Napinga sehemu ya malipo ya Lema...

Napinga sehemu ya malipo ya Lema...

VIKWAZO

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2011
Posts
1,900
Reaction score
581
Kwanza salamu, pia niwatakie heri ya Christmas na mwaka mpya.

Hoja ya msingi ni
MALIPO YA LEMA YANAONYESHA UDHAIFU WA MFUMO WETU.

Lema atalipwa milion 85 Tsh/= kama malimbikizo kwa kusimamishwa baada ya kusimamishwa ubunge,
( kwa mchanganuo zaidi soma hapa
Lema kuzoa Sh85 Milioni - Siasa - mwananchi.co.tz )
kama mwananchi nina tatizo na Lema kulipwa hiyo pesa, sioni Value for money kwa sisi kuwa na mfumo dhaifu kiasi hicho.

Tatizo nililonalo Lema kulipwa hiyo pesa ni maeneo yafuatayo:

1.) Milion 20 za mafuta kama Mbunge, Lema aliposimamishwa ubunge shughuli zake zilikoma, hivyo matumizi ya mafuta kwa shughuli za kibunge yalikoma pia!!! kwangu mimi kumlipa Mbunge Milion 20 za mafuta bila kuwa kazini au kufanya kazi ni kudhurumu wananchi, huu ni mfumo onevu, hiyo pesa haipashwi kulipwa,
kwa maelezo zaidi ni kwamba Lema atarudishiwa ghalama za kesi, ni ghalama zipi hizo? hakuna nauli alizokuwa anatumia? na kama ndio balance ipo itakuwaje tukimlipa tena kama umma pesa ya mafuta?
lakini Je Lema kwa wakati huo alikuwa anafanya shughuli zipi? sio M4C ( i embrace M4C but TAIFA kwanza) huko akulipwa chochote?

2.) posho ya jimbo Sh40 milioni ....... jimbo lipi hali kazi ilisimamishwa? jimbo la Arusha alikuwa na mbunge kwa wakati wote wa kesi? lema akufanya shughuli za kibunge jimboni mwake.
Lakini pia kwa kwenda mbali ni kwamba Lema alikuwa na shughuli maalumu ya chama yaani M4C ( no problems) lakini je hapa kuna tofauti gani na wale wafanyakazi hewa? mtu ayupo kwenye kituo cha kazi analipwa tu? hivi sisi tunalipa majina au shughuli/kazi ya mtu? where is the value for my TAX?

3.) Posho nyingine Sh6.6 milioni Kwa kazi ipi analipwa posho? ubunge ulikoma nimeshaeleza hapo juu, ofisi ya mbunge haikuwa na kazi tena kwa kukosa mbunge, na kama ilikuwepo na ina fanya kazi vipi amri ya mahakama kusimamisha ubunge wa Lema, kwa misingi hiyo nina amini hakukuwa na shughuli ya sisi kama taifa kulipa posho.

<<<<<<
Nakubaliana kwamba Lema alipwe malimbikizo ya mshahara wake yanafikia Sh18.4 milion, hii ni haki pekee kwa Lema, sikupaliana kwamba kama mtu umesimamishwa wazifa wako basi umma uendelee kukulipa pesa bila kuutumikia.

CHOMBEZO
Je Kwa misingi hiyo kama nikiwa bosi sehemu nikasimamishwa kazi, wakatia nikiwa kazini nilikuwa na allowance/posho ya mafuta, uchunguzi ukiisha nikarudi kazini nitapewa mafuta ya siku zote ambazo nilikuwa nimesimamishwa? rejea milion 20 za mafuta ya lema.
Wabunge wanalipwa hela ya mafuta (sio kwa matumizi mengine ni ya mafuta jimboni) lakini hiyo inaweza kubadilika na wabunge wakapewa mafuta na sio pesa, je ingekuwa hivyo ina maana leo LEMA angekwenda shell na kuchota mafuta ya milioni 20?
Je ningekuwa kiongozi nikasimamishwa kazi lakini nilikuwa na posho za kuendeshe ofisi, nikirusi nitalipwa posho za kuendesha ofisi iliyofungwa? ili nizifanyie kazi ipi? milioni 40 za jimbo

HITIMISHO:
Hoja yangu ni tuwe na kanuni zenye macho, zinazothamini kodi yetu, malipo lazima yenye thamani ya kazi, malipo holela ni hatari kwa taifa, napinda haya malipo regardless nani anapewa, msingi ni kuwa na taifa imala lenye uchumi unaonufaisha wote.

