Nape sasa amtaka Mbowe ajiuzulu

Nape sasa amtaka Mbowe ajiuzulu

Shinyanga.Katibu
wa Itikadi na
Uendezi wa Chama Cha mapinduzi (CCM),Nape Nnauye amemtaka Kiongozi wa
Upinzani Bungeni,Freeman Mbowe kujiuzulu nafasi hiyo mara moja kwa
sababu ameshindwa kuiongoza kambi hiyo.

Wito huo uliutoa mjini hapa Ijumaa jioni
alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara wa kuhitimisha ziara ya siku
Nne ya Katibu Mkuu wa Chama hicho, Abdulrahman Kinana katika mkoa huo.

Nape alisema vurugu zilizotokea hivi
karibuni Bungeni ni uthibitisho wa wazi kuwa,Mbowe ameshindwa kuiongoza
kambi hiyo kwa kuwa kabla yake hakukuwahi kuonekana fujo na vurugu
kama hizo katika chombo hicho kinachoheshimika.

Alisema udhaifu wa Mbowe katika
kuiongoza kambi hiyo ndiyo unaosababisha ishindwe kufanya kile ambacho
Watanzania wanakitarajia kutoka kwa wapinzani.

Alisema wanasiasa ambao wanasababisha na
kushabikia fujo na vurugu hawafai kwa madai kuwa wanaipeleka nchi
mahali pabaya.

Hata hivyo, alisema hilo halitafanikiwa
kwa sababu Serikali, CCM na Watanzania wapo makini dhidi ya mtu yeyote
anayepanga kuwachonganisha. Aliishangaa Chadema kwa kushinikiza wabunge
waongezwe kwenye Bunge la Katiba huku ikitaka wengi wa hao watokane na
wanasiasa.

“Chadema inataka wawakilishi wa wakulima
wawe kumi tu wakati wakulima ni asilimia 80 ya Watanzania wote. Hivi
kweli wana lengo la kuwatetea Watanzania au maslahi binafsi
tu,?”alihoji Nape.N

nape waliwataka wananchi kufanya uamuzi
wa busara wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na Uchaguzi
Mku

Huyu nape anajifanya hajui kwamba upinzani ktk kipindi kilichopita
hawakuwa na nguvu kama ilivyo sasa. Kwa issue ya kujiuzulu, atajiuzulu yeye
kwanza. AMA KWELI NYANI HAONI KUNDULE.
 
Nape aliyasema haya akiwa mbele ya mfadhili wao balozi wa China si ndiyo?
 
Naunga mkono hoja. Mh. Mbowe ajiuzulu haraka sana.

Ajiuzulu kwani alipewa cheo chake kwa hisani kama vuvuzela?sometimes uelewa wa watu una walakini, muulzen ****** ana matatzo yepi kila akikalia kiti mizozo hutokea, na hata wapinzan walipotoka bungeni kiti kiliruhusu wabunge wa magamba kuwajadili wabunge walotoka na kuhitimisha kwa kuunga mkono hoja bila kujadili rasimu iliyo mbele yao, je hiyo ndo busara?think twice ndugaaaay ni mvurugaji anayewaua magamba a slow but sure death, nyie chekeleeni but mzee 6 aliwasaidia sana kurudsha imani kwa wananchi but for now kasi mnayotetereka nayo inatisha
 
Lakini siku anaondoka mbowe madarakani labda cdm ife kwamba kile chama ni chake hakuna mtu wa kumwambia kitu ndani na nje ya chadema ,jamani cdm ni ya mbowe.

Mdomo ni mali yako mkuu, so you can as well use it as a pit latrine
 
Ajiuzulu kwanza ndugai kwa kulifanya bunge la wananchi kuwa kijiwe cha ccm!
 
Shinyanga.Katibu wa Itikadi na Uendezi wa Chama Cha mapinduzi (CCM),Nape Nnauye amemtaka Kiongozi wa Upinzani Bungeni,Freeman Mbowe kujiuzulu nafasi hiyo mara moja kwa sababu ameshindwa kuiongoza kambi hiyo.

