Deus F Mallya
JF-Expert Member
- Jul 28, 2011
- 705
- 440
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana Siasa za Tanzania tangu mwaka 2004 hadi sasa. Kwa kawaida kwenye vyama vya Siasa kuna watu 'Potential' ambao huwa kwenye 'Big five'. Leo nimelazimika kuuliza kama Nape Moses Nnauye anategemewa na CCM kwa kiasi gani? Yupo kwenye 'Big five' au hata 'Top ten'??.. Kwa wanaowafahamu na kufuatilia kwa karibu siasa za CCM (Political Obsevers) naomba tushirikiane hapa.
NAPE NNAUYE ni Mwanasiasa Kijana ambaye awali alijipambanua kuwa anaweza kukinyoosha chama na kurejesha Imani za Watanzania. Huyu kwa sasa ni Katibu wa Itikadi na Wenezi CCM. Tangu alipopata nafasi hiyo amekuwa akifanya kinyume na pengine akimeza maneno yake mara kadhaa. Tujikumbushe: Utekelezaji wa Azimio la Kujivua gamba,hoja ambayo alizunguka nayo sehemu kadhaa akiwaambia wananchi kuwa mafisadi watafukuzwa ndani ya siku 90. Baadaye akameza maneno yake mbele ya waandishi wa habari. Nape amekuwa akiitolea serikali majibu ya hoja mbalimbali (Hoja ambazo zilitakiwa kujibiwa ama na BoT,Wizara na Ikulu).
Nape ni kama amezidiwa na nguvu ya watu anaowaongoza ndani ya chama. Nape amekuwa akisubiri Viongozi wakuu wa CHADEMA waituhumu Serikali ya CCM ndo ajibu tena kwa ujasiri wa ajabu. Pengine ndiyo kazi ya Itikadi na uenezi CCM??.. Huku akiwekeza nguvu zote na za bosi wake kuiangalia CHADEMA kwa jicho la kengeza,CCM imekuwa ikiendelea kushindwa kwenye Chaguzi ndogo na pale inapowezekana wanacheza rafu kama Igunga... Pia Wanachama zaidi ya 800,000 wamejiunga na CHADEMA kwa kipindi kifupi sana.. Pamoja na kuwa nilijua CCM itakufa kabla ya mwaka 2015 lakini sikutegemea ife kifo cha gafla kiasi hiki.
Nawasilisha!
NAPE NNAUYE ni Mwanasiasa Kijana ambaye awali alijipambanua kuwa anaweza kukinyoosha chama na kurejesha Imani za Watanzania. Huyu kwa sasa ni Katibu wa Itikadi na Wenezi CCM. Tangu alipopata nafasi hiyo amekuwa akifanya kinyume na pengine akimeza maneno yake mara kadhaa. Tujikumbushe: Utekelezaji wa Azimio la Kujivua gamba,hoja ambayo alizunguka nayo sehemu kadhaa akiwaambia wananchi kuwa mafisadi watafukuzwa ndani ya siku 90. Baadaye akameza maneno yake mbele ya waandishi wa habari. Nape amekuwa akiitolea serikali majibu ya hoja mbalimbali (Hoja ambazo zilitakiwa kujibiwa ama na BoT,Wizara na Ikulu).
Nape ni kama amezidiwa na nguvu ya watu anaowaongoza ndani ya chama. Nape amekuwa akisubiri Viongozi wakuu wa CHADEMA waituhumu Serikali ya CCM ndo ajibu tena kwa ujasiri wa ajabu. Pengine ndiyo kazi ya Itikadi na uenezi CCM??.. Huku akiwekeza nguvu zote na za bosi wake kuiangalia CHADEMA kwa jicho la kengeza,CCM imekuwa ikiendelea kushindwa kwenye Chaguzi ndogo na pale inapowezekana wanacheza rafu kama Igunga... Pia Wanachama zaidi ya 800,000 wamejiunga na CHADEMA kwa kipindi kifupi sana.. Pamoja na kuwa nilijua CCM itakufa kabla ya mwaka 2015 lakini sikutegemea ife kifo cha gafla kiasi hiki.
Nawasilisha!