Kama kuna sheria zinatoa mwanya huu zifutwe mara moja ili kuongeza thamani ya pesa yetu katika matumizi (VALUE FOR MONEY)

NUKUU
quote_icon.png
By Kitila Mkumbo Moja ya matatizo yetu kama nchi na wananchi ni kuchukia watu wanaofikiri tofauti.

Tumezoea mazoea; ukiona mtu anaenda tofauti na mazoea tunaanza kumpa majina kibao: kanunuliwa, msaliti, anajipendekeza, hana ushirikiano, n.k.. Lazima tubadilike na kujua kwamba binadamu tu tofauti kimwili, kiakili na kila kitu.

Ili tutoke hapa tulipo lazima turuhusu akili zifikirii sawasawa na tena tuhangaike kufikiri kitofautitofauti. Kama tunataka kila mtu afikiri kama sisi ni kuendeleza utamaduni wa kutumia akili za kuazima.

@VIKWAZO (jina hapo nimebadilisha) ni miongoni mwa watu wachache hapa nchi aliyeamua kujipambanua na kuamua kufikiri kitofautitofauti. "Kosa" lake ni kwamba ameamua kuacha kufanya mambo kwa mazoea na ameamua kuhangaika kufikiri kitofautitofauti. @VIKWAZO (Nimedadilsha jina tena) analaaniwa kwa kudiriki kwake kuhangaika kufikiri na kuachana na mazoea. Atabambikizwa majina yote ya ovyo kama usaliti, kujipendekeza, n.k. Tunamtia moyo aendelee kuhangaika kufikiri, wapo watakaomuelewa.



 
Downs mbona inalipwa hujapinga? ni stahiki zake ni lazima alipwe kwa mujibu wa sheria, Lema hajatunga hizo sheria, unashindwa kuwa na Uchungu na Mabilioni ambayo Downs italipwa unaenda kudai milioni 80.
 
Mbona kawaida tu hiyo emu kajaribu kuulizia mfanyakazi wa TRA au bandar akisimamishwa akirudi inakuwaje kama ujaambiwa wanalipwa mpaka ela zao za chai za miaka yote waliokua benchi
 
Mbona kawaida tu hiyo emu kajaribu kuulizia mfanyakazi wa TRA au bandar akisimamishwa akirudi inakuwaje kama ujaambiwa wanalipwa mpaka ela zao za chai za miaka yote waliokua benchi

Ndicho ninachopinga, malipo kama haya hapana kama yapo yaondolewe, watu walipwe mishahara yao tu
 
Downs mbona inalipwa hujapinga? ni stahiki zake ni lazima alipwe kwa mujibu wa sheria, Lema hajatunga hizo sheria, unashindwa kuwa na Uchungu na Mabilioni ambayo Downs italipwa unaenda kudai milioni 80.

Kwa hiyo hii ni kulipa kisasi zidi ya mtoa kodi yaani mwananchi? kwa maana nyingine chukua chako mapema au?
hapa naongelea TAIFA bora, weka siasa pembeni
 
unfortunately sheria zetu ndivyo zilivyo.... Kwa sasa hakuna tunachoweza kubadilisha ila tuhakikishe tunapa katiba mpya SAFI imbayo tutabainisha mambo yote yenye utata kwa sasa.....

Swali la kizushi... Mheshimiwa wa Monduli bado anapokea posho ya "Waziri Mkuu MSTAAFU?
 
Bila shaka Bunge lina taratibu sheria na kanuni zake zakuwalipa wabunge wanaorudishwa bungeni kwa mazingira kama ya Mh Lema.
Lema hatakuwa mbunge wa kwanza kulipwa hivyo, kama unavyosema endapo kuna mapungufu katika sheria husika basi marekebisho hayana budi yafanyike.
Hapa swali ninalouliza mkuu kama Lema hapashwi kulipwa marupurupu uliyohainisha hapo juu kwa vile hakuwa mbunge kipindi hicho kwa nini unataka alipwe mshahara wa siku ambazo hakuwa mbunge,nilifikiri kigezo ulichotumia kutaka asilipwe stahiki nyingine kwa nini kisitumike pia kwenye mshahara tofauti hiko wapi?.
 
unfortunately sheria zetu ndivyo zilivyo.... Kwa sasa hakuna tunachoweza kubadilisha ila tuhakikishe tunapa katiba mpya SAFI imbayo tutabainisha mambo yote yenye utata kwa sasa.....

Swali la kizushi... Mheshimiwa wa Monduli bado anapokea posho ya "Waziri Mkuu MSTAAFU?
Kwa sasa LEMA anaweza kukikataa hiyo pesa chafu, kisha kuweka shinikizo ili tuwe na sheria bora, hiyo ni kazi yake ya msingi kama mbunge,
Bora wewe umeliona ili suhala kwa mapana yake
 
Downs mbona inalipwa hujapinga? ni stahiki zake ni lazima alipwe kwa mujibu wa sheria, Lema hajatunga hizo sheria, unashindwa kuwa na Uchungu na Mabilioni ambayo Downs italipwa unaenda kudai milioni 80.

Kwa hiyo Lema kapata Excuse kuchukuwa hizo pesa ambazo ajazifanyia kazi.
 
Bila shaka Bunge lina taratibu sheria na kanuni zake zakuwalipa wabunge wanaorudishwa bungeni kwa mazingira kama ya Mh Lema.
Lema hatakuwa mbunge wa kwanza kulipwa hivyo, kama unavyosema endapo kuna mapungufu katika sheria husika basi marekebisho hayana budi yafanyike.
Hapa swali ninalouliza mkuu kama Lema hapashwi kulipwa marupurupu uliyohainisha hapo juu kwa vile hakuwa mbunge kipindi hicho kwa nini unataka alipwe mshahara wa siku ambazo hakuwa mbunge,nilifikiri kigezo ulichotumia kutaka asilipwe stahiki nyingine kwa nini kisitumike pia kwenye mshahara tofauti hiko wapi?.
Sawa lakini na sisi wananchi tuna haki ya kuhoji jinsi pesa yetu ya kodi inavyotumika, kumbuka LEMA ni sehemu tu ya wanaolipwa haya malipo yasiyo na msingi [ hapa naongelea posho na sio mshahara wake]
 
Kwa hiyo Lema kapata Excuse kuchukuwa hizo pesa ambazo ajazifanyia kazi.

Kuna watu wanaleta utetezi kisiasa kwa kuzani kila mtu mwanasiasa, sasa hapa watakwamba hata hoja ya kukataa posho za wabunge itakwama, mantiki kuwe na malipo ya haki kama vile mishahara na sio posho wakati ujafanya kazi.

Posho kama ya mafuta wakati hakufanyakazi kwa miezi 8, sio sahihi
 
Sasa siku zote ulikuwa wapi kupinga sheria ya kulipa haya malimbikizi?kwann uanze kupinga ulipwaji wa Lema badala ya kuanza kupinga sheria iliyopitishwa na bunge lenye wabunge wengi wa ccm ili kuhalalisha ulipwaji huu wa mamilioni ya shilingi??HOJA YAKO NI NZURI ILA IMEKAA KISHABIKI
 
Kwa hiyo Lema kapata Excuse kuchukuwa hizo pesa ambazo ajazifanyia kazi.

K amefanya kazi wewe huoni M4C ailizo kuwa akifanya? niambie hawa wafuatao wana fanya nini Bungeni, Wasira kazi kulala, Mohamed E, na wengineo,

Bora Lema alikuwa akipiga M4C, kuliko hao wanaolala Bungeni na wengine kugeuka Mabubu huko
 
Kuna watu wanaleta utetezi kisiasa kwa kuzani kila mtu mwanasiasa, sasa hapa watakwamba hata hoja ya kukataa posho za wabunge itakwama, mantiki kuwe na malipo ya haki kama vile mishahara na sio posho wakati ujafanya kazi.

