Wadau
Leo mida ya mchana Mhesh Nape Nnauye alipita maeneo ya soko kuu Arusha karibu na kijiwe cha kahawa maarufu kwa makada wa chadema.
Kilichonifurahisha akiwa ndani ya gari lake makada hao wa chadema bila uoga walimfuata kumsalimia na kisha kumuomba Kada huyo wa CCM angalau awapatie hela kidogo kwa ajili kahawa na kashata.Bila kusita wala kujali itikadi tena kwa moyo wa ubinadamu na kuzingatia hali zao Mhesh Nape aliwapatia vijana hao hela kidogo kisha kuendelea na safari yake.Naamini Mhesh Nape alikuwa kwenye majukumu mazito yakichama lakini aliona nivema tena kwa busara kubwa atumie muda huo mfupi angalao kuwasikiliza na kuwasaidia makada hao wa Chadema.
Ukweli jambo hili ulilolifanya limenifurahisha sana kwani limeonyesha kuwa kwa CCM siasa sio uadui bali maendeleo. Kwa siku ya leo kumekuwa na utulivu eneo hilo na upendo umetawala.
Hongera sana Kada wa Chama cha Mapinduzi na Mbunge wa Mtama.
Karibuni.