nasafirisha parcel kati ya dar na zanzibar.

nasafirisha parcel kati ya dar na zanzibar.

unajua nini!!watu wanajifanya hawaelewi,mie sijesema siku tatu,nimesema maximum 3 days,inashuka zaidi ya hapo hata siku moja tu,inategemea...ndio nipo bandarini...na utaratibu mtu anaufuata bandarini zanzibar.

Ni pm tufanye kazi kama tutaenda sawa.

Ila mim huwa sitaki mzigo wangu ulale, nikituma napenda mtu aupate siku hiyo hiyo,
 
Kodi za bandarini zimekaaje wakuu, let say natoa mizigo from Zenji to Dar mfano set za TVs flat screen na mengine

cc: Zanzibar Spices Apologise lady Abdulwahid

Ngoja waje hao wajibu kama washawah kulipa kodi, mim zangu kama homeshopping center, napita pembeni kabisa.

Tra ni wasumbufu sana, hvo ni bora ukapata mtu wa pale ofisin akakusaidia ila vinginevyo unaweza kuta gharama uliyonunulia na kodi ni bora ukanunua huku.
 
Last edited by a moderator:
sio kila baharia anafanya kazi speed boat boss....
kuna majahazi,boom na meli za mizigo...mfano kama uko kwenye jahazi baharini na upepo hamna,utategemea kufika siku ngapi?

Kuhusu majahazi huko ndio nyumbani kabisaa.
Abiria tu wale wa kuzamia kwenye majahazi wanalipa elf 5,000
Sasa iweje parcel mtu alipe elf tano.
Na jahazi kwa huku Zanzibar sehem kuu ni Kisakasaka,Nungwi na Mkokotoni achilia mbali hizo sehem ndogondogo.
Na huko kote ni nje ya mji,sasa hadi mzigo umfikie mtu kaishatumia pesa kibaooo.

Halafu unavyosema majahazi,na boom hiki ni kitu kile kile unabadilisha lugha tu ya mtaani kuwa ya uhalisia.
Mtu akitoka Saadani mfano kwa jahazi kuja Zanzibar ni wastan wa nusu siku tu,na kama hali ya upepo mbaya Majahazi mengi yana mashine za kuboost na haizidi siku moja.Dar to Zanzibar haina mkondo mkali kama wa kutokea Tanga kwenda Pemba na Pemba kuja Zanzibar.

Nakushauri ungeweka wazi kwamba wewe utatumia njia zipi,maana kama ni majahazi almaarufu maboom basi lazima mtumaji mzigo aingie gharama kubwa sana zaidi ya hiyo kutokana na vituoa vya majahazi hayo vyote kuwa nje ya mji.
 
sifanyi kazi speed boat...

Sasa kama huafanyi kazi speed boat hakuna urahisi mtu wa ku risk wa kukupa mzigo siku tatu as maximum kumfikia mhusika.
kama ni siku tatu ni bora niende Shirika la Posta ambapo ni salama zaidi na bei rahisi kupita maelezo,ila watu tunaona usumbufu tu.
Angalau ungesema kwamba nasafirisha mizigo,kama tv,nk ili iwe rahisi kwako kupata wateja,maana kwenye speed boat inakuwa ghali kiasi angalua wewe ungeweka kama buku 10.Ila hata hivyo hayo majahazi kila siku yanaingia maji bado hatari ipo pale pale.
Niliwahi kupanda kutoka Kisakasaka,wote tulifika tumelowa.
 
Kodi za bandarini zimekaaje wakuu, let say natoa mizigo from Zenji to Dar mfano set za TVs flat screen na mengine

cc: Zanzibar Spices Apologise lady Abdulwahid

Kodi huwa hakuna kama una receipt ya kununua mzigo wako,na mara nyingi parcel hizi huwa ni kama za home use au kwa uchache wake na sio quantity kubwa.
Na mara nyingi wasafirishaji huwa wanautoa mzigo au kifurushi chako mpaka njee ya bandari,sasa wewe unachukua na kuondoka,la zaidi na TRA wanajuana wao.
Kwa ufupi TRA pale ni usanii tu,maana wewe ukipita hata na Deck ya tv hawakuzuii,ila kuna siku ukimkuta mwenye njaaa anasema hembu lete receipt ukimpa anazuga anakuachia,so hakuna mfumo rasmi pale.Ili ukwepe usumbufu kama ni msafirishaji,hakikisha unakuwa na receipt,cha kuchekesha hata recipt kama haina muhuri we unapita tuu.