Wito huo uliutoa mjini hapa Ijumaa jioni alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara wa kuhitimisha ziara ya siku Nne ya Katibu Mkuu wa Chama hicho, Abdulrahman Kinana katika mkoa huo.

Nape alisema vurugu zilizotokea hivi karibuni Bungeni ni uthibitisho wa wazi kuwa,Mbowe ameshindwa kuiongoza kambi hiyo kwa kuwa kabla yake hakukuwahi kuonekana fujo na vurugu kama hizo katika chombo hicho kinachoheshimika.

Alisema udhaifu wa Mbowe katika kuiongoza kambi hiyo ndiyo unaosababisha ishindwe kufanya kile ambacho Watanzania wanakitarajia kutoka kwa wapinzani.

Alisema wanasiasa ambao wanasababisha na kushabikia fujo na vurugu hawafai kwa madai kuwa wanaipeleka nchi mahali pabaya.

Hata hivyo, alisema hilo halitafanikiwa kwa sababu Serikali, CCM na Watanzania wapo makini dhidi ya mtu yeyote anayepanga kuwachonganisha. Aliishangaa Chadema kwa kushinikiza wabunge waongezwe kwenye Bunge la Katiba huku ikitaka wengi wa hao watokane na wanasiasa.

"Chadema inataka wawakilishi wa wakulima wawe kumi tu wakati wakulima ni asilimia 80 ya Watanzania wote. Hivi kweli wana lengo la kuwatetea Watanzania au maslahi binafsi tu,?"alihoji Nape.N

nape waliwataka wananchi kufanya uamuzi wa busara wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na Uchaguzi Mku

Labda ni kweli Mbowe anatakiwa kujiuzulu! Labda......

Ila mimi nadhani kuganga njaa baada ya kukosa mwelekeo ni tatizo, hasa kwa mustakabali wa siasa za nchi yoyote. Katika nchi zenye kujali maana, kiongozi huwa ni zao la hekima, busara na uchapakazi kati ya sifa nyingine. Ni Tanzania tu ambapo kiongozi anaweza kupatikana kwa kujipendekeza na kuwa mtumwa wa kutekeleza matakwa ya "wakubwa". Vinginevyo binafsi sioni ni kwa vipi chama chochote (on earth) kinaweza kumudu kuwa na viongozi aina ya Nape na Mwigulu type na bila haya bado wakajiona salama.

Kwa wanaomjua Nape, ni wazi wanajua ni mtu ambaye hana hoja. Kila atakaposikika lazima aropoke kama ametoka usingizini bila kujali anayoyasema yana athari gani kwake na chama chake. Sijui ni nani aliyesema propaganda ni kuropoka!

Kama hoja ni Mbowe kujiuzulu kwa sababu kipimo cha vurugu kimemchuja then nafikiri kabla ya kuropoka hilo angepaswa kuangalia ni wangapi katika chama chake wanapaswa kuanza kujiuzulu (Nadhani huko kumekuwa na historia za bifu matusi na nusura za kushikana mashati (magauni) Sioni kama ni lazima kusema majina hapa. Sasa kama hiyo sababu inatosha, nadhani Nape alikuwa anampasha Mwenyekiti wake kuwa kama kumetokea mambo hayo anapaswa kujiuzulu nafasi yake.

Kama ni kujiuzulu mimi naona listi ndefu ya waliopaswa kujiuzulu. Ntatoa mifano michache:

1. Sioni ni kwa nini Nape asijiuzulu kwa kuwadanganya wananchi mara kibao ikiwemo ile "vua gamba ya siku 90" ambayo umekuwa miaka sasa na hakujavuliwa hata kucha moja! Hii ni sawa na kusema CCM inawajua kwa majina wanofisidi mali ya taifa na kwa kuwaonea aibu, au kwa kukosa sauti ( kwa kuwa wengi wameoza) wameamua kupotezea kwani kumgusa mtu ni kufungua "sanduku la pandora"

2.Spika wa bunge na Naibu wake wanapaswa kujiuzulu kwa kushindwa kusimamia haki na utawala wa sheria bungeni, hivyo kuliingiza bunge katika aibu na vurugu za mara kwa mara. Vinginevyo wawaeleze wananchi ni kwa nini haya yatokee kwao tu na siyo kwa kina Msekwa , Sapi au Sita.

