NASAKA MKE WANGU NASAKA MKE WANGUuuuuuuuu

NASAKA MKE WANGU NASAKA MKE WANGUuuuuuuuu

ulingoo.. mayoyo... ulingoo.. mayoyo... 2namuomba samito, aonyeshe maringo yake ya ulaya,.. bingiribingiri chomamoto...
afu kuna ule mchezo 2likuwa 2naulizwa unampenda nan, ukisema tu, unaskia, nilonge nisilonge... watu longaa... dah memoriez za long kinoumer
 
Watoto wangu eeh....mimi baba yenu.....eeeh, sina nguvu tena.....eeeh, za kuuwa simba.....
 
Bulicheka na mkewe eliza eliza .......................
 
Sijuiiii Sijuiiiiiii. Wa mwisho akamatwe......

Haaaa huu wa kioo ndio nimeuchanganya na huo nasaka mke wangu. Huu w aki ndio ulikuwa wa kuvutana. Au sio Jestina? Nishasahu Nasaka mchezo wa nasakam mke wangu scene ya mwisho nini kilitokea. kuna yeyote anakumbuka

tulikuwa tunasimama duara tumeshikana mikono, then mke wako anakaa ndani ya duara. Mwishoni ile...

huu mti gani...
wa mchongoma...
nikiukata...etc

then unazunguka, kisha unakata mti (aka ile mikono ilishikana) mkeo anatoka na kukimbia unamkimbiza hadi umkamate...kumbuka steringi hafi, lol
 
kuna ule wa...

tule tumbakishie baba, rule tumbakishie baba

atakayedondosha kijit, hicho kipigo chake, lol
 
nilipenda sanas mchezo wa baba na mama nikiwa na family friends duh kucheza chumbani na kuzima taa

ila tulikuwa hatufanyi kitu wala nyeg* zilikuwa haskuna kutufanya tuvunje unyumba it was fun

kukumbatiana na kuongea kibaba kimama na wadogo kuwa watoto

lol
 
tulikuwa tunasimama duara tumeshikana mikono, then mke wako anakaa ndani ya duara. Mwishoni ile...

huu mti gani...
wa mchongoma...
nikiukata...etc

then unazunguka, kisha unakata mti (aka ile mikono ilishikana) mkeo anatoka na kukimbia unamkimbiza hadi umkamate...kumbuka steringi hafi, lol

Hivi sasa hivi at age 5 ,6 watoto wancheza nini ?
 
mimi nimekuwa mkubwa
nimeshangazwa na ule wimbo wa ukuti ukuti....

kwa sababu kwenye ule wimbo wanasema tumpeleke mnazi mmoja...

enzi tupo watoto tulikuwa tunatumia hospitali ya mnazi mmoja na sikuona ajabu

leo tanzania nzima wanaujua ule wimbo but swali ni kwa nini wote tuliimba mnazi mmoja?????

Sababu ulianzia Dar
 
1) pipipi...pipiii...eeeeh kidedea..umekumbuka huu wimbo?
2) saa..saa..saa ya kwenda kwetu..kwaheri mwalimu kwaheri tutaonana...keshooo..!!
3) mwanambuzi me me amlilia *****...mwanambuzi me me amlilia *****,kamwambia kwea kwea milima na mawe..
4) aeiou...aeiou...hizi ni silabi kuu..tamka kwa sauti kuu silabi aeiou..
5) kiooo..kiooo..alikivunja nani..
KWENYE KUBAHATISHA
dodo dodo miti walio kawawa sindikiza urembo na wengine walegalega urembo watoka ni sasa wasasia ndelule panda mwana ndelule doo!.mia
 
KUSOMA
Leo tunasoma kitabu.Sote tunasoma
a e i o u.
Tunasoma
ba be bi bo bu
Tunasoma
Baba bibo beba
Tuemfurahi kusoma kitabu.
kitabu chetu ni kizuri.

SHAIRI
Tumeishi kwa elimu,
Elimu ya kizamani,
Elimu ile halamu,
maana ya kikoloni,
Imetuishia hamu,
kuiga ya ugenini,
Elimu yetu ya sasa,
Yawafaa wananchi,

Karudi baba mmoja,
Toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja,
Na kutetemeka mwili'
Watoto wake wakaja,
Ili kumtaka hali,
Akakata na kauli,
...mia
 
kuna mchezo tulikuwa tunaita KOMBOLELA...Mnajificha, halafu mmoja anatafuta wenzake, wa mwisho anawaokoa wenzake.
Nakumbuka mimi nlikuwa tukichezaga huo mchezo, nlikuwa naenda mbali kusalimia au unakuta nimetumwa.
Basi wananitafuta nije niwakomboe mpaka giza wanachoka. Kumbe mi nko mtaa wa pili.. It was soo funny!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom