KWA SASA NI KUKAMILISHA UJENZI WA UCHUMI MKUBWA (Miradi mikubwa ya umeme, ujenzi wa reli SGR, ununuzi wa madege na treni za mwendo kasi, ujenzi wa Fly Overs, Ujenzi wa miundo mbinu ya kilimo cha umwagiliaji, ujenzi wa bandari na mabarabara na viwanja vya ndege na ujenzi wa makao makuu Dodoma) Tutaelewa na tutajifunga mikanda.
Tunasubiri increament na madaraja turekebishe hali za maisha kisha tuendane na upepo, madeni yanatutoa msatarini kabisa fulu kudhalilika huku mitaani, raia wanatuinjoi tu
 
Hii serikali ndio inayoongoza kutoa ahadi hewa Afrika. Tatizo ni kukurupuka kwani wanachokisema na kukipanga huishia njiani na kuanza kurukia vyengine.
 
Kuiamini serikali hii ni kama ile kauli ambayo tulikuwa tukifundishwa kanisani "Kesheni mkiomba Yesu atarudi"!

Watumishi wanatakiwa wajifunze kujiongeza tu wenyewe kwa kumuibia muajiri hata muda tu unatosha kufidia haya madhira waliyoyaleta mbona ofisini siku hizi hakuna noma kama kitambo ile watu macho wazi siku hizi mnapangiana tu namna ya kumpiga muajiri ukijifanya wewe unakomaa hakika utaitesa familia uku unaona.
 
Back
Top Bottom