3.Mawaziri waliofeli kama kina Maghembe, Malima na wenzao waunge listi kwa kusababisha maafa ya kuanguka jumla kwa elimu nchini na kuweka rehani amani ya nchi. Mathalan kiongozi kama Nchimbi anapaswa, pamoja na kujiuzulu, kujipeleka mwenyewe the Hague kwa kuangalia, kusimamia na kusababisa mauaji ya raia huku kwa nguvu zote akiwalinda na kuwapandisha vyeo wanaohusika, bila kusahau matukio ya kulipuka mabomu kwenye kambi za jeshi na ahadi ya kujiuzulu yakirudia.(jambo lililotokea Mbagala na hajajiuzulu)

4.Mwenyekiti wa CCM taifa anapaswa kujiuzulu kwa kukubali kuhubiri ilani zisizotekelezeka za chama chake, na kuwalinda mafisadi amabao ushahidi upo wa kutosha kuhusu kuhusika kwao. Kama rais ni vema akajiuzulu kw akushindwa kwa serikali yake, kusimamia maazimio na malengo muhimu hivyo kuongeza ugumu na kupanda kwa gharama za maisha, huku kukiwa na ongezeko la upotevu wa maliasili za taifa, ufisadi uliokithiri, kuongezeka kwa vitendo vya rushwa na kushuka kwa elimu nchini. Maisha ya raia yamezidi kuwa ya wasiwasi huku wengi wakishindwa hata kujua kesho wataishije.

Kwa kuhitimisha, sidhani kama ndani ya CCM kuna mtu mwenye sauti isiyo na unafiki ya kuwaambia wananchi ni nani ajiuzulu na nani msafi. Nape anapaswa kuonywa kuacha unafiki na kupiga kelele kwa kujipendekeza kwa wakubwa, badala yake ajikite kujenga heshima yake iliyoporomoka kwani hata baada ya CCM na CHADEMA kupita TANZANIA itaendelea itakuwepo na Nape na wajukuu zake watakuwepo, hivyo ni vizuri kujenga historia ya weledi na heshima. historia amabayo wanaofuata wataona fahari kuisoma na kuisimulia.
 
Gazeti la mwananchi la leo lina kicwa cha habari kinasomesomeka "NAPE SASA AMTAKA MBOWE AJIUZULU"
Kwa mtizamo wangu Nape ni sawa na debe tupu ambalo kwa asili yake haliachi kuvuma!!

Ningemshauri Nape kuondoa boriti katika jicho lake kwanza kabla hajaangalia Kibanzi kilichopo kwenye jicho la jirani yake. (Mbowe)

