Nashindwa kuifichua siri hii

Nashindwa kuifichua siri hii

Muda unvyoendelea, ndivyo kosa lako linavyokuwa kubwa. Yaani kila shemeji yako anapotoka na rafiki yako mwenye kucheat, nawe unashirikishwa kiasi fulani jambo hilo. Haisaidii wewe kukaa kimya tu. Dunia huharibiwa si na wale watendao maovu tu, bali pia wanaoona maovu na hawafanyi lolote.
Jitwike ujasiri. Kwanza waepe kabisa wapenzi wawili wanaoharibu mambo. Hao si marafiki wazuri. Huyo mwanaume anaweza kukulia hata wewe kama hujui. Tafuta namba ya simu ya siri au unda moja ya kwenye mtandao. Kisha mpelekee ujumbe rafiki yako ananymously kwamba kuna randezvous mahali fulani. Yeye akashuhudie yeye mwenyewe. Itakuwa vibaya kama jamaa atajua kwamba ulijua muda mrefu na hukufanya lolote. Kwa upande mwingine mambo yakija julikana kwamba ni wewe ulitoa siri, own it. Kubali. Kama ni urafiki wa kweli utabaki. Lakini urafiki wa kinafiki haufai.

Siku moja nilikuwa ninampima mwenye mke kwa kumfake (yard stick) na hadithi ya kutunga kuhusu rafiki yangu mwingine huko kazini anayetembea na mke wa rafiki yake wakati mimi nafahamu jambo hilo, nikamuomba anipe ushauri nifanye nini kuhusu hilo, he, yeye alinionya ninyamaze kimya kabisa maana kitakachotokea juu yao nitakuwa ninahusika nacho, akasema "mimi nikijua kuwa rafiki yangu anakula mke wangu nayonga kabisa kwa mikono yangu" he, nilivyosikia vile nikaufyata kabisa mkia nikanyamaza kimya nina mwaka sasa.
 
Kwanini alikuambia? ana nia gani?

ni kama nilimfumania akitoka guest, nami nilionyesha kama nimekerwa na kitendo kile nami nikatishia kwenda kusema kwa jamaa ndiyo akasema balaa lake ukisema litakuwa kubwa maana jamaa ataniminya hadi niseme tu, anasema wamekuwa wakikutana na jamaa yule kwenye guest ile kwa muda mrefu hivyo jamaa angetumia ujanja na pesa zake kwa wahudumu wa guest kuujua undani wa jambo hilo, aliona bora anieleze mimi ili nami niuone umuhimu wa kuificha siri ile kwa manufaa ya urafiki wetu. Baada ya pale tukawa tunataniana na shemeji na kuzidi kunipa mbina za namna wanavyofanikisha kukutana na jamaa yetu muovu na kukiri kuwa amekuwa kama mume wake sasa maana huwa anakutana naye kimapenzi mara nyingi kuliko hata mume wake mwenyewe wa ndoa, bahati mbaya uovu huu hata baadhi ya ndugu zake yule mwanamke wanaufahamu kwakuwa siku nyingine anaaga kwenda mkoani kwao akisema anakwenda kukaa wiki moja lakini yeye anafika kwao mbeya na kukaa siku mbili tu na kuwahi kurudi na kufikia guest hiyo kwa siku zilizobaki kabla hayaripoti kwa mume wake kuwa ndo kwanza anarudi kutoka mkoani siku hiyo kumbe alikuwa hapa hapa jijini akila uroda na rafiki yetu.
 
Kaka nimewahi ku-experience hiyo hali. Ninachoweza kushauri ni kujiepusha sana na kujaribu kurekebisha hiyo kitu itakuwa na madhara makubwa, maana mambo ya mahusiano yana changamoto sana na hawatakuelewa. All you can do ni kuweka umbali wa kutosha na hao ndugu. nature itafanya kazi
 
ni na mashaka na ukweli wa huu uzi, sekondari kisha jeshini,chuo kikuu kisha tumeona afu watoto duh,jkt ya juzi tu haya yote mmeyatimiza vp?

kakwambia kaenda JKT iliyoanza juzijuzi?? kwa kukufahamisha tu, ni kuwa JKT kwa mujibu wa sheria ilikuwepo toka zamani sema hapo kati kutokana na hali ngumu ya uchumi ikasimama...ndo wameirudisha tena
 
Mwambie ukweli tu. Cha muhimu tu hakikisha hilo jambo umelithibitisha mwenyewe na sio habari ya kuambiwa/kusikia tu. Huyo anayekwambia hujui ana motive gani kwa hivyo inaweza isiwe kweli....maana hainiingii akilini mke wa mtu akwambie anachepuka huku akijua wewe ni rafiki wa mumewe.
 
Hawa watoto wa enz za kikwete hata ukiwaambia surual za modo zilikuwepo kabla na watu walivaa sana watakubishia, sasa wakisikia JKK/JESHI wanajua imeanza 2013 tu.

Mkuu . Mi kuna kijana mmoja alinibishia hizi nyimbo za zilipendwa. kuna wimbo Fulani nadhani Koro korola, uliimbwaga km sikosei miaka ya 60 Enzi zetu hiyo mimbo likuwa Zilipendwa. Sasa wajanja wakaja kuzirudia na zikawa zinapendwa. Sasa siku moja ukaimbwa huyo kijana akasema kaimba vizuri kweli. nikamwambia hizhi nyimbo ni za zamani jamani kijana alibisha na kutaja hiyo bendi iliyozirudia nyimbo hizo ndio zao na ni nyimbo za karibuni tu!
 
Siku moja nilikuwa ninampima mwenye mke kwa kumfake (yard stick) na hadithi ya kutunga kuhusu rafiki yangu mwingine huko kazini anayetembea na mke wa rafiki yake wakati mimi nafahamu jambo hilo, nikamuomba anipe ushauri nifanye nini kuhusu hilo, he, yeye alinionya ninyamaze kimya kabisa maana kitakachotokea juu yao nitakuwa ninahusika nacho, akasema "mimi nikijua kuwa rafiki yangu anakula mke wangu nayonga kabisa kwa mikono yangu" he, nilivyosikia vile nikaufyata kabisa mkia nikanyamaza kimya nina mwaka sasa.

ni kama nilimfumania akitoka guest, nami nilionyesha kama nimekerwa na kitendo kile nami nikatishia kwenda kusema kwa jamaa ndiyo akasema balaa lake ukisema litakuwa kubwa maana jamaa ataniminya hadi niseme tu, anasema wamekuwa wakikutana na jamaa yule kwenye guest ile kwa muda mrefu hivyo jamaa angetumia ujanja na pesa zake kwa wahudumu wa guest kuujua undani wa jambo hilo, aliona bora anieleze mimi ili nami niuone umuhimu wa kuificha siri ile kwa manufaa ya urafiki wetu. Baada ya pale tukawa tunataniana na shemeji na kuzidi kunipa mbina za namna wanavyofanikisha kukutana na jamaa yetu muovu na kukiri kuwa amekuwa kama mume wake sasa maana huwa anakutana naye kimapenzi mara nyingi kuliko hata mume wake mwenyewe wa ndoa, bahati mbaya uovu huu hata baadhi ya ndugu zake yule mwanamke wanaufahamu kwakuwa siku nyingine anaaga kwenda mkoani kwao akisema anakwenda kukaa wiki moja lakini yeye anafika kwao mbeya na kukaa siku mbili tu na kuwahi kurudi na kufikia guest hiyo kwa siku zilizobaki kabla hayaripoti kwa mume wake kuwa ndo kwanza anarudi kutoka mkoani siku hiyo kumbe alikuwa hapa hapa jijini akila uroda na rafiki yetu.


Kwa hali hii we piga kimya tu mkuu, tena ikiwezekana jiepushe na huyo rafiki yako mzinzi. Naiona hatari iliyoko mbele yako siku ukisema jambo hili.
Hawa wanawake walioolewa halafu tena wanakubali kuwa michepuke usidhani hawahitaji ndoa zao, akikujua wewe ndo umelisanua utambeba kwa visasi, tena watakuwa kitu kimoja na huyo rafiki yako wahakikishe na wewe wamekukomesha kwa umbea wako, wenyewe wanaita hivyo
 
jeshini wapi, jkt iliyoanza juzi tu halafu chuo kikuu na sasa mmeoa na huku jamaa akiwa anachepuka na mke wa mwenzake kwa miaka mitano sasa! Ina maana mlioa kabla hamjafika o level? Au uliposema jeshini ulimaanisha nini?
kwa nijuavyo mm, hapo zamani watu walienda jeshini then chuo, hiyo system ikaachwa then imerudishwa tena miaka ya hivi karibuni, so u never know labda broo ni wa kitambo
 
Mleta uzi hebu fanya mambo yako na imani una majukumu mengi tu. Mengine unaona unaacha tu yapite, je huyo rafiki yako yeye hachapi nje maybe unafichiaga siri. Take it easy ni bora ajue mwenyewe kuliko kuhusika wewe.
 
Khaa!! Ndio uje kusikia huyo shemejio analipa kisasi kwa mumewe kwasababu mumewe anamla mkeo
 
Tuko marafiki watatu wa kiume wa karibu sana tangu shule ya sekondari, Jeshini hadi Chuo Kikuu, tumeoa na tuna watoto, lakini bahati mbaya rafiki yetu mmoja anatembea na mke wa rafiki yetu mmojawapo kwa zaidi ya miaka 5 sasa.

Mimi ninafahamu uovu huo lakini nashindwa kumtonya rafiki yetu mwenye mke kwa kuhofia kitakachotokea. Anayetembea na mke wa mwenzake hajui kama mimi ninajua.

Shemeji anajua kama mimi ninajua kwamba anatembea na rafiki yetu kwa kuniambia yeye mwenyewe, mwenye mke hajui kabisa kama hili linafanyika.
Sijui kama na mke wangu pia kasalimika kwa aina hii.

Nipeni mawazo nifanye nini kwenye hili

Kweli ndio utakuweka huru
 
Sio kosa lako ni kwa sababu ya hiki kizazi cha elimu ya mulugo tulichonacho,,,jkt ilikuwepo kitambo sana sio hii yakwenu ya kibongo flava
 
Back
Top Bottom