So,mzigo kama Tv na home uses nyingine unapita muhim uwe na recipt na uwe mjanja,wanatabia ya kujaribu mtu pale.Unaweza kuona anakuambia lipia elf 20 ukikomaa hadi elf 5,sasa ndio ujue kwamba sio mfumo rasmi.
Ila ukimpa msafirishaji na ukimlipa gharama za upakizi na utoaji unakuwa unakwepa usumbufu maana wanajuana wao kwa wao
 
Huyu mleta post afebris

Tatizo kashindwa kujieleza,wewe ungesema kwamba unafanya kazi kwenye majahazi almaarufu maboom pale Malindi,nyuma ya Bwawani.

Sasa ungeleeza kuliangana na taratibu za kupakia na kushusha mzigo ndio unafanya kwamba siku tatu zitimie.Sasa hapa mtu angeweza kukuelewa kwamba upo kwenye position ipi.
Halafu pia lazima utofautishe bei za Speed boat na Majahazi,maana kwenye speed boat bei ni kama zako na mtu anaupata ndani ya masaa 3.Na zaidi ya hapo parcel yake inapata na AC ndani ya boat,aiseee raha tupu,inaona hadi Tv,na kubwa zaidi Parcel yake inapatanda boat moja na wazungu.
Ila kwenye jahazi pale Tv ni tanga la jahazi,Ac ni upepo wa shombo la Saradini.So,angalia bei

Jingine ni kwamba ingie kwenye kusafirisha mizigo ya kati,yaani kama Tv,fridge nk,ili iwe rahisi kushindana na watu wa speed boat ambapo kule ni ghali kiasi.Sasa wewe ungeshusha ungeweza kuweka mazingira mazuri zaidi kwako.
Maana hata hiyo elf 5,000 umeyosema ni kwamba hiyo ni yako tuu,na sio ya kulipia mambo mengine.Unakuta inaweza kufika hadi elf 15 hata kama ni Jahazi.

Ushauri:
Kama unasafirisha kutoka Zanzibar kuja Dar ni vizuri sio mbaya kwa jahazi pia,ila kama ni kutoka Dar kuja Zanzibar usijaribu hata mara moja.
Zanzibar inaingiza zaidi mizigo kutoka Dar kuja huku Zanzibar,ila Jahazi linaweza kurudia Dar likiwa tupu kabisaa kwakuwa mizigo ya kutoka huku kuja Dar demand haipo.Maana huku Zanzibar karibia 70% ya vyakula vyote vinatokea Tanzania Bara.
Kwahiyo ukipakia mzigo unaweza kufika ukiwa chapati kabisaa,maana jahazi hazina vya kushikia mzigo usizurure,maana tabia ya jahazi ni kufanya vitu vizurure kutokana na mawimbi
 
nabaki na cheka tu,wewe mzee mkorofi sana haha,mie sio baharia wa jahazi nmetoa mfano tu,bali wa meli za mizigo,na ninaposema siku 3,meli ya mzigo haisafiri kila siku,so kama mtu kakupa mzigo leo na meli inaondoka kesho,sasa huoni hapo itatumia siku ngapi?ila ratiba zinabadilika.....na kuhusu tv natuma pia....
 
We acha uhuni,Zanzibar Dar 3 days umeona wapi?
Mtuu unaagiza sim kutoka UK inachukua chini ya wiki.Itakuwa hapa hata kunguru wanavuka.

Yaani ulivyoweka siku 3 ndio umekimbiza wateja.

Mie kila wiki nasafirisha vimizigo hivyo kwa ndugu zangu waliopo Dar na ni only 2hrs na nusu mtu anapata mzigo wake.Unaenda Bandarini unampa Staff wa boat na wengine nijamaa zangu maana wengine tumekaa sana port.Ukimpa basi wakati huo huo unampigia sim mtu akapokee.Sasa kwa sie tunaokaa Buguruni ni masaa matatu tu mzigo unafika nyumbani.
We hata parcel ya Biriani ukiisafirisha inafika haijapoa

Kuhusu bei,hapo ni sawa,ndio bei za kawaida hizo.

badilisha suala la siku tatu,la sivyo wewe mwizi,mie sipendi saana kuremba.
Mkuu nakuomba pm tafadhali. Nina mazungumzo na wewe...
 
Mleta mada,

Ni vema pia ukashawishi wateja kwa kuelezea baadhi ya vitu ambavyo unadhani mtu atafaidika kwa kuagiza Zanzibar badala ya kununua dsm.

Sijafika zanzibar lakini natamani kujua vitu gani huko ni bei nafuu.
 
Mleta mada,

Ni vema pia ukashawishi wateja kwa kuelezea baadhi ya vitu ambavyo unadhani mtu atafaidika kwa kuagiza Zanzibar badala ya kununua dsm.

Sijafika zanzibar lakini natamani kujua vitu gani huko ni bei nafuu.

zanzibar kwa sasa almost kila kitu kimezidiwa na dar..
 