Hivi kwa akili yake na uelewa wake Nape anafikiri kile alichokifanya Job Ndugai naibu speaker kinastahili kufumbiwa macho na badala yake kuangalia tuu upande wa mh. Mbowe? Hebu tujiulize ka-swali kadogo tu. hivi kweli kwa Job kama mwenyekiti ilihitajika busara kiasi gani kwake kumruhsu Kiongozi mkuu wa kambi ya upinzani kuongea alichotaka kuongea? Au ni kwasababu alikuwa na uhakika kile alichotaka kuzungumza mh. Mbowe kilikwa mwiba kwa yake maamuzi na makubaliano yao kwenye vikao nyao vya ndani kuwa Job ahakikishe kwa kadri awezavyo kuto ruhusu kabisa mbunge yeyote yule anayeweza kuwafungua Watanzania macho kuhusu ukweli wa yale mabovu yaliyokuwa yamefanywa na chama chako na serikali yako katika mchakato huu muhimu wa katiba ya Watanzania walio ccm na wale wasio ccm? Nape nakukumbusha kuwa katiba tunayoindaa leo haikuwepo kwenye sera za chama chako na haikuwahi kuwa sera ya CCM kuwa na katiba mpya coz CCM mnajua fika nini gharama za kuwa nakatiba Mpya na nzuri. Nasema mnajua kwasababu hakuna kilichojificha kuwa uwepo wa katiba mpya unatishia mustakabali wa chama chako kuendelea kuwa madarakani. Wakati huohuo uwepo wa katiba nzuri inayojibu matakwa ya wananchi ni mwanzo mzuri wa nchi yetu kuendelea na wananchi wengi kuishi maisha ya daraja la kwanza tofauti na ilivyo sasa wanaoifaidi keki ya taifa ni kikundi cha watu wachache wenye nyadhifa za kisiasa.
Nakukumbusha Nape ushughulike na serikali ya chama chako ilipolifikisha taifa letu kwa sasa. Angalia tatizo la madawa ya kulevya, angalia ufisadi uliokithiri, angalia tatizo la elimu nchini, Rushwa inavyonuka kila mahali polisi wanavyowanyanyasa raia, mabomu yanayoua waandishi wa habari na wananchi wa kawaida nk. Haya ndiyo ungewaambiwa wahusika kina shukuru kawambwa, Hosea na hatimaye mwenyekiti wako wa chama ambaye ndiye raisi


Hebu mwogepe Mungu na uwe na angalau kabusara kidogo utalinda utu wako. Watanzania wa leo siyo mbumbumbu kama wale wa "zidumu fikra za mwenyekiti wa chama"



Think!
 
Hana lolote ajiuzuru hajawai hata kutoa hoja yenye akili mjengoni sembuse kuiongoza kambi yenye vichwa vya kutosha
 
Kaishiwa hoja na kashindwa kuliongoza lichama lake lililokosa mwelekeo na sasa anaingilia visivyomhusu
 
Chama kilichoko madarakani kuzungumza katika maneno mia moja lazima kitaje chama cha upinzani(kimoja kati ya vingi) mara sabini ni dalili mbaya sana. Kwani hao walioichagua CCM walifanya hivyo ili ipambane na Chadema? Uchaguzi umekwisha mpo madarakani,yale muliyoahidi mumeshindwa kuyatekeleza sasa mnataka kiongozi wa upinzani ajiuzulu. Kwani yeye ndiye anayesababisha CCM ishindwe kutoa huduma za Afya,Elimu, kudhibiti dhuluma,tatizo la madawa ya kulevya nk nk?
Badala ya kusimama jukwaani na kutumia muda kidogo alionao kuelezea mafanikio ya serikali yao na jinsi ya kukabiliana na changamoto zilizopo kwa mbinu mpya wao agenda ni CHADEMA. Hii kweli ni akili? Hata mkeo(kwa wanaume tu) akiona badala ya kila siku kuzungumzia njia za kutatua matatizo yenu ya ndani wewe unamzungumzia jirani ambaye kuna tetesi kuwa anamwinda mkeo basi ujue umeumia. Onyesha utatuzi wa shida zenu sio kujikita na habari za mpinzani wako maana utakuwa wewe ndio unampandisha chati ya ubora na wewe kuonyesha udhaifu wako.
 
Utarajie nini kutoka kwa kiumbe aliyejaza minyoo tumboni akijidanganya ni kitambi!, Tumsamehe bure tu huyu kwani siku ikimuisha minyoo aliyojaza tumboni ile na hatimaye tumbo kurejea ktk hali ya kawaida na akili zake zitatengamaa.
 
Naunga mkono hoja. Mh. Mbowe ajiuzulu haraka sana.

Mbowe will never make it to statemanship.
Kubishana bungeni na kuongoza fujo imemharibia sifa ya kuwa cool headed in times of crisis.

CHADEMA imeanza kuwa reduced to a party of liquor and illicit puff smoking representatives who use more brawn tha brain in the august House.
 
Back
Top Bottom