Kwa kuanza kabisa Mimi ni mwalimu wa primary ajira mpya kwa hii intake ya Desemba!
Nakiri wazi kuwa tangu nimalize chuo mwaka 2016 ndo nimebahatika kupata ajira mwaka jana lakini Hali yangu kimwili, na kiakili kwa Sasa haijakaa sawa kutokana na changamoto ninazopitia.
Kwanza naomba niweke wazi kuwa tangu mwezi desemba nipo kituoni (kazini) na sijawahi pewa mshahara hata mmoja maana kila nikifuatilia halmashauri naambiwa kuwa nisubiri uhakiki wa vyeti bado unaendelea na huu mwezi sina hakika ya kulipwa yaani hapa nilipo nadaiwa na watu hata kupokea simu naogopa, na mbaya zaidi kila siku naishi kwa mikopo na siku nikikosa kabisa nalala njaa kabisa, nilijaribu kumueleza mkuu wa shule lakini katika bajeti yao walinipa sh 10000 tu wakidai kuwa chalk na vifaa vingine vya shule havijanunuliwa na wakizidisha bajeti itawalemea.
Yaani sikuwahi jua kuwa mtu unaweza ikafika hatua ukaishi kwa mateso hivi.
Yaani inafika kipindi napika ugali naweka chumvi kisa sina mboga.
Muda mwingine nakoroga uji natia chumvi.
Huku kwetu maji tunanunua siku nikikosa hela ya kununulia maji nanawa maji niliyooshea vyombo.
Yaani Mambo mengi magumu ambayo nayapitia na mpaka saivi nimedhoofu mwili hasa, sina amani kabisa yaani.
Na kingine nikiweke wazi na hii shida sijui nimeirithi wapi maana ni Toka utoto mfano kama hapa nateseka Sana lakini kutoka hapa na kwenda kwa majirani nikaombe chakula nashindwa kabisa maana naweza kaa hata siku mbili sijaonja kitu lakini kuomba chakula kwa mtu nashindwa kabisa.
Na saivi hakuna mtu hata wa kumkopa maana asilimia kubwa nimewakopa na wengine wananidai maana nikiwaambia bado sijaanza kupokea mshahara wanahisi nawadanganya.
Ila nateseka sana Tena Sana kibaya zaidi naishi kwenye nyumba ya kupanga ambapo mwenye nyumba ananidai kodi Toka januari na analalamika nimlipe Kodi yake au nihame.
Naombeni ushauri jamani maana wazo lililopo kichwani ni kutoenda shule Hadi mshahara utakapo ingia ili hizi siku nitumie hata kufanya vibarua. Je, naweza achishwa kazi kwa kosa la kutoenda shule.
Nakiri wazi kuwa tangu nimalize chuo mwaka 2016 ndo nimebahatika kupata ajira mwaka jana lakini Hali yangu kimwili, na kiakili kwa Sasa haijakaa sawa kutokana na changamoto ninazopitia.
Kwanza naomba niweke wazi kuwa tangu mwezi desemba nipo kituoni (kazini) na sijawahi pewa mshahara hata mmoja maana kila nikifuatilia halmashauri naambiwa kuwa nisubiri uhakiki wa vyeti bado unaendelea na huu mwezi sina hakika ya kulipwa yaani hapa nilipo nadaiwa na watu hata kupokea simu naogopa, na mbaya zaidi kila siku naishi kwa mikopo na siku nikikosa kabisa nalala njaa kabisa, nilijaribu kumueleza mkuu wa shule lakini katika bajeti yao walinipa sh 10000 tu wakidai kuwa chalk na vifaa vingine vya shule havijanunuliwa na wakizidisha bajeti itawalemea.
Yaani sikuwahi jua kuwa mtu unaweza ikafika hatua ukaishi kwa mateso hivi.
Yaani inafika kipindi napika ugali naweka chumvi kisa sina mboga.
Muda mwingine nakoroga uji natia chumvi.
Huku kwetu maji tunanunua siku nikikosa hela ya kununulia maji nanawa maji niliyooshea vyombo.
Yaani Mambo mengi magumu ambayo nayapitia na mpaka saivi nimedhoofu mwili hasa, sina amani kabisa yaani.
Na kingine nikiweke wazi na hii shida sijui nimeirithi wapi maana ni Toka utoto mfano kama hapa nateseka Sana lakini kutoka hapa na kwenda kwa majirani nikaombe chakula nashindwa kabisa maana naweza kaa hata siku mbili sijaonja kitu lakini kuomba chakula kwa mtu nashindwa kabisa.
Na saivi hakuna mtu hata wa kumkopa maana asilimia kubwa nimewakopa na wengine wananidai maana nikiwaambia bado sijaanza kupokea mshahara wanahisi nawadanganya.
Ila nateseka sana Tena Sana kibaya zaidi naishi kwenye nyumba ya kupanga ambapo mwenye nyumba ananidai kodi Toka januari na analalamika nimlipe Kodi yake au nihame.
Naombeni ushauri jamani maana wazo lililopo kichwani ni kutoenda shule Hadi mshahara utakapo ingia ili hizi siku nitumie hata kufanya vibarua. Je, naweza achishwa kazi kwa kosa la kutoenda shule.