Posho kama ya mafuta wakati hakufanyakazi kwa miezi 8, sio sahihi

Wewe umeona kwa Lema? Hao wanaoumwa mwaka mzima mbona wanalipwa? Wabunge wangapi huwa hawaonekani Bungeni na wanalipwa? Muhimu ni kuwauliza waliotunga sheria na si kumuuliza Lema, Make Magamba hamfikilii kabla ya kuongea, Unaleta Mambo ya Nepi na Kadi wakati yeye Anamiliki ya CCJ
 
.
..umetumwaaaaaaaaaaaaaa...nenda LUMUMBA kama huna ajira...kukusaidia masika imeanza kalime..kilimo ni uti wa mgongo..chukua na hii ya maabara..kilimo moja!!!
Leo tunaitwa wakulima tukihoji matumizi ya pesa yetu sisi wananchi sio?
 
Wewe umeona kwa Lema? Hao wanaoumwa mwaka mzima mbona wanalipwa? Wabunge wangapi huwa hawaonekani Bungeni na wanalipwa? Muhimu ni kuwauliza waliotunga sheria na si kumuuliza Lema, Make Magamba hamfikilii kabla ya kuongea, Unaleta Mambo ya Nepi na Kadi wakati yeye Anamiliki ya CCJ

Kasome hitimiosho nililoweka, lema sio objective yangu, ila ni sheria mbovu, kuna sehemu umeona nimeandika kwamba Lema kateka Bunge na kudai malimbikizo yake.

Anyway nimeona kwa lema na sikubalini na malipo ya ovyo kama haya kwa mtu yeyote.
Tunawezaje kuipinga ccm kwa matumizi mabovu lakini tunashangilia inapokuja kwamba yale matumizi mabovu tunalipwa wapiganaji?

HELA NI NZITO kumbe
 
Kasome hitimiosho nililoweka, lema sio objective yangu, ila ni sheria mbovu, kuna sehemu umeona nimeandika kwamba Lema kateka Bunge na kudai malimbikizo yake.

Anyway nimeona kwa lema na sikubalini na malipo ya ovyo kama haya kwa mtu yeyote.
Tunawezaje kuipinga ccm kwa matumizi mabovu lakini tunashangilia inapokuja kwamba yale matumizi mabovu tunalipwa wapiganaji?

HELA NI NZITO kumbe

Mkuu Hizo ni Pesa Ndogo sana na alitakiwa apewe zaidi ya Hizo,alitakiwa apewe Bajeti nzima ya Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana, make ni waizara inayo tengewe Pesa bila kuwa na Kazi ya Kufanya, CCM wakiongozwa na Mkuu wao ndo wanatumia pesa bila jasho, Kwa sasa Mkuru yuko Serengeti ana Consume his own Service, Wachumi wananisaidia hapo, Kile kitendo cha Producer kuwa ndo mnunuzi mkuu wa Product/Service yake mwenyewe ndo anacho fanya Mkuru kule Serengeti, Inapaswa uanzia huko kuhoji na si kuhoji Milino 80

 
Mkuu Hizo ni Pesa Ndogo sana na alitakiwa apewe zaidi ya Hizo,alitakiwa apewe Bajeti nzima ya Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana, make ni waizara inayo tengewe Pesa bila kuwa na Kazi ya Kufanya, CCM wakiongozwa na Mkuu wao ndo wanatumia pesa bila jasho, Kwa sasa Mkuru yuko Serengeti ana Consume his own Service, Wachumi wananisaidia hapo, Kile kitendo cha Producer kuwa ndo mnunuzi mkuu wa Product/Service yake mwenyewe ndo anacho fanya Mkuru kule Serengeti, Inapaswa uanzia huko kuhoji na si kuhoji Milino 80

zinatoka kwa watu wasio na pesa, hata ccm nao wanapotumbua wanasema ni pesa ndogo kwa VIJISENT ukumsikia?
lazima tuwe na sheria/kanuni makini
 
Back
Top Bottom