Napenda kuoa ila sipendi kufanya sherehe

Napenda kuoa ila sipendi kufanya sherehe

Ninapenda sana kufunga ndoa maana ni maagizo kutoka kwa Mungu baba ila sipendi kufanya sherehe naona gharama sana, sasa sijui itakuaje mchumba akitaka sherehe.
Labda ya kimila unaweza fanya kimya kimya. Mimi nilibatiza watoto wangu kanisani, tulivyo kuwa tunatoka mchungaji akanifuata "sherehe mnafanyia ukumbi gani?" Nikamjibu sitafanya sherehe tunarudi nyumbani. Mchungaji alinishangaa baadae alinisema hadi niliona aibu. Sijarudi tena kanisani nina mwaka na miezi juu
 
Labda ya kimila unaweza fanya kimya kimya. Mimi nilibatiza watoto wangu kanisani, tulivyo kuwa tunatoka mchungaji akanifuata "sherehe mnafanyia ukumbi gani?" Nikamjibu sitafanya sherehe tunarudi nyumbani. Mchungaji alinishangaa baadae alinisema hadi niliona aibu. Sijarudi tena kanisani nina mwaka na miezi juu
yap
 
Ninapenda sana kufunga ndoa maana ni maagizo kutoka kwa Mungu baba ila sipendi kufanya sherehe naona gharama sana, sasa sijui itakuaje mchumba akitaka sherehe.

Rafiki! nadhani avator yako hapo inahusika.
Naomba nikushauri kwa Mujibu Biblia ambayo ninaamini ndio unayoiamini, ndoa na harusi ni vitu viwili ambavyo wala havina uhusiano kabisa..

1.Ndoa ni makubaliano ya kuishi kama mume na mke kati ya jinsia mbili tofauti, ili kuwawezesha kutekeleza amri ya Mungu, mkazae na kuijaza nchi,Kasome kitabu cha Musa, Mwanzo.

Pili ni kuweza upambana na tamaa za mwili, Kasome Waraka wa Paulo kwa Wakorinto..

2. Harusi ni sherehe ambayo walioona wanaandaa chakula wanakula na ndugu na marfiki kufurahia na kufahamiana na hayo sio maagizo ya Mungu. Tatizo lililopo sasa hivi ni kwamba harusi inapewa kipaumbele kuliko ndoa, na kwa sababu tumezoea kuchangisha wachangishwaji wana nafasi ya kukontroll ndoa yako. ndio wakijua hakuna pombe wanachanga 10,000.

Nakushauri kama uwezo wa kufanya sherehe wewe huna kafunge ndoa yako, ukimaliza rudi nyumbani andaa chakula cha mchana mle na mwenzako, kama una uweza waalike majirani yako...ila achana kufuata mapokeo ambayo hayana faida yoyote ktk maisha yako,
Nimefunga ndoa 10 years ago na nilifanya harusi ila sikupenda headache ya kukumbizana na michango wala kupoteza muda, niliandaa bajeti niliyoimudu na nikatumia pesa yangu wenyewe almost 90% nikamaliza mchezo na tunafuraha hakuna kudhalilika mtaani eti unaringa wakati mke tumekuozesha sie na harusi tumekuanyia..
ondo woga askari
 
Rafiki! nadhani avator yako hapo inahusika.
Naomba nikushauri kwa Mujibu Biblia ambayo ninaamini ndio unayoiamini, ndoa na harusi ni vitu viwili ambavyo wala havina uhusiano kabisa..

1.Ndoa ni makubaliano ya kuishi kama mume na mke kati ya jinsia mbili tofauti, ili kuwawezesha kutekeleza amri ya Mungu, mkazae na kuijaza nchi,Kasome kitabu cha Musa, Mwanzo.

Pili ni kuweza upambana na tamaa za mwili, Kasome Waraka wa Paulo kwa Wakorinto..

2. Harusi ni sherehe ambayo walioona wanaandaa chakula wanakula na ndugu na marfiki kufurahia na kufahamiana na hayo sio maagizo ya Mungu. Tatizo lililopo sasa hivi ni kwamba harusi inapewa kipaumbele kuliko ndoa, na kwa sababu tumezoea kuchangisha wachangishwaji wana nafasi ya kukontroll ndoa yako. ndio wakijua hakuna pombe wanachanga 10,000.

Nakushauri kama uwezo wa kufanya sherehe wewe huna kafunge ndoa yako, ukimaliza rudi nyumbani andaa chakula cha mchana mle na mwenzako, kama una uweza waalike majirani yako...ila achana kufuata mapokeo ambayo hayana faida yoyote ktk maisha yako,
Nimefunga ndoa 10 years ago na nilifanya harusi ila sikupenda headache ya kukumbizana na michango wala kupoteza muda, niliandaa bajeti niliyoimudu na nikatumia pesa yangu wenyewe almost 90% nikamaliza mchezo na tunafuraha hakuna kudhalilika mtaani eti unaringa wakati mke tumekuozesha sie na harusi tumekuanyia..
ondo woga askari
well said salute
 
Labda ya kimila unaweza fanya kimya kimya. Mimi nilibatiza watoto wangu kanisani, tulivyo kuwa tunatoka mchungaji akanifuata "sherehe mnafanyia ukumbi gani?" Nikamjibu sitafanya sherehe tunarudi nyumbani. Mchungaji alinishangaa baadae alinisema hadi niliona aibu. Sijarudi tena kanisani nina mwaka na miezi juu
Huyo hakuwa mchungaji ni mganga njaa tu huyo...
anaendekeza tumbo na hao ndio wale wanafiki ambao Yesu alikupingana nao sana akiwaeleza wanafuata desturi na mafundisho potofu..
Mie nimebatiza watoto 3 na wala sijawahi fanya sherehe yaaina yoyote wala kubadilisha ratiba yang ya chakula.
Nakushauri usiachane na Mungu wako kwa sababu ya maneno ya mchungaji njaaa...
 
Hata mimi ninakaugonjwa ka kuchukia sherehe.
Mungu akijaalia nikiolewa napenda ndoa iwe simple sana hata kama tutaenda kwa Shekhe atufungishe then tunarudi home kusherehekea na familia naona sawa tu.
Sijui nina tatizo mana sio mpenzi wa sherehe na hata nikialikwa kuhudhuria ni issue.
hata mimi sipendi sherehe kubwa kabisa natamani hata tufunge chumbani tusitoke tena
 
Nilioa wakat nina laki na nusu mfukon,,nilikua na mawazo kama yako lakin kuleta mapendekezo nikakuta baget mil.15 ilihal mm nina laki na nusu,,niliumiza kichwa kichwa lakin mungu alifanya wepes zikapatikana ml 10.2 nikaserebuka sanaaaa kwa michango ya washkaji lakin kilikua kipind cha Mkwere wa Msoga...

Ila kama unaweza oa sherehe sio ndoa..oiga kimya kimya haina shida.. Wewe ndio muoaji sasa kwa nn unaogopa kuambiwa na mpenz wako kwamba akihitaji sherehe?? Mkishindwa kuelewana kabla ya ndoa itakuaje humo ndani
 
Pole. Ila ni kweli hupendi sherehe??,au ni kukosa tu hela. Na hii ni changamoto. Inayofanya vijana wengi wasiwe na wazo la kuoa.
 
Mi nadhan nikihairisha hili suala basi na hixi sherehe zimechangia
 
Me niligomagaa kabisa kufanya vya sherehe na mwenzangu tukakubaliana lakin hilo swala nilipolifikisha kwa wazee nikaambiwa kaa kushoto tafuta mahari na mavazi yetu vikao vikaanza mbelen nikajikuta na mimi nishaingiamo japoo ilikuwa kimbinde lakin mambo yalikwenda mujarabu MUNGU akatenda tukamaliza salama lakin asikwambie mtuu alafu ukute mwanamke mwenyewe anataka mambo shazi utajuuta
 
Hata mimi ninakaugonjwa ka kuchukia sherehe.
Mungu akijaalia nikiolewa napenda ndoa iwe simple sana hata kama tutaenda kwa Shekhe atufungishe then tunarudi home kusherehekea na familia naona sawa tu.
Sijui nina tatizo mana sio mpenzi wa sherehe na hata nikialikwa kuhudhuria ni issue.
Kumbe we bado! Ngoja nije nifanye nusra
 
Binafsi hata mimi ishu za sherehe dizaini zimenikalia kushoto hasa ukifikiria kuchangisha watu hapo ndo hamu inanitoka kabisa. Plan zangu ntapokuja kuoa atleast 60% ya gharama zitoke mfukoni kwangu hapo ntakuwa na amani na sherehe, hata ntao waalika watakuwa ndugu na marafiki na majirani wale wakaribu tu
 
Mi nitaoa ila sherehe hapana aisee..nikiona mwanamke anahusudu sherehe sana naanza kukaa naye mbali!
 
sherehe inafanyiwa according na uwezo ulonawo ila sasa tuna spend pesa kibao sabb ya shereh za ndoa sbb ya watu kuiga kizungu na kutupilia mbal mafunzo ya dini ,ndo mana watu wengin kuoa inakua ngumu saana akiwaza kuhs sherehe sbb una amrishwa kufany kitchen party,,....
 
Ndoa ni ile ibada mkuu mengine ni kuifurahisha dunia tu
 
Back
Top Bottom