Mleta mada,

Ni vema pia ukashawishi wateja kwa kuelezea baadhi ya vitu ambavyo unadhani mtu atafaidika kwa kuagiza Zanzibar badala ya kununua dsm.

Sijafika zanzibar lakini natamani kujua vitu gani huko ni bei nafuu.

karibu zanzibar mkuu,kama una pesa unaweza ukaoa asubuhi na kurudi na mkeo jioni dar 🙂
 
zanzibar kwa sasa almost kila kitu kimezidiwa na dar..

Vitu vya Electronic na Magari bado Zanzibar ni rahisi mno.
Ila sema tu watu wengi wakija Zanzibar wanakuwa ni wa kununua na kuondoka tofauti nasie ambao tuna nasaba pande zote mbili.
Maana kuna sehem unajua kabisa kwamba gari unapata kwa bei gani,na maduka gani au godown zipi mzigo wa vitu vya electronics ni rahisi.Sasa hii kwa mgeni lazima itakusumbua na utaenda kwenye maduka yaliyozoeleka.na licha ya hivyo bado vipo bei ya chini.

Faida nyingine kubwa kwa Zanzibar ni uaminifu wa hali ya juu kwa bidhaa husika.Hakuna ujanja ujanja kama Dar.Maana kama kitu kina tatizo mtu anakuambia kabisaa.Imani zaidi bado ipo

Ila Dar unaweza kununua bidhaa hapo hapo ukabadilishiwa.Wengine unanunua Gari ukisema unaenda kumalizia pesa kesho unakitu Radio,rims,vyote vimebadilishwa na kuwekwa vya hali ya chini,na wengine hufikia mpaka kubadilisha Engine ya Gari wakiona kama sio mzoefu wa magari na kukusukumizia vimeo.Kwa Dar kuifikia Zanzibar kazi sana,maana kila siku wafanyabiashara wa Bongo wanakuwa wasaniii sanaa.
 
nabaki na cheka tu,wewe mzee mkorofi sana haha,mie sio baharia wa jahazi nmetoa mfano tu,bali wa meli za mizigo,na ninaposema siku 3,meli ya mzigo haisafiri kila siku,so kama mtu kakupa mzigo leo na meli inaondoka kesho,sasa huoni hapo itatumia siku ngapi?ila ratiba zinabadilika.....na kuhusu tv natuma pia....

Hahaha,kumbe unajua kujieleza
Utakuwa upo kwa Batashi wewe au kwenye Sealink,ni kweli zile meli za mizigo zinakuwa na ratiba hasa kuangalia na wingi wa mzigo.
Ila mara nyingi ni siku mbili labda kuwe na standby order imeyofanya wasubirie.Kama ni kwenye Sealink pale kwa Bakhressa,hapa hakuna jinsi,maana hili hadi liunganishe Pemba ndio lije Unguja na kwenda Dar,hapa lazima utoe kweli siku tatu za kusubiria mzunguuko wake.
Najua unaogopa kutaka ni Meli gani upo,maana ni fitna,najua hata kwenye AZAM hawaruhusiwi kuchukua vifurushi ila watoto wa mjini wanapiga hela,mie kwangu naona poa saana,maana wananisaidia sana hata Documents zangu za gari napitia kwao.
 
Hivi yule Zidane bado yupo kwenye nyanja za Bandarini hapo.... Jamaa Alikuwa Muaminifu sana miaka kama sita au saba iliyopita...
 
Hahaha,kumbe unajua kujieleza
Utakuwa upo kwa Batashi wewe au kwenye Sealink,ni kweli zile meli za mizigo zinakuwa na ratiba hasa kuangalia na wingi wa mzigo.
Ila mara nyingi ni siku mbili labda kuwe na standby order imeyofanya wasubirie.Kama ni kwenye Sealink pale kwa Bakhressa,hapa hakuna jinsi,maana hili hadi liunganishe Pemba ndio lije Unguja na kwenda Dar,hapa lazima utoe kweli siku tatu za kusubiria mzunguuko wake.
Najua unaogopa kutaka ni Meli gani upo,maana ni fitna,najua hata kwenye AZAM hawaruhusiwi kuchukua vifurushi ila watoto wa mjini wanapiga hela,mie kwangu naona poa saana,maana wananisaidia sana hata Documents zangu za gari napitia kwao.

hahaha nashkuru umenifahamu...
 
Hivi yule Zidane bado yupo kwenye nyanja za Bandarini hapo.... Jamaa Alikuwa Muaminifu sana miaka kama sita au saba iliyopita...

Mkuu ngoja nitampigia simu Materazi kumuuliza kama jamaa bado yupo kwenye game kisha nitakujulisha
 
Zanzibar Spices nahitaji birika la kuchemshia maji uninunulie na kunitumia kwa huyu jamaa nipm namba yako nikurushie pesa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom