Shenkalwa
JF-Expert Member
- May 3, 2011
- 580
- 132
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) itikadi na uenezi ya chama cha mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema ipo haja sasa kujadili kwa kina namna ya kupunguza tofauti kubwa ya kipato iliyopo kati ya maskini na matajiri kwani ni hatari kwa amani ya nchi.
Alisema hayo kwenye viwanja vya Sokoni Igoma jijini Mwanza wakati akihutubia mkutano ulioandaliwa na ccm katika ziara ya baadhi ya viongozi wa chama hicho mkoani hapa.
Nape alisema nchi nyingi duniani zimekuwa zikikumbwa na machafuko kutokana na kuachiwa kukua kwa tofauti kubwa ya kipato kati ya maskini ambao ndio wengi na matajiri wachache.
"ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji...Heri kuziba ufa kuliko kujenga ukuta. Ni muhimu leo wapenda amani wa nchi hii tujadili kwa kina namna bora ya kupunguza tofauti kubwa ya kipato nchini kwani ikiachwa hivi baada ya muda nchi hii itachafuka," alisema Nape.................."
Source: NIPASHE October 20, 2011.
Huyu jamaa sijui kama anaelewa anachokiongea naona mimi nashindwa kumpata kabisa. Sio katika mkutano huo tu lakini maneno anayoyaongea katika mikutano yake mingi simuelewi analenga nini.
Ukichukulia kwa mfano watu aliokuwa anaongea nao huko Igoma, Mwanza kwenye viwanja vya sokoni ni hao maskini na walala hoi ambao kwa namna yeyote maneno hayo ya nape hayawasaidii zaidi ya kupoteza muda wao kumsikiliza.
Mimi kwa mawazo yangu niliona bora angeliongea maneno hayo kwenye mikutano ya viongozi wenzake wa magamba kwa sababu wao ndio wanaoipeleka nchi hii kubaya, ndio mafisadi, ndio waliosababisha hilo pengo kati ya matajiri/mafisadi na masikini walalahoi. Hao ndio wanaotakiwa watafute namna ya kurekebisha mambo, kuinua uchumi wa wananchi na kuwafunga mafisadi na wezi wa mali ya umma wote.
Yeye na chama chao ndiyo walioifilisi nchi hii kwa kujilimbikizia mali ndani na nje ya nchi hii pamoja na kujijali wenyewe na familia zao na kuwaacha walio wengi wakitaabika kwa mlo mmoja kwa siku.
Sasa leo anakwenda kuwaambia walalahoi wa igoma Mwanza maneno hayo ambayo hayawasaidii. Tena naona kwao ni kama kejeli. Sijui kama huyu bwana mdogo ana uwezo kweli wa nafasi aliyopewa na magamba wenzake.
Alisema hayo kwenye viwanja vya Sokoni Igoma jijini Mwanza wakati akihutubia mkutano ulioandaliwa na ccm katika ziara ya baadhi ya viongozi wa chama hicho mkoani hapa.
Nape alisema nchi nyingi duniani zimekuwa zikikumbwa na machafuko kutokana na kuachiwa kukua kwa tofauti kubwa ya kipato kati ya maskini ambao ndio wengi na matajiri wachache.
"ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji...Heri kuziba ufa kuliko kujenga ukuta. Ni muhimu leo wapenda amani wa nchi hii tujadili kwa kina namna bora ya kupunguza tofauti kubwa ya kipato nchini kwani ikiachwa hivi baada ya muda nchi hii itachafuka," alisema Nape.................."
Source: NIPASHE October 20, 2011.
Huyu jamaa sijui kama anaelewa anachokiongea naona mimi nashindwa kumpata kabisa. Sio katika mkutano huo tu lakini maneno anayoyaongea katika mikutano yake mingi simuelewi analenga nini.
Ukichukulia kwa mfano watu aliokuwa anaongea nao huko Igoma, Mwanza kwenye viwanja vya sokoni ni hao maskini na walala hoi ambao kwa namna yeyote maneno hayo ya nape hayawasaidii zaidi ya kupoteza muda wao kumsikiliza.
Mimi kwa mawazo yangu niliona bora angeliongea maneno hayo kwenye mikutano ya viongozi wenzake wa magamba kwa sababu wao ndio wanaoipeleka nchi hii kubaya, ndio mafisadi, ndio waliosababisha hilo pengo kati ya matajiri/mafisadi na masikini walalahoi. Hao ndio wanaotakiwa watafute namna ya kurekebisha mambo, kuinua uchumi wa wananchi na kuwafunga mafisadi na wezi wa mali ya umma wote.
Yeye na chama chao ndiyo walioifilisi nchi hii kwa kujilimbikizia mali ndani na nje ya nchi hii pamoja na kujijali wenyewe na familia zao na kuwaacha walio wengi wakitaabika kwa mlo mmoja kwa siku.
Sasa leo anakwenda kuwaambia walalahoi wa igoma Mwanza maneno hayo ambayo hayawasaidii. Tena naona kwao ni kama kejeli. Sijui kama huyu bwana mdogo ana uwezo kweli wa nafasi aliyopewa na magamba wenzake.