UmkhontoweSizwe
Platinum Member
- Dec 19, 2008
- 8,530
- 7,735
Hoja yangu inalenga hasa kwa maeneo ya mjini ambako ndo kuna kizungumkuti katika uendeshaji wa halmashauri za miji.
Pendekezo langu ni kwamba tupunguze maeneo ya halmashauri za miji.
Mfano: 1. Badala ya Jiji kama Dar kuwa halmshauri za miji tatu tu (Ilala, Temeke na Kinondoni), kuwe na serikali za miji nyingi. Iwe ni miji inayojitegemea na kujiendesha yenyewe.
Nionavyo: Dar sasa hivi ingekuwa na Serikali za miji siyo chini ya 6, (eg. Kigamboni, Mbagala, City Center, Magomeni, Ubungo/Kimara, Sinza/Mlimani/Mikocheni, Kinondoni/Mwananyamala/Msasani, Kipawa/Ukonga/Yombo, nk – wengine mnaweza kunisaidia mgawanyo). Hii inatokana na kupanuka kwa eneo la mji na ongezeko la idadi ya watu.
2. Jiji la Mwanza (2nd largest) lingekuwa na miji km 4 hivi, city center/mabatini, Buzuruga/Nyakato/Mahina, Igoma, Pasiansi/Nyamanoro/Bwiru, Igogo/Butimba, nk.
Faida:
1. Itazipunguzia halmashauri za wilaya ukubwa wa maeneo ya kuhudumia na mzigo wa huduma yenyewe.
2. Tutasogeza huduma karibu zaidi na wananchi, tofauti na ilivyo sasa ambapo halmashauri za miji zinahudumia maeneo makubwa na matokeo yake ufanisi unakuwa kiduchu sana, kama siyo hakuna kabisa.
3. Tutasogeza kwa wananchi vikao vya maaamuzi. Wananchi watachagua viongozi wao wa miji na kufanya maamuzi yatakayoendana na mazingira na utashi wao. Viongozi wataochaguliwa watawajibika kwa wananchi moja kwa moja.
4. Tuasogeza karibu zaidi kwa wananchi upangaji, utekelezaji na usimamizi wa mipango ya maendeleo, tofauti na sasa hivi ambapo uamuzi unafanywa wilayani na wananchi kubaki km watazamaji tu.
5. Tutaongeza ajira. Badala ya kuhudumiwa na kundi dogo la watu wa wilayani, kila mji utakaoanzishwa utaajiri wataalam wake, kwa hiyo watu wengi wataajiriwa.
6. Itasaidia kuweka suala la maendeleo mikononi mwa wananchi wenyewe badala ya kutegemea serikali kuu.
7. Kwa kuwa mwenye kisu kikali ndiye hula nyama, miji itakayoboresha huduma kwa wananchi ndo itakayovutia uwekezaji zaidi na hivyo kupata makusanyo zaidi ya kodi na hivyo kuwa na mapato zaidi.
Hili ni wazo ghafi. Wenajamvi mnasemaje? Na wataalam wa mipango miji mnasemaje?
Jumapili njema.
Pendekezo langu ni kwamba tupunguze maeneo ya halmashauri za miji.
Mfano: 1. Badala ya Jiji kama Dar kuwa halmshauri za miji tatu tu (Ilala, Temeke na Kinondoni), kuwe na serikali za miji nyingi. Iwe ni miji inayojitegemea na kujiendesha yenyewe.
Nionavyo: Dar sasa hivi ingekuwa na Serikali za miji siyo chini ya 6, (eg. Kigamboni, Mbagala, City Center, Magomeni, Ubungo/Kimara, Sinza/Mlimani/Mikocheni, Kinondoni/Mwananyamala/Msasani, Kipawa/Ukonga/Yombo, nk – wengine mnaweza kunisaidia mgawanyo). Hii inatokana na kupanuka kwa eneo la mji na ongezeko la idadi ya watu.
2. Jiji la Mwanza (2nd largest) lingekuwa na miji km 4 hivi, city center/mabatini, Buzuruga/Nyakato/Mahina, Igoma, Pasiansi/Nyamanoro/Bwiru, Igogo/Butimba, nk.
Faida:
1. Itazipunguzia halmashauri za wilaya ukubwa wa maeneo ya kuhudumia na mzigo wa huduma yenyewe.
2. Tutasogeza huduma karibu zaidi na wananchi, tofauti na ilivyo sasa ambapo halmashauri za miji zinahudumia maeneo makubwa na matokeo yake ufanisi unakuwa kiduchu sana, kama siyo hakuna kabisa.
3. Tutasogeza kwa wananchi vikao vya maaamuzi. Wananchi watachagua viongozi wao wa miji na kufanya maamuzi yatakayoendana na mazingira na utashi wao. Viongozi wataochaguliwa watawajibika kwa wananchi moja kwa moja.
4. Tuasogeza karibu zaidi kwa wananchi upangaji, utekelezaji na usimamizi wa mipango ya maendeleo, tofauti na sasa hivi ambapo uamuzi unafanywa wilayani na wananchi kubaki km watazamaji tu.
5. Tutaongeza ajira. Badala ya kuhudumiwa na kundi dogo la watu wa wilayani, kila mji utakaoanzishwa utaajiri wataalam wake, kwa hiyo watu wengi wataajiriwa.
6. Itasaidia kuweka suala la maendeleo mikononi mwa wananchi wenyewe badala ya kutegemea serikali kuu.
7. Kwa kuwa mwenye kisu kikali ndiye hula nyama, miji itakayoboresha huduma kwa wananchi ndo itakayovutia uwekezaji zaidi na hivyo kupata makusanyo zaidi ya kodi na hivyo kuwa na mapato zaidi.
Hili ni wazo ghafi. Wenajamvi mnasemaje? Na wataalam wa mipango miji mnasemaje?
Jumapili njema.